-
Ule Uasi-imani Mkubwa WasitawiMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kwa habari ya tengenezo, kila kutaniko lilisimamiwa na baraza la waangalizi, au wazee wa kiroho.b Wazee wote walikuwa na mamlaka sawa, na hakuna yeyote wao aliyepewa mamlaka ya ‘kupiga ubwana’ juu ya kundi lililo katika utunzaji wao. (Mdo. 20:17; Flp. 1:1; 1 Pet. 5:2, 3) Hata hivyo, kadiri uasi-imani ulivyofunuka wazi, mambo yalianza kubadilika—kwa haraka.
Miongoni mwa mikengeuko ya mapema kabisa kulikuwa na kutenganishwa kwa maneno “mwangalizi” (Kigiriki, e·piʹsko·pos) na “mwanamume mzee,” au “mzee” (Kigiriki, pre·sbyʹte·ros), hivi kwamba maneno hayo hayakutumiwa tena kurejezea cheo kilekile kimoja cha daraka. Mwongo mmoja hivi baada ya kifo cha mtume Yohana, Ignatius, “askofu” wa Antiokia, katika barua yake kwa Wasmirna, aliandika hivi: “Hakikisheni kwamba mwamfuata askofu [mwangalizi], kama Yesu Kristo amfuatavyo Baba, na presbiteri [baraza la wanaume wazee] kama kwamba mnafuata wale Mitume.” Hivyo Ignatius alitetea maoni ya kwamba kila kutaniko lapasa kusimamiwa na askofu mmoja,c au mwangalizi, ambaye alipaswa kutambuliwa kuwa tofauti, na mwenye mamlaka kubwa kuliko, wapresbiteri, au wanaume wazee.
Ingawa hivyo, kutenganishwa huko kulitokeaje? Augustus Neander katika kitabu chake, The History of the Christian Religion and Church, During the Three First Centuries, aeleza wazi lililotukia: “Katika karne ya pili . . . , ni lazima iwe ndipo cheo cha sasa cha msimamizi mkuu wa kuchaguliwa wa wapresbiteri kilipofanyizwa, ambaye, kwa sababu ndiye hasa aliyekuwa na uangalizi wa kila kitu, alipewa lile jina la [e·piʹsko·pos], na hapo akatofautishwa na wale wapresbiteri wengine wote.”
Hivyo msingi uliwekwa ili jamii ya makasisi iibuke hatua kwa hatua. Karibu karne moja baadaye, Cyprian, “askofu” wa Carthage, Afrika Kaskazini, alikuwa mtetezi imara wa mamlaka ya maaskofu—kuwa kikundi tofauti na wapresbiteri (ambao baadaye walijulikana kuwa makuhani au mapadrid), na mashemasi, na watu wa kawaida. Lakini yeye hakupendelea umashuhuri wa askofu mmoja juu ya wengine.e
-
-
Ule Uasi-imani Mkubwa WasitawiMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
b Katika Maandiko maneno “mwangalizi” na “mwanamume mzee,” au “mzee,” hurejezea cheo kilekile kimoja. (Mdo. 20:17, 28, NW; Tito 1:5, 7, NW) “Mwanamume mzee” huonyesha sifa za ukomavu za yule ambaye huwekwa rasmi hivyo, na “mwangalizi” huonyesha daraka lililo asili ya kuwekwa rasmi huko—kuangalia masilahi za watu wale waliokabidhiwa kwenye utunzaji wake.
-