Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwyp makala 124
  • Ninaweza Kuboreshaje Ustadi Wangu wa Kuzungumza?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ninaweza Kuboreshaje Ustadi Wangu wa Kuzungumza?
  • Vijana Huuliza
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa nini uzungumze uso kwa uso?
  • Jinsi ya kuanzisha mazungumzo
  • Jinsi ya Kuboresha Stadi za Mazungumzo
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kuanzisha Mazungumzo ili Kutoa Ushahidi Isivyo Rasmi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Mazungumzo Ni Usanii
    Amkeni!—1995
  • Kupendezwa na Watu
    Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
Pata Habari Zaidi
Vijana Huuliza
ijwyp makala 124
Mvulana tineja akizungumza pamoja na wanafunzi wenzake wakati wa mlo wa mchana.

VIJANA HUULIZA

Ninaweza Kuboreshaje Ustadi Wangu wa Kuzungumza?

Katika makala hii

  • Kwa nini uzungumze uso kwa uso?

  • Jinsi ya kuanzisha mazungumzo

  • Vijana Wenzako Wanasema Nini

Kwa nini uzungumze uso kwa uso?

Baadhi ya watu husema kwamba kuzungumza uso kwa uso huwafanya wahisi mkazo na wanapendelea zaidi kutuma ujumbe.

“Unapozungumza uso kwa uso unahitaji kuwa makini zaidi kwa kuwa huwezi kubadili au kufuta maneno ambayo yameshatoka nje.”​—Anna.

“Kutuma ujumbe ni kama tamasha iliyorekodiwa ilhali kuzungumza uso kwa uso ni kama kuwa kwenye tamasha yenyewe. Ninapozungumza ninajiambia, ‘Uwe mwangalifu na unachosema!’”​—Jean.

Hata hivyo, hatimaye, utahitaji kujifunza ustadi wa kuzungumza na watu uso kwa uso. Kwa mfano, utahitaji ustadi huo ikiwa unatamani kuanzisha urafiki na watu wapya, kupata kazi na kuidumisha, au kuanzisha urafiki wa kimahaba utakapokuwa tayari.

Lakini usiwe na hofu kuzungumza na wengine uso kwa uso, kunaweza kukufanya uhisi vizuri. Unaweza kujizoeza kufanya hivyo hata ikiwa wewe ni mwenye haya.

Taa.

Dokezo: Usiogope kufanya makosa. Kujifunza ustadi wa kuwa na mazungumzo ni kama kujifunza kuendesha baiskeli. Huenda “ukaanguka” mara kadhaa, lakini kadiri unavyoendelea kujizoeza, ndivyo utakavyoboresha ustadi wako, nawe utafurahia—ndivyo ilivyo kuhusu ustadi wetu wa kuzungumza!

“Nyakati nyingine, bila kukusudia utasema jambo ambalo si sawa na kujutia. Unahitaji kuruhusu makosa mengine yapite tu na kujicheka.”​—Neal.

Jinsi ya kuanzisha mazungumzo

  • Uliza maswali. Fikiria habari ambayo itawavutia watu, kisha utumie habari hiyo kuanzisha mazungumzo. Kwa mfano:

    “Unafanya kazi gani?”

    “Hapa kuna tovuti nzuri. Umewahi kuijaribu?”

    “Ulisikia kuhusu . . . ?”

    Fikiria jambo hususa linalowakutanisha pamoja. Kwa mfano, je, mnasoma shule moja au mnafanya kazi pamoja? Tumia jambo ambalo linawapendeza nyote kuwa msingi wa maswali yako.

    Wavulana wawili wakizungumza pamoja huku wakila chakula. Inaonekana wanazungumzia mpira.

    “Fikiria maswali ambayo yanakuvutia wewe na ungependa kusikia wengine watakavyoyajibu.”​—Maritza.

    Taa.

    Dokezo: Unaweza kutumia maswali kama hayo yaliyo hapo juu kuanzisha mazungumzo yanayofurahisha. Ikiwezekana uliza maswali ambayo mtu atahitaji kujieleza badala ya kujibu ndiyo au hapana tu. Kwa mfano, ukimwuliza “Ni sehemu gani ambayo ulifurahia zaidi katika sinema ile?” atajieleza zaidi kuliko ukimwuliza “Je, ulifurahia kutazama sinema?”

    Tahadhari: Usimhoji kana kwamba wewe ni polisi kwa kuuliza swali moja baada ya lingine. Pia, usiulize maswali kuhusu mambo ya kibinafsi. Maswali kama vile “Ni nini unachohofu sana?” au “Kwa nini wewe sikuzote unapenda kuvaa nguo za bluu?” yanaweza kumwaibisha. Swali hilo la pili hata linaweza kumfanya ahisi kwamba unamchambua!

