Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Matangazo
    Huduma ya Ufalme—2002 | Aprili
    • Matangazo

      ◼ Toleo la vichapo la Aprili na Mei: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Iwapo mtu anapendezwa unapomrudia, panga kumpelekea magazeti kwa ukawaida. Watu wakipendezwa, toa broshua Anataka au Rafiki ya Mungu na ujitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Juni: Mungu Anataka Tufanye Nini? au kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Ikiwa wenye nyumba wana vichapo hivyo, toa broshua inayofaa ambayo kutaniko inayo akibani. Julai: Broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutolewa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Broshua Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? zaweza kutolewa inapofaa.

      ◼ Mahubiri yetu ya kila mwaka ya eneo la mbali yatafanywa Julai na Agosti. Makutaniko yaliyo na maombi hususa ya kuhubiri eneo la mbali yanaweza kuandikia ofisi ya tawi kabla ya Mei 15, 2002. Kutaniko lolote ambalo halijapewa eneo la mbali laweza kupanga kuhubiri eneo lisilohubiriwa kwa ukawaida.

      ◼ Beji za kusanyiko la wilaya la mwaka wa 2002 katika Kifaransa, Kiganda, Kiingereza, Kirundi, na Kiswahili zitatiwa ndani ya upakizi wa vichapo. Si lazima ziombwe. Beji zitapakiwa kwa mafungu ya kadi 25 ikitegemea ukubwa wa kila kutaniko. Ikiwa beji za ziada zahitajiwa na makutaniko, zapasa kuombwa kwenye Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14-SW). Vifuko vya beji vya plastiki vyapaswa kuombwa kwa ajili ya yeyote kutanikoni anayevihitaji.

      ◼ Ni muhimu kwa Sosaiti kuwa na anwani na namba za simu za karibuni za waangalizi-wasimamizi na waandishi wote. Ikiwa kutakuwa na badiliko lolote, Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko inapaswa kujaza fomu ya Badiliko la Anwani ya Mwangalizi-Msimamizi/Badiliko la Anwani ya Mwandishi (S-29-SW) na kuituma kwa Sosaiti haraka iwezekanavyo. Hiyo yatia ndani mabadiliko yoyote katika anwani ya eneo lao.

      ◼ Waandishi wa kutaniko wanapaswa kuweka fomu za kutosha za Ombi la Utumishi wa Painia wa Kawaida (S-205-SW) na Ombi la Utumishi wa Painia-Msaidizi (S-205b-SW). Zaweza kuagizwa kwenye Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14-SW). Wekeni angalau akiba ya mwaka mmoja. Chunguzeni fomu zote za ombi la painia wa kawaida ili kuhakikisha kwamba zimejazwa kikamili. Ikiwa wenye kutoa maombi hawakumbuki vizuri tarehe ya ubatizo wao, wanapaswa kukadiria tarehe na kuiandika mahali.

      ◼ Iwapo wakati wowote utapanga kusafiri kwenda nchi nyingine, na utake kufahamishwa tarehe, nyakati, na mahali pa kuhudhuria mikutano ya kutaniko, kusanyiko la mzunguko au la wilaya, uliza ofisi ya tawi inayosimamia kazi katika nchi hiyo. Utapata orodha ya anwani za ofisi za tawi katika ukurasa wa mwisho wa Yearbook ya karibuni.

      ◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:

      Watch Tower Publications Index 2001—Kiingereza

      Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu —Kijaluo

      ◼ Video Mpya Zinazopatikana:

      Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi—Sehemu ya 7—Lugha ya Ishara ya Marekani

      Respect Jehovah’s Authority—On Videocassette—Lugha Ishara ya Marekani

      Warning Examples for Our Day—On Videocassette—Kiingereza

  • Endelea Kunufaika na Mnara wa Mlinzi na Amkeni!
    Huduma ya Ufalme—2002 | Aprili
    • Endelea Kunufaika na Mnara wa Mlinzi na Amkeni!

      Kwa kuwa sasa maandikisho ya posta ya magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yanakomeshwa, jitihada zitatakikana ili kuhakikisha kwamba sisi na wale tunaohubiria hatukosi hata toleo moja la magazeti hayo.

      Magazeti ya Kibinafsi: Andikisho lako linapoisha, ongeza agizo lako la sasa kwenye idara ya magazeti. Wazazi wanapaswa kuagiza magazeti ya kutosha ili kila mmoja katika familia awe na gazeti lake mwenyewe. Kuandika jina lako kwenye gazeti lako kutahakikisha kwamba huliachii mtu bila kukusudia katika utumishi wa shambani. Mara tu magazeti yanapofika, akina ndugu wanaoyashughulikia watahakikisha kwamba kila toleo la magazeti hayo lapatikana kwenye Jumba la Ufalme.

      Watu Wanaopelekewa Magazeti kwa Ukawaida: Wahubiri wanapaswa kujitahidi kuwa na watu wanaowapelekea magazeti kwa ukawaida, wanaopenda kupokea kila toleo. Kuwapelekea watu hao magazeti kibinafsi kutatokeza fursa za kusitawisha kupendezwa walikoonyesha na kuanzisha mafunzo ya Biblia.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 1998, ukurasa wa 12.

      Walio na Mahitaji ya Pekee: Hali ya pekee ambayo itaruhusiwa kutuma andikisho kwa posta ni kama kuna mtu anayependezwa kikweli lakini anaishi katika eneo lisilogawiwa kutaniko lolote. Ikiwa mtu anayeishi katika eneo la kutaniko hawezi kufikiwa ili kupelekewa magazeti kwa ukawaida lakini angependa kupata magazeti, zungumza na Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko. Wakikubali, anaweza kufanyiwa andikisho. Fomu za kawaida za andikisho (M-1-SW na M-101-SW) zaweza kutumiwa kwa kusudi hilo.

      Tuna uhakika kwamba Yehova ataendelea kubariki jitihada zetu zote za kutangaza Ufalme kupitia magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!

  • Habari za Kitheokrasi
    Huduma ya Ufalme—2002 | Aprili
    • Habari za Kitheokrasi

      ◼ Majumba ya Ufalme yafuatayo yaliwekwa wakfu hivi karibuni:

      Burundi: Kinama na Nyabihanga.

      Kenya: Eldoret-Race Course, Kagio, Kaimosi, Kilgoris, Kivaa, Luanda, Masinga Dam, Naivasha, Ondiri, na Sultan Hamud.

      Tanzania: Ifuwa, Kahe, Malowe, Nditu, Nkala, Sumbawanga Kaskazini, na Turiani.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki