16 Ikatukia kwamba tulipokuwa tukienda mahali pale pa kusali, tulikutana na kijakazi fulani mwenye roho, roho mwovu wa uaguzi.+ Aliwapatia mabwana zake faida nyingi kwa kubashiri.*
16 Na ikatukia kwamba tulipokuwa tukienda pale mahali pa sala, kijakazi fulani mwenye roho,+ roho mwovu wa uaguzi,+ akakutana nasi. Yeye alikuwa akiwapatia mabwana zake faida+ nyingi kwa kufanya ufundi wa kubashiri.