Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb15 kur. 4-7
  • Barua Kutoka Baraza Linaloongoza

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Barua Kutoka Baraza Linaloongoza
  • 2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Habari Zinazolingana
  • Njia za Kupanua Huduma Yako
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Mashahidi wa Yehova—Ripoti ya Kitabu-Mwaka 1994
    1994 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Idara ya Ulimwenguni Pote ya Usanifu-Majengo na Ujenzi
    2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Fuliza Kuzaa Matunda Kwa Uvumilivu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
Pata Habari Zaidi
2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb15 kur. 4-7
Picha ya ukurasa mzima katika ukurasa wa 5

Barua Kutoka Baraza Linaloongoza

Ndugu na Dada Wapendwa:

“Sikuzote sisi humshukuru Mungu tunapowataja ninyi nyote katika sala zetu, kwa maana daima sisi hukumbuka akilini kazi yenu ya uaminifu na kazi yenu ya jasho yenye upendo na uvumilivu wenu kwa sababu ya tumaini lenu katika Bwana wetu Yesu Kristo mbele za Mungu wetu na Baba.” (1 The. 1:2, 3) Maneno hayo yanaonyesha vizuri sana jinsi tunavyohisi kuwahusu! Tunamshukuru sana Yehova kwa kazi nzuri mnayotimiza. Kwa nini?

Mwaka uliopita, mlifanya kwa bidii ‘kazi ya uaminifu’ na ‘kazi ya jasho’ ili kuunga mkono Ufalme. Wengi wenu mmepanua huduma yenu kwa njia mbalimbali. Baadhi yenu mmehamia katika nchi za kigeni, ili kujitolea katika maeneo yenye uhitaji mkubwa wa waeneza-injili wa Ufalme. Wengine mmepanua utumishi wenu kwa kushiriki katika mahubiri ya hadharani. Wengi wenu mmechochewa kuwa mapainia wasaidizi wakati wa majira ya Ukumbusho, mwezi wa ziara ya mwangalizi wa mzunguko, au wakati wa kampeni ya pekee ya mwezi Agosti 2014. Ingawa hali zenu zinatofautiana, tunaona kwamba mnamtumikia Yehova kwa nafsi yenu yote, na tunawapongeza kwa hilo. (Kol. 3:23, 24) Kwa kweli, “kazi yenu ya uaminifu” inatupa sababu ya kumshukuru Yehova!

Pia, tunathamini sana kwa “kazi yenu ya jasho” kuhusiana na miradi mbalimbali ya ujenzi wa majengo ya kitheokrasi ulimwenguni pote. Tuna uhitaji mkubwa wa majengo hayo, kwa sababu idadi ya watu wa Yehova inaendelea kuongezeka. (Isa. 60:22) Hebu wazia, mwaka uliopita tulifikia kilele cha wahubiri 8,201,545, na wastani wa mafunzo 9,499,933 ya Biblia kila mwezi. Kutokana na ongezeko hilo, kumekuwa na uhitaji wa kupanua au kukarabati majengo ya ofisi za tawi. Bila shaka, hilo pia lamaanisha kwamba Majumba ya Ufalme zaidi yanahitajika! Wakati huohuo, kuna uhitaji wa ofisi za utafsiri katika sehemu mbalimbali za dunia, ili watafsiri wetu waishi na kufanya kazi katika maeneo ambayo lugha yao inazungumzwa.

Kwa hiyo, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Ninawezaje kuunga mkono ujenzi wa majengo hayo?’ Baadhi yetu tunaweza kujitolea kushiriki katika kazi ya ujenzi. Na iwe tuna ufundi wa kujenga au hapana, sisi sote tunaweza kuchangia vitu vyetu vyenye thamani ili kuendeleza miradi hiyo muhimu. (Met. 3:9, 10) Wakati wa ujenzi wa maskani, Waisraeli walichochewa kutoa michango mingi sana hivi kwamba tangazo likatolewa ili kuwazuia wasilete zaidi. (Kut. 36:5-7) Bila shaka, mfano huo wa Kimaandiko unagusa mioyo yetu na kutuchochea. “Kazi yenu ya jasho” katika mambo hayo muhimu ya utumishi mtakatifu ni sababu yetu nyingine ya kumshukuru Yehova!

Tuna sababu ya pekee ya kushangilia tunapowaona ndugu zetu wakiendelea kuvumilia hali ngumu. Kwa mfano, wafikirie ndugu zetu wapendwa nchini Korea Kusini. Tangu mwaka wa 1950, ndugu vijana nchini humo wametumikia vifungo vya gereza vyenye urefu tofauti-tofauti kwa sababu ya kutolegeza msimamo wao wa Kikristo wa kutounga mkono upande wowote. Ndugu zetu wamevumilia mateso hayo bila kuyumba-yumba. Mfano wao wa uvumilivu unaimarisha imani yetu!

Nchini Eritrea, ndugu zetu watatu wamefungwa gerezani kwa zaidi ya miaka 20. Wengine, kutia ndani dada zetu na watoto wao, wamefungwa gerezani kwa vipindi vifupi-vifupi. Jitihada nyingi zimefanywa ili waachiwe huru, lakini bila mafanikio yoyote kufikia sasa. Ndugu zetu hawajavunja uaminifu wao. Wamedumisha uaminifu wao chini ya hali ngumu sana. Hatuwasahau waaminifu hao katika sala zetu.—Rom. 1:8, 9.

Bila shaka, wengi wenu hamjafungwa gerezani kwa sababu ya imani yenu. Hata hivyo, wengi wenu mnakabili matatizo ya uzeeni, matatizo ya afya yanayodumu, upinzani kutoka kwa mwenzi asiye mwamini au watu wa ukoo, na pia changamoto nyingine unazozijua wewe mwenyewe. Licha ya hayo, mnaendelea kumtumikia Yehova kwa uaminifu! (Yak. 1:12) Tunawapongeza sana kwa hilo. Uvumilivu wenu ni sababu nyingine inayotufanya tumshukuru Yehova.

Naam, kazi yenu ya uaminifu, kazi yenu ya jasho, na uvumilivu wenu hutupatia sababu nzuri za ‘kumshukuru Yehova, kwa maana yeye ni mwema.’ (Zab. 106:1) Kwa kweli tunawapenda ninyi nyote, na tunasali kwamba Yehova awaimarishe, awategemeze, na kuwabariki ili mwendelee kumtumikia milele.

Ndugu zenu,

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki