-
MatangazoHuduma ya Ufalme—2009 | Juni
-
-
Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Juni: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Ikiwa wenye nyumba tayari wana kitabu hicho, wahubiri wanaweza kutoa kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli, Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, au broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? Julai na Agosti: Wahubiri wanaweza kutoa yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 zinazopatikana: Endeleeni Kukesha!, Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, Serikali Itakayoleta Paradiso, “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” Our Problems—Who Will Help Us Solve Them?, au broshua nyingine yoyote ya lugha ya kienyeji inayopatikana. Septemba: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Inapowezekana, wahubiri watajitahidi kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kwanza mtu anapochukua kitabu. Mwonyeshe mwenye nyumba jinsi kitabu hicho kinavyoweza kumnufaisha kwa kumwonyesha kifupi jinsi funzo la Biblia linavyofanywa.
◼ Jitihada nyingi zitafanywa ili kutangaza makusanyiko ya wilaya na ya kimataifa ya mwaka wa 2009 yatakayofanywa duniani kote. Wahubiri watakuwa na pendeleo la kugawa mwaliko wa pekee katika eneo lao. Kampeni ya kugawa mwaliko huo inapaswa kufanywa majuma matatu kabla ya kusanyiko ambalo kutaniko litahudhuria.
◼ Wahubiri wote watapata beji za kusanyiko kupitia kutaniko. Ndugu kutoka nchi nyingine watakaohudhuria kusanyiko la kimataifa watatumia beji ileile.
◼ Huenda ratiba za mikutano zikabadilishwa ikihitajika ili ndugu waweze kuhudhuria Kusanyiko la Wilaya la “Endeleeni Kukesha!” Katika Mkutano wa Utumishi wa mwisho kabla ya kuhudhuria kusanyiko, mashauri na vikumbusho vinavyofaa katika eneo lenu vinapaswa kupitiwa. Mwezi mmoja au miwili baada ya kusanyiko lenu, sehemu ya mahitaji ya kwenu inaweza kutumiwa ili kupitia mambo makuu ya kusanyiko ambayo wahubiri wameona kuwa yenye manufaa katika huduma.
-
-
Ratiba ya Juma Linaloanza Julai 6Huduma ya Ufalme—2009 | Juni
-
-
Ratiba ya Juma Linaloanza Julai 6
JUMA LINALOANZA JULAI 6
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
lv sura ya 7 ¶1-9, masanduku kwenye uku. 76, 78
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 17-20
Na. 1: Mambo ya Walawi 19:1-18
Na. 2: Je, Sisi Sote Tulikuwa Katika Makao ya Kiroho Kabla Hatujazaliwa Tukiwa Wanadamu? (rs uku. 197 ¶3–uku. 198 ¶3)
Na. 3: Usiwe Mwizi Kamwe! (lr sura ya 24)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5: Matangazo.
Dak. 5: Mhoji mzee mmoja au wawili wa kutaniko, au watumishi wa huduma. Ni nini lililowachochea wafanye maendeleo ili kufanya kazi njema? (1 Tim. 3:1-9) Wengine waliwasaidia na kuwatia moyo jinsi gani? Wamepata baraka gani?
Dak. 25: “Je, Uko Tayari kwa Ajili ya Karamu ya Kiroho?” Sehemu hii ishughulikiwe na mwandishi wa kutaniko. Taja kusanyiko ambalo kutaniko limegawiwa kuhudhuria. Pitia sanduku “Vikumbusho vya Kusanyiko la Wilaya.” Wakati wa kuzungumzia fungu la 7, tumia muda mfupi kupitia barua na broshua Mavazi na Mapambo kwa Wanaotembelea Betheli au kitabu Tengenezo, ukurasa wa 138, fungu la 2, na ukurasa wa 139, fungu la 1.
-
-
Mambo ya Kusema Kuhusu MagazetiHuduma ya Ufalme—2009 | Juni
-
-
Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Mei 1
Soma Mathayo 24:3. Kisha useme: “Watu fulani wanafikiri kwamba swali hili linahusu mwisho wa dunia. Je, unafikiri dunia itaharibiwa? [Mruhusu ajibu.] Kulingana na jibu la Yesu, hatungojei mwisho wa dunia, bali mwisho wa kitu kingine. Makala iliyo kwenye ukurasa wa 16 inazungumzia habari hiyo kwa undani zaidi.”
Amkeni! Mei
“Wahubiri fulani husema kwamba tukifanya mambo yanayompendeza Mungu, atatupa utajiri. Lakini labda unawajua watu wema ambao ni maskini. Je, unafikiri Mungu anataka tuwe matajiri? [Mruhusu ajibu, kisha usome Waebrania 13:5.] Makala hii inaeleza jinsi Mungu anavyotubariki.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 12.
Mnara wa Mlinzi Juni 1
“Vitabu vyenye mashauri kuhusu kulea watoto, upendo, na kupata uradhi, vinapendwa sana leo. Je, wewe binafsi umeviona kuwa vyenye manufaa? [Mruhusu ajibu.] Wengi hupuuza chanzo hiki cha mashauri yenye kutegemeka. [Soma 2 Timotheo 3:16.] Gazeti hili linaeleza kwa nini tunaweza kuitegemea Biblia na linataja mashauri mbalimbali ya Biblia yanayoweza kutusaidia.”
Amkeni! Juni
“Kama unavyojua, suala la kutoa mimba au kutotoa mimba limezusha mjadala mkali sana. Je, unafikiri Biblia inaweza kumsaidia mtu kufanya uamuzi unaofaa? [Mruhusu ajibu, kisha usome 2 Timotheo 3:16, 17.] Gazeti hili linazungumzia maoni ya Biblia kuhusu jambo hilo.”
-