    Pia, unaweza kuepuka kuonekana kama polisi ikiwa kabla au baada ya kuuliza swali unamweleza maoni yako kuhusu swali hilo. Yaani, hilo linamaanisha kwamba muwe na mazungumzo—si mahojiano.

    Mvulana aliyevaa mavazi ya polisi akiwa amemkazia macho mwenzake huku akiandika mambo fulani. Kijana aliye upande wa pili ameshtuka na ana hofu huku mwanga mkali ukimmulika usoni.

    Je, maswali yako yanakufanya uonekane kama polisi?

    Kanuni ya Biblia: “Fikira za mtu zimefichika kama kilindi cha maji; lakini mtu mwenye busara ajua kuzichota humo.”​—Methali 20:5, Biblia Habari Njema.

  • Uwe msikilizaji mzuri. Ili uwe na mazungumzo yanayofurahisha ni muhimu kutumia uwezo wako wa kusikiliza kuliko uwezo wako wa kuzungumza.

    “Ninajaribu kutimiza lengo langu la kujifunza jambo moja jipya kumhusu mtu ninayezungumza naye. Kisha baadaye, ninajikumbusha jambo hilo ili kulitumia katika mazungumzo yanayofuata.”​—Tamara.

    Taa.

    Dokezo: Ikiwa mnajikuta mmenyamaza, usiwe na wasiwasi. Angalia mambo yanayowazunguka. Je, mpo shuleni? kazini? Au kwenye tukio fulani? Labda mnaweza kuzungumzia kuhusu mambo hayo. Kwa mfano, unaweza kumwuliza mfanyakazi mwenzako, “Je, inakuchukua muda mrefu kuja kazini?”

    Tahadhari: Usifikirie sana kuhusu utakachosema atakapomaliza kukujibu. Ukisikiliza kwa makini, utaweza kuendeleza mazungumzo kupatana na kile atakachokujibu.

    Kanuni ya Biblia: “Mwepesi wa kusikia, si mwepesi wa kusema.”​—Yakobo 1:19.

  • Pendezwa naye. Utafurahia mazungumzo yenu zaidi ikiwa unamjali yule unayezungumza naye.

    Wasichana wawili wameketi kwenye benchi huku wanatazamana. Msichana aliye kushoto anamsikiliza kwa makini yule aliye kulia akizungumza.

    “Ikiwa utamwonyesha yule unayezungumza naye kuwa unajali yale anayosema, mtakuwa na mazungumzo yenye kufurahisha—hata ikiwa mnajikuta mmenyamaza pindi fulani.”​—Marie.

    Taa.

    Dokezo: Kwanza mpongeze kutoka moyoni kisha unaweza kumwuliza swali. Kwa mfano, “Koti lako ni zuri. Ulilinunua wapi?”

    Tahadhari: Usiingilie maisha yake ya kibinafsi. Utakuwa umevuka mipaka ikiwa utasema “Koti lako ni zuri. Ulilinunua bei gani?”

    Kanuni ya Biblia: “Mkiangalia, si faida zenu wenyewe, bali pia faida za wengine.”​—Wafilipi 2:4.

Unaweza kusema nini mwishoni mwa mazungumzo yenu? Kijana mmoja anayeitwa Jordan anasema: “Malizia mazungumzo kwa njia nzuri. Unaweza kusema, ‘Nimefurahi kuzungumza nawe’ au ‘Uwe na siku njema.’ Kufanya hivyo kunaweza kutokeza fursa ya kuwa na mazungumzo mnapokutana tena.”

Vijana Wenzako Wanasema Nini?

  • Bethel.

    “Kujifunza kuzungumza na wengine ni kama kujifunza kuzungumza lugha mpya. Mwanzoni si rahisi lakini unapotia jitihada na kufanya mazoezi, unaweza kufaulu.”​—Bethel.

  • Isaac.

    “Mtu mwingine anapozungumza, sikiliza kwa makini. Mtazame usoni. Itikia au tikisa kichwa inapofaa. Tabasamu. Unapoonyesha kwamba unasikiliza vizuri wanachosema, wanathamini.”​—Isaac.

  • Kate.

    “Nilikuwa na wasiwasi mwingi nilipoongea na wengine. Nyakati fulani bado ninahisi hivyo. Lakini ninapopendezwa kikweli na yule ninayezungumza naye ninaacha kukazia fikira wasiwasi wangu.”​—Kate.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki