Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb15 uku. 118-uku. 119 fu. 4
  • “Nilipambana Kama Simba”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Nilipambana Kama Simba”
  • 2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Habari Zinazolingana
  • Kweli Hugeuza Maisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • “Mimi Ni Macho Yake Naye Hutumika Kama Miguu Yangu”
    Amkeni!—1992
  • Tunahitaji Faraja
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Baba Ambaye Watoto Wanahitaji
    Amkeni!—2004
Pata Habari Zaidi
2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb15 uku. 118-uku. 119 fu. 4

JAMHURI YA DOMINIKA

“Nilipambana Kama Simba”

Luis Eduardo Montás

  • ALIZALIWA 1906

  • ALIBATIZWA 1947

  • HISTORIA FUPI Aliyekuwa ofisa katika chama cha kisiasa cha dikteta Rafael Trujillo. Alijifunza kweli ya Biblia na kumtumikia Yehova kwa uaminifu hadi alipokufa mwaka wa 2000.

Picha katika ukurasa wa 118

LUIS, mtu wa ukoo wa Trujillo alikuwa mweka-hazina wa chama tawala cha Partido Dominicano (Chama cha Dominika). Hata hivyo, Luis alikichukia kikundi cha kisiasa cha Trujillo na mara kwa mara alijaribu kuacha kazi yake, lakini dikteta hakumruhusu.

Trujillo alipowaua kaka wawili wa Luis, Luis alijaribu mara mbili kumuua dikteta huyo. Hata hivyo, watu hawakujua kwamba Luis alihusika. Luis alienda kwa watu wanaowasiliana na pepo ili apate msaada wa kumuua mtu huyo, ambaye alisema: “Alitenda kama mnyama na kujiona yuko juu ya kila mtu.” Katika mojawapo ya nyumba za watu waliowasiliana na pepo aliona mezani kitabu “The Truth Shall Make You Free” na akaanza kukisoma. Luis alikipenda sana kitabu hicho hivi kwamba akaenda nacho nyumbani na akafikia mkataa kuwa hiyo ndiyo dini ya kweli aliyokuwa akitafuta.

Luis aliposafiri kwenda Ciudad Trujillo, alihudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova na kuchukua vitabu na magazeti mengi. Alisoma machapisho hayo usiku kucha kisha akaomba afundishwe Biblia. Alipozidi kufanya maendeleo, Luis aliamua kujiuzulu katika serikali ya Trujillo. Dikteta alipojua hilo, alimpa cheo kikubwa cha kuwa balozi wa Dominika nchini Puerto Riko. Lakini Luis alikataa kazi hiyo ingawa alijua kwamba uamuzi wake ungefanya ateswe.

Luis alisema hivi: “Niliteswa kwa kila njia, na serikali iliniwekea mitego ya kila aina. Lakini niliazimia kuachana na maisha ya ulimwengu huu.” Luis akawa mhubiri jasiri wa habari njema hivi kwamba makasisi Wakatoliki katika eneo aliloishi wakaanza kumwita “mhubiri.” Oktoba 5, 1947, miezi sita baada kuhudhuria mikutano kwa mara ya kwanza, Luis alibatizwa.

Baada ya kubatizwa Luis alitafutwa, akafungwa gerezani katika seli ya upweke. Walijaribu kumkamata mara nyingi. Hata hivyo, kila mara alipokamatwa na kupelekwa mahakamani, alitumia fursa hiyo kutoa ushahidi. “Nilipambana kama simba ili kuitetea imani yangu,” alisema Luis, “na ninakumbuka mambo hayo kwa shangwe.”

Rekodi nzuri ya Luis ya kumtumikia Mungu kwa uaminifu ilitambuliwa katika jamii. Mwaka wa 1994, gazeti El Siglo la Dominika lilisema hivi kumhusu Luis: “Bw. Luis Eduardo Montás anatambuliwa huko San Cristobal kuwa mwenye kuchukua mambo kwa uzito. Alitumia vipawa vyake kuwasaidia watu, mwanaume mpole na mwenye huruma. Kila kitu kinachojulikana kumhusu katika historia ya San Cristobal kinahusiana na ujitoaji wake akiwa mwanaume Mkristo.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki