-
Kuimba Wimbo Mpya wa Sherehe ya UshindiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
4. Inakuwaje kwamba 144,000 wote wanasimama juu ya Mlima Sayuni?
4 Yohana anaona Yesu na pia mwili kamili wa 144,000 warithi wenzi wa Ufalme wa kimbingu wakiwa wanasimama juu ya Mlima Sayuni. Katika wakati unaowakilishwa na njozi, wengi, lakini si wote, wa wale 144,000 tayari wako katika mbingu. Baadaye katika njozi iyo hiyo, Yohana anajifunza kwamba baadhi ya watakatifu wangali wanapaswa kuvumilia na kufa wakiwa waaminifu. (Ufunuo 14:12, 13) Kwa wazi, basi, baadhi ya 144,000 wangali wako duniani. Kwa hiyo inakuwaje kwamba Yohana anaona 144,000 wote wakisimama pamoja na Yesu juu ya Mlima Sayuni?a Kwamba, wakiwa washiriki wa kundi la Wakristo wapakwa-mafuta, sasa hawa ‘wamekaribia Mlima Sayuni na jiji la Mungu aliye hai, Yerusalemu la kimbingu.’ (Waebrania 12:22, NW) Kama Paulo wakati alipokuwa angali duniani, tayari wao—katika maana ya kiroho—wameinuliwa juu wakawe katika muungano na Kristo Yesu katika mahali pa kimbingu. (Waefeso 2:5, 6) Kwa kuongezea, katika 1919 wao waliitikia mwito, “Njooni juu huku,” na kitamathali ‘walienda ndani ya mbingu katika wingu.’ (Ufunuo 11:12, NW) Kwa sababu ya maandiko haya, sisi tunaweza kuona kwamba wote 144,000—kusema kiroho—wako kwenye Mlima Sayuni pamoja na Yesu Kristo.
5. Ni majina ya nani yaliyoandikwa juu ya vipaji vya nyuso za 144,000, na ni nini maana ya kila jina?
5 Hao 144,000 hawana sehemu yoyote pamoja na waabudu wa hayawani-mwitu, ambao wametiwa alama ya nambari ya ufananisho 666. (Ufunuo 13:15-18) Kwa kutofautiana, washikamanifu hawa wana jina la Mungu na la Mwana-Kondoo limeandikwa juu ya vipaji vya nyuso zao. Hapana shaka Yohana, Myahudi, aliona jina la Mungu katika herufi za Kiebrania, יהוה.b Katika kuwa na jina la Baba ya Yesu limeandikwa kwa ufananisho juu ya vipaji vya nyuso zao, hawa watiwa-muhuri wanajulisha wote kwamba wao ni mashahidi wa Yehova, watumwa Wake. (Ufunuo 3:12) Kuwa kwao na jina la Yesu pia likiwa linaonyeshwa juu ya vipaji vya nyuso zao hudokeza kwamba wanakiri kuwa wao ni milki yake. Yeye ni “mume” wao aliyewaposa, na wao wanatazamia kuwa “bibi-arusi” wake, “uumbaji mpya” wakitumikia Mungu wakitazamia uhai wa kimbingu. (Waefeso 5:22-24; Ufunuo 21:2, 9; 2 Wakorintho 5:17, NW) Uhusiano wao wa usiri pamoja na Yehova na Yesu Kristo huathiri mawazo na matendo yao.
Wakiimba Kana Kwamba ni Wimbo Mpya
6. Yohana anasikia wimbaji gani, naye anauelezaje?
6 Kupatana na hili, Yohana aripoti: “Na mimi nikasikia mvumo kutoka katika mbingu kama mvumo wa maji mengi na kama mvumo wa ngurumo yenye sauti kubwa; na mvumo ambao mimi nilisikia ulikuwa kama wa waimbaji ambao hujifuatisha wenyewe kwa kinubi wakipiga vinubi vyao. Na wao wanaimba kana kwamba ni wimbo mpya mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya viumbe hai wanne na wazee; na hakuna yeyote aliyeweza kuwa bingwa wa wimbo huo ila wale mia na arobaini na nne elfu, ambao wamenunuliwa kutoka dunia.” (Ufunuo 14:2, 3, NW) Si ajabu kwamba Yohana, aliposikia sauti 144,000 zikiungana katika korasi moja ya kimelodia, anakumbushwa mngurumo wa poromoko la maji na makofi yenye mlio wa mngurumo. Ni wenye kupendeza kama nini mfuatisho huo kama wa kinubi! (Zaburi 81:2) Ni kwaya gani ya kidunia ambayo ingefikia utukufu mkuu wa korasi hiyo yenye uzuri mwingi mno?
7. (a) Wimbo mpya wa Ufunuo 14:3 ni nini? (b) Inakuwaje kwamba wimbo wa Zaburi 149:1 ni mpya kwa siku yetu?
