MAISHA YA MKRISTO
Mpango wa Kuwafariji Wale Walio Betheli
Kila mtu hupatwa na majaribu na anahitaji faraja na utegemezo. Hata wale ambao wana nguvu kiroho au wana mapendeleo ya pekee ya utumishi wanaweza kuvunjika moyo. (Ayu 3:1-3; Zb 34:19) Tunaweza kujifunza nini kutokana na mpango wa kuwafanyia uchungaji washiriki wa familia ya Betheli?
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA “MTEGEMEE MUNGU,” KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Washiriki wa familia ya Betheli wanakabili matatizo gani?
Ni mambo gani manne yanayofanywa ili kuwafariji?
Kuwafariji wengine kumewasaidiaje ndugu wanaoandaa faraja?