Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
Tangazo
Lugha mpya zinazopatikana: Betsimisaraka (Northern), Betsimisaraka (Southern), Konkomba, Matses, Mi'kmaq
  • Leo

Alhamisi, Oktoba 30

Kwa kadiri ambavyo tumefanya maendeleo, na tuendelee kutembea kwa utaratibu katika mwendo huohuo.—Flp. 3:16.

Yehova hataona kwamba umeshindwa kwa kukosa kutimiza lengo ambalo linapita uwezo wako. (2 Kor. 8:12) Ona kipingamizi hicho kuwa fursa ya kujifunza. Kumbuka mambo ambayo tayari umetimiza. Biblia inasema hivi: “Mungu hakosi kuwa mwadilifu hivi kwamba asahau kazi [yako].” (Ebr. 6:10) Basi wewe pia hupaswi kusahau. Fikiria kuhusu mambo ambayo tayari umetimiza—iwe ni kusitawisha urafiki pamoja na Yehova, kuwaambia wengine kumhusu, au kubatizwa. Kama vile ulivyofanya maendeleo na kutimiza malengo ya kiroho wakati uliopita, unaweza kuendelea kufanya maendeleo ili kutimiza lengo lako sasa. Kwa msaada wa Yehova, unaweza kutimiza lengo lako. Unapoendelea kufanyia kazi lengo lako la kiroho, usisahau kufurahia kuona jinsi Yehova anavyokusaidia na kukubariki unapojitahidi kutimiza lengo lako. (2 Kor. 4:7) Usipokufa moyo, utapata baraka kubwa hata zaidi.—Gal. 6:9. w23.05 31 ¶16-18

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Ijumaa, Oktoba 31

Baba mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu mmenipenda na mmeamini kwamba nilikuja nikiwa mwakilishi wa Mungu.—Yoh. 16:27.

Yehova anafurahi kuwaonyesha kibali chake wale anaowapenda. Maandiko yanataja pindi mbili ambapo Yehova alimwambia Yesu kwamba yeye ni Mwana wake mpendwa, anayemkubali. (Mt. 3:17; 17:5) Je, ungependa kumsikia Yehova akikuhakikishia kwamba una kibali chake? Yehova hazungumzi nasi moja kwa moja, lakini anazungumza nasi kupitia Neno lake. Tunaposoma katika vitabu vya Injili maneno yenye upendo ya Yesu aliyowaambia wanafunzi wake, ni kana kwamba tunamsikia Yehova akizungumza nasi. Yesu aliiga kikamilifu utu wa Baba yake. Hivyo, tunaposoma kwamba Yesu aliwaambia wafuasi wake waaminifu ambao si wakamilifu kwamba amewakubali, tunaweza kuwazia Yehova akituambia maneno hayohayo. (Yoh. 15:​9, 15) Majaribu yanapotokea, hayamaanishi kwamba tumepoteza kibali cha Mungu. Badala yake, yanatupatia fursa ya kuthibitisha kina cha upendo wetu kwa Mungu na kwamba tunamtumaini.—Yak. 1:12. w24.03 28 ¶10-11

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025

Jumamosi, Novemba 1

Kutoka katika vinywa vya watoto wadogo na wanaonyonya, umetoa sifa.—Mt. 21:16.

Ikiwa wewe ni mzazi, wasaidie watoto wako watayarishe maelezo yanayolingana na umri wao. Nyakati nyingine, mambo mazito kama vile matatizo ya ndoa au masuala ya kiadili, huzungumziwa wakati wa funzo, lakini huenda kuna fungu moja au mawili ambayo mtoto anaweza kutoa maelezo. Pia, wasaidie watoto wako waelewe kwa nini huenda hawatachaguliwa kila mara wanapoinua mkono. Kufafanua jambo hilo kunaweza kuwasaidia wasivunjike moyo watu wengine wanapochaguliwa. (1 Tim. 6:18) Sisi sote tunaweza kutayarisha maelezo yenye kujenga ambayo yatamletea Yehova heshima na kuwatia moyo Wakristo wenzetu. (Met. 25:11) Ingawa wakati mwingine tunaweza kutoa maelezo mafupi ya mambo tuliyojionea, tunapaswa kuepuka kuzungumza sana kujihusu. (Met. 27:2; 2 Kor. 10:18) Badala yake, tunajitahidi kumkazia fikira Yehova, Neno lake, na watu wake kwa ujumla.—Ufu. 4:11. w23.04 24-25 ¶17-18

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki