Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb23 Mei uku. 3
  • Uwe na Maoni Kama ya Yehova Kujihusu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uwe na Maoni Kama ya Yehova Kujihusu
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2023
  • Habari Zinazolingana
  • Maamuzi Yanayoonyesha Unamtegemea Yehova
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2023
  • Uwe Mwenye Kiasi Inapohusu Mambo Usiyoyajua
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2025
  • Kubali Upendo wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2025
  • Yehova “Huwaponya Waliovunjika Moyo”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2023
mwb23 Mei uku. 3

MAISHA YA MKRISTO

Uwe na Maoni Kama ya Yehova Kujihusu

“Yehova anawafurahia watu wake.” (Zb 149:4) Ingawa sisi si wakamilifu, anaona sifa zetu nzuri na uwezo tulio nao. Hata hivyo, pindi fulani huenda ikawa vigumu kwetu kuwa na maoni kama hayo yenye usawaziko kujielekea. Huenda tukahisi kwamba hatufai kwa sababu ya jinsi wengine wanavyotutendea. Au, ikiwa tutakazia fikira makosa tuliyofanya wakati uliopita, huenda tukawa na shaka ikiwa kweli Yehova anatupenda. Ni nini kinachoweza kutusaidia tunapohisi hivyo?

Kumbuka kwamba Yehova anaona mambo ambayo wanadamu hawawezi kuona. (1Sa 16:7) Hilo linamaanisha kwamba anafahamu mambo ambayo hata sisi wenyewe hatufahamu kujihusu. Inapendeza kwamba Biblia inatusaidia kuelewa maoni ya Yehova kutuhusu. Tunaweza kuelewa maoni yake tunapochunguza mistari na masimulizi ya Biblia yanayofunua jinsi Yehova anavyowapenda waabudu wake.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA UHAKIKISHIE MOYO WAKO MBELE ZA YEHOVA, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Mfano wa mkimbiaji na baba yake unatufundisha nini kuhusu jinsi Yehova anavyotuona?

  • Mtu aliyetenda dhambi nzito anapochukua hatua za kurekebisha uhusiano wake na Yehova, anaweza kufanya nini ili kuuhakikishia moyo wake mbele za Yehova?—1Yo 3:19, 20

  • Ndugu huyo alinufaikaje kwa kusoma na kutafakari masimulizi ya Daudi na Yehoshafati?

Masimulizi ya Biblia yanayotuhakikishia kwamba . . .

Yehova anatupenda hata iwe wengine wana maoni gani kutuhusu

  • Enoko (Mwa 5:24; Ebr 11:5; Yud 14, 15)

  • Hana (1Sa 1:1–2:11, 18-21, 26)

Yehova huwasamehe kabisa watenda dhambi wanaotubu

  • Manase (2Nya 33:1-7, 12, 13)

  • Paulo (1Ti 1:12-16)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki