Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gm sura 1 kur. 4-11
  • Kwa Nini Uisome Biblia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Uisome Biblia?
  • Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kitabu Chenye Kuuzwa Zaidi ya Vyote
  • Kitabu Chenye Uvutano
  • Yachukiwa na Kupendwa
  • Dai Kwamba Hiyo Ni Neno la Mungu
  • Biblia ya William Tyndale Kwa Ajili ya Watu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • William Tyndale—Mwanamume Mwenye Busara
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Jinsi Biblia Ilivyotufikia—Sehemu ya Pili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Biblia Ni Ujumbe Kutoka kwa Mungu
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
gm sura 1 kur. 4-11

Sura 1

Kwa Nini Uisome Biblia?

Twaishi katika ulimwengu wenye matatizo mengi mno na majibu machache mno. Mamilioni wengi hukosa chakula kwa ukawaida. Hesabu zenye kuongezeka ni wazoevu wa dawa za kulevya. Familia zaidi na zaidi zinavunjika. Daima katika habari ni ngono ya watu wa ukoo na jeuri ya familia. Hewa tunayopumua na maji tunayokunywa vinatiwa sumu polepole. Wakati uo huo, zaidi na zaidi kati yetu wanaathiriwa na uhalifu. Je! unafikiri matatizo kama hayo yatapata kutatuliwa?

1. (Tia ndani utangulizi.) Ni matatizo gani ya ki-siku-hizi yanayoonyesha kwamba ainabinadamu yahitaji mwongozo?

KUONGEZEA hayo, twaishi katika kipindi cha machaguo magumu. Kwa kielelezo, wengi wanapinga vikali utoaji mimba, wakiuita uuaji wa kimakusudi wa asiyezaliwa. Wengine wanahisi kwa nguvu vivyo hivyo kwamba wanawake wana mamlaka juu ya miili yao wenyewe na wapaswa kujiamulia wenyewe jambo kama hilo. Wengi huona ngono ya watu wa jinsia moja, uzinzi, na ngono ya kabla ya ndoa kuwa ukosefu mkubwa wa adili. Wengine wanaamini mazoea hayo ni jambo la uchaguzi wa kibinafsi. Nani anayepaswa kusema wa kweli ni nani na mwenye kosa ni nani?

2, 3. Wengi leo huionaje Biblia?

2 Biblia hutoa uongozi katika mambo ya adili, nayo hueleza juu ya matatuzi yenye mafanikio ya matatizo ya uhalifu, njaa, na uchafuzi. Tatizo ni kwamba, watu wengi hawaioni tena Biblia kuwa mamlaka katika mambo kama hayo. Wakati mmoja, ilisikilizwa kwa heshima—angalau katika nchi za Magharibi. Ingawa Biblia iliandikwa na wanadamu, wakati uliopita walio wengi katika Jumuiya ya Wakristo waliikubali kuwa Neno la Mungu na waliamini kwamba Mungu mwenyewe alikuwa ameyaongoza yaliyomo.

3 Hata hivyo, leo, ni mtindo kutilia shaka kila jambo: desturi, mawazo, adili, hata kuwapo kwa Mungu. Hasa, watu hutilia shaka thamani ya Biblia. Yaelekea wengi huiona kuwa ya kikale na isiyohusu. Ni wenye elimu wachache wa ki-siku-hizi wanaoiona Biblia kuwa Neno la Mungu. Watu wengi wangependelea kukubaliana na msomi James Barr, aliyeandika hivi: “Maoni yangu juu ya muundo wa mapokeo ya kibiblia ni maoni ya kuwa ni kazi ya kibinadamu. Ni taarifa ya binadamu juu ya imani zake.”1

4, 5. Kwa nini ni muhimu kujua kama Biblia ina pumzi ya Mungu au la? Kusudi la kichapo hiki ni nini?

4 Je! hiyo ndiyo rai yako? Unafikiri Biblia ni neno la Mungu, au la binadamu? Hata ujibuje swali hilo, fikiria wazo hili: Iwapo Biblia ni neno la binadamu tu, basi kulingana na kusababu vizuri jibu lililo wazi kwa matatizo ya ainabinadamu halipo. Wanadamu watalazimika tu kujikokota wapite vizuri kwa kadiri wawezavyo, wakitumaini wataepuka kwa njia fulani kujitia sumu ya kujiangamiza au kujilipua katika vita ya nyukilia. Lakini ikiwa Biblia ni Neno la Mungu, basi ndicho kitu tunachohitaji hasa kitupitishe katika wakati huu mgumu.