7 Na huu “wimbo mpya” ni nini? Kama tulivyoona tulipozungumzia Ufunuo 5:9, 10, wimbo huo unahusiana na makusudi ya Ufalme wa Yehova na uandalizi mzuri ajabu wake kupitia Yesu Kristo, kwa ajili ya kufanya Israeli wa kiroho “ufalme na makuhani kwa Mungu wetu.” Ni wimbo wa sifa kwa Yehova wenye kutangaza vitu vipya anavyotimiza kupitia Israeli wa Mungu na kwa niaba yao. (Wagalatia 6:16) Washiriki wa Israeli wa kiroho wanaitikia mwaliko wa mtunga zaburi: “Sifuni Yah enyi watu! Imbieni Yehova wimbo mpya, sifa yake katika kundi la washikamanifu. Acheni Israeli ashangilie katika Mfanyi wake mtukufu, wana wa Sayuni—acheni wao wawe wenye shangwe katika Mfalme wao.” (Zaburi 149:1, 2, NW) Kweli, maneno hayo yaliandikwa karne nyingi zilizopita, lakini katika siku yetu, yameimbwa kwa uelewevu mpya. Katika 1914 Ufalme wa Kimesiya ulizaliwa. (Ufunuo 12:10) Katika 1919 watu wa Yehova duniani walianza kutangaza “neno la ufalme” wakiwa na bidii iliyofanywa upya. (Mathayo 13:19) Wakichochewa na andiko la mwaka kwa ajili ya 1919 (Isaya 54:17) na wakitiwa moyo na kurudishwa kwao kwenye paradiso ya kiroho, wao walianza katika mwaka huo ‘kuimbia Yehova kwa muziki katika mioyo yao.’—Waefeso 5:19, NW.
8. Ni kwa nini ni wale 144,000 tu wanaoweza kujifunza wimbo mpya wa Ufunuo 14:3?
8 Ingawa hivyo, ni kwa nini ni wale 144,000 tu wanaoweza kujifunza wimbo unaotajwa kwenye Ufunuo 14:3? Ni kwa sababu unahusiana na wanayoona wakiwa warithi wachaguliwa wa Ufalme wa Mungu. Wao pekee ndio wanaolelewa kuwa wana wa Mungu na kupakwa mafuta kwa roho takatifu. Wao pekee ndio walionunuliwa kutoka dunia na kuwa sehemu ya Ufalme huo wa kimbingu, na wao pekee ndio “watakuwa makuhani . . . na watatawala wakiwa wafalme” pamoja na Yesu Kristo kwa miaka elfu ili kuleta aina ya binadamu kwenye ukamilifu. Wao pekee ndio wanaoonwa “wanaimba kana kwamba ni wimbo mpya” katika kuwapo kwenyewe kwa Yehova.c Maono haya yasiyo na kifani na mataraja huwapa wao uthamini wa pekee wa Ufalme na kuwawezesha kuimba juu ya huo katika njia ambayo hakuna mwingine awezaye.—Ufunuo 20:6; Wakolosai 1:13; 1 Wathesalonike 2:11, 12, NW.
-
-
Kuimba Wimbo Mpya wa Sherehe ya UshindiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
10. Inawezekanaje kwa 144,000 kuimba “mbele ya” wale wazee wa ufananisho 24?
10 Wale 144,000 wanawezaje kuimba “mbele ya” wazee, kwa kuwa wazee ndio hao 144,000 wakiwa katika vyeo vyao vya kimbingu vyenye utukufu? Mapema katika siku ya Bwana, wale “wafu katika muungano pamoja na Kristo” walifufuliwa wakiwa viumbe vya roho. Hivyo, Wakristo wapakwa-mafuta waaminifu ambao wameshinda sasa wako katika mbingu, wakitimiza kwa ufananisho kazi zao zinazolinganika na zile za migawanyo 24 ya wazee wa kikuhani. Wao wanatiwa ndani ya ile njozi ya tengenezo la Yehova la kimbingu. (1 Wathesalonike 4:15, 16; 1 Nyakati 24:1-18; Ufunuo 4:4; 6:11, NW) Kwa hiyo lile baki la 144,000 ambalo lingali duniani linaimba wimbo mpya mbele ya, au katika mwono wa, ndugu zao waliofufuliwa katika mbingu.
11. Ni kwa nini washindi wapakwa-mafuta wanarejezewa kuwa wazee 24 na pia 144,000?
11 Kufikia hapa twaweza pia kuuliza: Ni kwa nini washindi hawa wapakwa-mafuta wanarejezewa kuwa wazee wa ufananisho 24 na pia 144,000? Ni kwa sababu Ufunuo hukiona kikundi hiki kutokana na vituo vya msimamo viwili tofauti. Sikuzote wazee 24 wanaonyeshwa wakiwa katika cheo chao cha mwisho kabisa kuzunguka kiti cha ufalme cha Yehova, wakiwa wamewekwa kuwa wafalme na makuhani katika mbingu. Wao hufananisha kikundi kizima cha 144,000 katika vyeo vyao vya kimbingu, ijapokuwa kwa wakati uliopo baki dogo la hawa lingali duniani. (Ufunuo 4:4, 10; 5:5-14; 7:11-13; 11:16-18) Hata hivyo, Ufunuo sura ya 7, huelekeza fikira juu ya 144,000 kama wakitolewa katika aina ya kibinadamu, na hukazia kusudi tukufu la Yehova la kutia muhuri hesabu kamili ya Waisraeli wa kiroho mmoja mmoja na kuupa wokovu umati mkubwa usiohesabika. Ufunuo sura ya 14 huandaa picha ikithibitisha kwamba jamii kamili ya Ufalme 144,000 washindi mmoja mmoja watakusanyishwa pamoja na Mwana-Kondoo juu ya Mlima Sayuni. Sifa za kutimizwa ili kuwa katika hesabu hiyo pamoja na 144,000 zinajulishwa pia, kama tutakavyoona sasa.d
-