Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mrt makala 14
  • Je, Yohana Mbatizaji Alikuwa Mtu Halisi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Yohana Mbatizaji Alikuwa Mtu Halisi?
  • Habari Zaidi
  • Habari Zinazolingana
  • Mauaji Kwenye Sherehe ya Sikukuu ya Kuzaliwa
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Yohana Mbatizaji Alikuwa Nani?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Uuaji Kimakusudi Wakati wa Karamu ya Siku ya Kuzaliwa
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Uuaji Wakati wa Karamu Moja ya Siku ya Kuzaliwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Habari Zaidi
mrt makala 14
Yohana Mbatizaji akiwabatiza watu.

Je, Yohana Mbatizaji Alikuwa Mtu Halisi?

Masimulizi ya Injili yanamtaja mwanamume anayeitwa Yohana Mbatizaji, aliyehubiri kuhusu Ufalme wa Mungu katika eneo la Yudea. Je, masimulizi ya Biblia kumhusu Yohana ni sahihi? Fikiria mambo haya:

  • Biblia inasema: “Yohana Mbatizaji alikuja kuhubiri katika nyika ya Yudea, akisema: ‘Tubuni, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia.’” (Mathayo 3:1, 2) Je, vyanzo vingine vya kihistoria vinathibitisha maneno hayo? Ndiyo.

    Flavio Yosefo, mwanahistoria wa karne ya kwanza alimzungumzia mwanamume anayeitwa “Yohana, aliyeitwa Mbatizaji,” ambaye “aliwahimiza Wayahudi kuishi maisha ya uadilifu,” wawe na “ujitoaji kimungu,” na “wabatizwe.”​—Jewish Antiquities, Buku la 18.

  • Biblia inasema kwamba Yohana alimkaripia Herode Antipa, mtawala wa wilaya ya Galilaya na Perea. Herode alidai kuwa Myahudi anayeishi kupatana na Sheria. Yohana alimkosoa Herode kwa kumwoa Herodia, mke wa ndugu-nusu yake. (Marko 6:18) Jambo hilo limezungumziwa pia na vyanzo vingine tofauti na Biblia.

    Mwanahistoria Yosefo alisema kwamba Antipa “alivutiwa kimapenzi na Herodia” na “aliamua kuwasilisha ombi la kufunga ndoa na mwanamke huyo bila aibu.” Herodia alikubali ombi hilo na kumwacha mume wake ili kuolewa na Antipa.

  • Biblia inasema kwamba “watu kutoka Yerusalemu na Yudea yote na maeneo yote yaliyokuwa karibu na Yordani walikuwa wakimwendea [Yohana], naye akawabatiza katika Mto Yordani.”​—Mathayo 3:5, 6.

    Yosefo aliunga mkono jambo hilo, na akaandika kwamba “umati” wa watu walikuja kumwona Yohana na kwamba watu hao “walichochewa [au, kuamshwa] kwa kiwango kikubwa na mahubiri yake.”

Ni wazi kwamba Yosefo, mwanahistoria wa karne ya kwanza alimtambua Yohana Mbatizaji kuwa mtu halisi. Sisi pia tunaweza kuwa na uhakika huo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki