Utangulizi
Je, unatamani kuishi katika ulimwengu usiokuwa na vita au ukatili? Watu wengi wanafikiri kwamba jambo hilo ni zuri, lakini lisilowezekana. Biblia inaeleza kwa nini jitihada za wanadamu za kukomesha vita hazifanikiwi. Pia, inaeleza sababu zinazotusaidia kuwa na uhakika kwamba inawezekana kuwa na amani ulimwenguni pote na hilo litatokea hivi karibuni.
Katika gazeti hili, maneno “vitaʺ na “ukatiliʺ yanarejelea mapigano kati ya vikundi vilivyo na silaha ili kutatua mizozo ya kisiasa. Majina ya baadhi ya watu walionukuliwa yamebadilishwa.