Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwyp makala 74
  • Ninaweza Kuepukaje Uchovu wa Kupita Kiasi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ninaweza Kuepukaje Uchovu wa Kupita Kiasi?
  • Vijana Huuliza
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa nini unachoka kupita kiasi?
  • Kwa nini ni jambo zito?
  • Unaweza kufanya nini?
  • Kuungua Nishati—Waweza Kuikabilije Hali?
    Amkeni!—1995
  • Kuungua Nishati—Ni Nani Aliye Hatarini na kwa Nini?
    Amkeni!—1995
  • Jinsi ya Kukabiliana na Uchovu Mwingi
    Amkeni!—2014
  • Kuungua Nishati Ni Zamu Yako?
    Amkeni!—1995
Pata Habari Zaidi
Vijana Huuliza
ijwyp makala 74
Kijana akiwa amelemewa na teknolojia, michezo, burudani, na kazi za shule

VIJANA HUULIZA

Ninaweza Kuepukaje Uchovu wa Kupita Kiasi?

Je, unasumbuliwa na uchovu wa kupita kiasi? Ikiwa ndivyo, makala hii inaweza kukusaidia!

  • Kwa nini unachoka kupita kiasi?

  • Kwa nini ni jambo zito?

  • Unaweza kufanya nini?

  • Vijana wenzako wanasema nini

Kwa nini unachoka kupita kiasi?

  • Kulemewa na kazi. Mwanamke kijana anayeitwa Julie anasema hivi: “Katika kila shughuli maishani, tunaambiwa tufanye vizuri zaidi, tufanye maendeleo zaidi, tuwe na malengo ya juu na tupate mafanikio makubwa. Si rahisi kuishi chini ya mkazo huo!”

  • Teknolojia. Tukiwa na simu za kisasa na vifaa vingine vya kielektroni, tunaweza kuwasiliana usiku na mchana, kwa kweli jambo hilo linaweza kutupa mkazo na baada ya muda, huenda tukachoka kupita kiasi.

  • Kutolala vya kutosha. Mwanamke kijana anayeitwa Miranda anasema hivi: “Shule, kazi, na burudani hufanya vijana wengi waamke mapema sana na wachelewe kulala na wanafanya hivyo karibu kila wakati.” Mara nyingi hali hiyo huchosha sana.

Kwa nini ni jambo zito?

Biblia inasifu kufanya kazi kwa bidii. (Methali 6:​6-8; Waroma 12:11) Lakini haipendekezi tufanye kazi kiasi kwamba kila kitu maishani mwetu kinaathirika kutia ndani afya yetu.

“Wakati fulani, niligundua kwamba sikuwa nimekula kwa siku nzima kwa sababu nilikuwa nikikazia fikira kutimiza majukumu mengi niliyokuwa nayo. Nilijifunza kwamba si vizuri kukubali kila jukumu ninalopata, yaani, kuwa na majukumu mengi mpaka ninaathiri afya.”​—Ashley.

Biblia ina sababu nzuri ya kusema hivi: “Mbwa aliye hai ni afadhali kuliko simba aliyekufa.” (Mhubiri 9:4) Kufanya mambo mengi kupita kiasi kunaweza kufanya ufikiri una nguvu kama za simba kwa muda fulani. Lakini kujichosha kwa njia hiyo kunaweza kuwa na madhara makubwa kwa afya yako.

Unaweza kufanya nini?

  • Jifunze kukataa kazi. Biblia inasema hivi: “Wenye kiasi wana hekima.” (Methali 11:2) Watu wenye kiasi hujua mipaka yao na hawakubali kazi nyingi zaidi ya uwezo wao.

    “Waathiriwa wakuu wa kuchoka kupita kiasi ni wale wasioweza kukataa kazi, wale wanaojaribu kufanya kila kazi wanayopewa. Mtu mwenye kiasi hafanyi hivyo. Ikiwa mtu atafanya hivyo, baada ya muda atachoka kupita kiasi.”​—Jordan.

  • Uwe na wakati wa kutosha wa kupumzika. Biblia inasema hivi: “Ni afadhali konzi moja ya pumziko kuliko konzi mbili za kazi ngumu na kukimbiza upepo.” (Mhubiri 4:6) Usingizi umekuwa ukiitwa “chakula cha ubongo,” lakini matineja wengi hawalali kwa saa nane hadi kumi kama inavyohitajiwa.

    “Ratiba yangu ilipokuwa na mambo mengi kupita kiasi, sikuwa na wakati wa kutosha wa kulala. Lakini wakati mwingine saa hizo za ziada za kulala ndizo ninazohitaji ili kuongeza ubora wa shughuli yangu na kuwa na furaha siku inayofuata.”​—Brooklyn.

  • Panga mambo vizuri. Biblia inasema hivi: “Mipango ya wenye bidii hakika huleta mafanikio.” (Methali 21:5) Kujifunza kupanga vizuri muda na utendaji wako ni ujuzi utakaokusaidia katika maisha yako yote.

    “Mikazo mingi inaweza kuepukwa kwa kuandika ratiba. Ukiandika ratiba yako, ni rahisi kugundua mahali unapohitaji kufanya marekebisho ili kuepuka kuchoka kupita kiasi.”​—Vanessa.

Vijana wenzako wanasema nini

Gianna

“Watu wengine huchoka kupita kiasi kwa sababu wanataka kupata pesa. Lakini 1 Timotheo 6:8 inatuambia turidhike na mahitaji ya msingi ya maisha. Ni jambo zuri kuishi maisha rahisi na kutojitaabisha kwa kufanya kazi kwa ajili ya kutafuta vitu ambavyo hata hatuvihitaji.”​—Gianna.

Waylon

“Kupanga ratiba ya juma zima kumenisaidia sana. Bila hiyo, nilikuwa nikikubali kazi nyingi kupita kiasi. Kisha ninakuwa na mkazo na ninashindwa kutimiza kila kazi.”​—Waylon.

Kara

“Unaweza kufikiri kwamba unahitaji kukubali kila mwaliko na kwamba hutakuwa na furaha ikiwa hutafanya hivyo. Lakini nimejifunza jambo tofauti na hilo. Unakuwa na furaha zaidi na bila mkazo mwingi ukiwa na muda wa kutosha kwa ajili ya kufanya mambo yako binafsi.”​—Kara.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki