Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Mei 1
Soma Mathayo 24:3. Kisha useme: “Watu fulani wanafikiri kwamba swali hili linahusu mwisho wa dunia. Je, unafikiri dunia itaharibiwa? [Mruhusu ajibu.] Kulingana na jibu la Yesu, hatungojei mwisho wa dunia, bali mwisho wa kitu kingine. Makala iliyo kwenye ukurasa wa 16 inazungumzia habari hiyo kwa undani zaidi.”
Amkeni! Mei
“Wahubiri fulani husema kwamba tukifanya mambo yanayompendeza Mungu, atatupa utajiri. Lakini labda unawajua watu wema ambao ni maskini. Je, unafikiri Mungu anataka tuwe matajiri? [Mruhusu ajibu, kisha usome Waebrania 13:5.] Makala hii inaeleza jinsi Mungu anavyotubariki.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 12.
Mnara wa Mlinzi Juni 1
“Vitabu vyenye mashauri kuhusu kulea watoto, upendo, na kupata uradhi, vinapendwa sana leo. Je, wewe binafsi umeviona kuwa vyenye manufaa? [Mruhusu ajibu.] Wengi hupuuza chanzo hiki cha mashauri yenye kutegemeka. [Soma 2 Timotheo 3:16.] Gazeti hili linaeleza kwa nini tunaweza kuitegemea Biblia na linataja mashauri mbalimbali ya Biblia yanayoweza kutusaidia.”
Amkeni! Juni
“Kama unavyojua, suala la kutoa mimba au kutotoa mimba limezusha mjadala mkali sana. Je, unafikiri Biblia inaweza kumsaidia mtu kufanya uamuzi unaofaa? [Mruhusu ajibu, kisha usome 2 Timotheo 3:16, 17.] Gazeti hili linazungumzia maoni ya Biblia kuhusu jambo hilo.”