BalanceFormcreative/iStock via Getty Images Plus
Pambana na Upweke kwa Kuwasaidia Wengine—Biblia Inasema Nini?
Watu ulimwenguni pote wanajihisi wapweke na wanashindwa kuwa na uhusiano wa karibu na wengine. Wataalamu wa afya wanaamini kwamba kuwasaidia wengine ni njia ya kupambana na hisia kama hizo.
“Kuwasaidia wengine walio na uhitaji kunaweza kutupatia kusudi maishani na kutusaidia kupambana na hisia za upweke au kutengwa kihisia.”—Taasisi za Kitaifa za Afya za Marekani.
Biblia inatupatia ushauri unaofaa kuhusu kile tunachoweza kufanya ili kuwasaidia wengine. Kufuata ushauri wake kunaweza kutusaidia kushinda hisia za upweke.
Unachoweza kufanya
Uwe mkarimu. Tafuta nafasi za kutumia wakati pamoja na wengine, hasa uso kwa uso. Uwe tayari kushiriki na wengine vitu ulivyo navyo. Unapofanya hivyo, watakuwa tayari zaidi kukutendea kwa shukrani, na hilo huendeleza urafiki.
Kanuni ya Biblia: “Muwe na mazoea ya kuwapa watu, nanyi mtapewa.”—Luka 6:38.
Tumia nguvu zako kuwasaidia wengine. Tafuta njia za kuwasaidia watu wanaokabili hali ngumu. Hilo linatia ndani kuwasikiliza kwa huruma au kuwasaidia kufanya kazi mbalimbali ambazo zitawapunguzia mzigo.
Kanuni ya Biblia: “Rafiki wa kweli hupenda nyakati zote.”—Methali 17:17.
Ili upate habari zaidi kuhusu jinsi ya kudumisha uhusiano mzuri pamoja na wengine, soma makala yenye kichwa “Kuboresha Uhusiano wa Familia na Marafiki.”