Maswali Kutoka kwa Wasomaji
◼ Watu wa Mungu wanapaswa ‘kutunza wale walio wao wenyewe,’ kwa hiyo Abrahamu angewezaje kufukuza Hagari na Ishmaeli hivi hivi tu wakaingie ndani ya nyika?
Ni jambo la upendo na lenye kufaa pia watumishi wa Mungu watunze washiriki wa jamaa walio na uhitaji. Kwa habari ya wazazi Wakristo, mtume Paulo aliandika hivi: “Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.”—1 Timotheo 5:8.
Sisi tunaweza kuwa na uhakika kwamba mwendo wa Abrahamu haukuwa kinyume cha roho ya shauri hilo la kutii Mungu, kwa maana yeye alituwekea sisi kielelezo cha imani ya kweli, akiwa “rafiki ya Yehova.”—Yakobo 2:23, NW; Waebrania 11:8-19.
Mungu aliahidi baraka kupitia uzao au mrithi wa Abrahamu. Wakati Sara alipokuwa mzee-mzee akiwa tasa bado, yeye alihimiza Abrahamu azae mwana kupitia Hagari mjakazi Mmisri wa Sara. Baadaye, Hagari alipokuwa mwenye mimba, yeye alianza kutenda kwa ufidhuli sana kuelekea Sara hivi kwamba jambo hilo lingeweza kuelezwa kuwa “jeuri,” au kosa la kutaka kudhuru mke mpendwa wa Abrahamu. (Kutoka 23:1; 2 Samweli 22:49; Zaburi 11:5) Abrahamu aliacha Sara amkumbushe Hagari kutofanya jambo lisilopasa cheo chake, na hapo ndipo Hagari alikimbia kwenda zake nyikani, labda akielekeza mwendo kurudi Misri. Usimulizi ule hausemi kwamba yeye alienda akiwa na maandalizi, kwa hiyo huenda ikawa alijua kwamba angeweza kupata chakula na maji kwenye maeneo fulani ya kupigia kambi, kama vile kutoka kwa vikundi vya Mabedui.—Mwanzo 12:1-3, 7; 16:1-6, NW.
Malaika mmoja alijitia katika jambo hilo na kuambia Hagari kwamba anapaswa kurudi, kwamba yeye angekuwa na wazaliwa wengi, na kwamba ‘mkono wa Ishmaeli mwana wake ungekuwa dhidi ya kila mmoja.’ (Mwanzo 16:7-12, NW) Si miaka mingi mno baadaye, Ishmaeli alithibitika kuwa dhidi ya Isaka mchanga, mrithi wa kweli wa Abrahamu ambaye alizaliwa kwa Sara. Ishmaeli alianza ‘kufanya dhihaka’ kuelekea Isaka, au kumtukana. Hilo lilikuwa jambo zito lisilo ushindani wa kidugu tu. Neno la Mungu linatambulisha jambo hilo kuwa ‘kunyanyasa’ uzao wa Abrahamu uliotabiriwa kwa njia ya kimungu. Kwa hiyo kitendo thabiti kilifaa kufanywa.—Mwanzo 21:1-9; Wagalatia 4:29-31, NW.
Yehova aliambia Abrahamu atii msimamo wa mke wake juu ya jambo lililohitaji kufanywa, ‘kuondosha nje Hagari na mwana wake.’ Ingawa Abrahamu hakufurahishwa na tazamio hilo la Hagari kuondoka pamoja na mwana wake, Abrahamu alifanya maandalizi ya vitu vya kimwili kwa ajili yao. Inawezekana wakati huu ulitofautiana na wakati uliotangulia ambapo Hagari alienda ndani ya nyika, ya kwamba wakati huu yeye aliondoka akiwa na gawio la mkate (labda hiyo ikigusia maana ya vyakula vya namna-namna) na maji—ambavyo viliandaliwa na Abrahamu. Ni dhahiri kwamba yeye alipotea mahali fulani “katika ile nyika ya Beer-sheba,” na magawio yake yaliisha kabla yeye hajapata kimoja cha vile visima vya eneo lile. Lakini muhali wake haukuondoa sifa njema kwa Abrahamu, kwa maana yeye alikuwa amefanya ‘maandalizi kwa ajili ya wale ambao walikuwa wake mwenyewe,’ hata kwa kuelekeana na mwenendo mbaya ambao ulitaka wao watolewe katika nafasi ya kuwa watu wa nyumba yake.—Mwanzo 21:10-21.
[Ramani/Picha katika ukurasa wa 31]
(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)
Bahari Kuu
Karneku
Megiddo
Yerusalemu
Hebroni
Beer-sheba
Bahari ya Chumvi
Negebu
[Credit Line]
Hii inategemea ramani ambayo haki ya unakili ni ya Pictorial Archive (Near Eastern History) Est. and Survey of Israel
[Picha]
Wadi Zin, bonde la mto mkavu kusini mwa Beer-sheba