5 Kichapo hiki kitatoa uthibitisho wa kwamba Biblia ni Neno la Mungu kweli kweli. Na watangazaji watumaini kwamba baada ya wewe kufikiria uthibitisho huo, utatambua kwamba Biblia ina majibu pekee yenye thamani kwa matatizo ya ainabinadamu. Lakini, kwanza, tungependa kuvuta uangalifu wako kwenye mambo fulani ya hakika ambayo, hayo yenyewe, yafanya Biblia istahili ufikirio wako.

Kitabu Chenye Kuuzwa Zaidi ya Vyote

6, 7. Ni mambo gani ya hakika yenye kutokeza juu ya Biblia yanayotaka uangalifu wetu?

6 Kwanza, hiyo ndicho kitabu chenye kuuzwa zaidi, kilichoenezwa zaidi katika historia yote. Kulingana na hariri ya 1988 ya Guinness Book of World Records, nakala zinazokadiriwa kuwa 2,500,000,000 zilichapwa kati ya 1815 na 1975. Hiyo ni tarakimu kubwa sana. Kwa habari ya tarakimu za mwenezo, hakuna kitabu kinginecho chote katika historia ambacho kimepata kukaribia hata kidogo Biblia.

7 Zaidi ya hayo, hakuna kitabu kinginecho chote kimepata kutafsiriwa katika lugha nyingi sana hivyo. Sasa Biblia yaweza kusomwa, yote au kwa sehemu, katika ndimi tofauti zaidi ya 1,800. American Bible Society yaripoti kwamba sasa yafikilika kwa asilimia 98 ya idadi ya watu wa sayari yetu. Wazia jitihada kubwa inayohusika katika kutokeza tafsiri nyingi hivyo! Ni kitabu gani kingine kimepata uangalifu kama huo?

Kitabu Chenye Uvutano

8, 9. Ni semi gani ambazo wengine wametoa zenye kuonyesha uvutano ambao Biblia imekuwa nao?

8 The New Encyclopædia Britannica huita Biblia kuwa “ndiyo labda mkusanyo wa vitabu katika historia ya kibinadamu wenye uvutano zaidi.”2 Heinrich Heine, mshairi Mjerumani wa karne ya 19 aliungama hivi: “Mnurisho wangu umetokana tu na kusoma kitabu fulani . . . Biblia. Kwa kufaa hiyo huitwa Maandiko Matakatifu. Mtu ambaye amepoteza Mungu wake aweza kumpata tena katika kitabu hiki.”3 Katika karne iyo hiyo, mchochezi wa kupinga utumwa William H. Seward alitangaza hivi: “Tumaini lote la maendeleo ya kibinadamu lategemea uvutano unaoongezeka daima wa Biblia.”4

9 Abraham Lincoln, rais wa 16 wa United States, aliiita Biblia kuwa “zawadi bora zaidi ambayo Mungu amepata kumpa binadamu . . . Kama si kwa ajili yayo hatungeweza kutofautisha yanayofaa na yasiyofaa.”5 Sir William Blackstone, mwanasheria Mwingereza alikazia uvutano wa Biblia aliposema: “Juu ya misingi hii miwili, sheria ya maumbile na sheria ya ufunuo [Biblia], zategemea sheria zote za wanadamu, yaani, hakuna sheria za wanadamu zinazopasa kuruhusiwa zipingane na hizi.”6

Yachukiwa na Kupendwa

10. Upinzani kuelekea Biblia umeonyeshwaje?

10 Wakati uo huo, twapaswa kuangalia kwamba hakuna kitabu kinginecho chote ambacho kimeelekezewa upinzani mkali sana na hata chuki katika historia yote. Biblia zimechomwa hadharani, tangu Enzi za Kati kuja mpaka karne yetu ya 20. Na kusoma au kutawanya Biblia kumeadhibiwa kwa kutozwa faini na kufungwa gerezani hata katika nyakati za ki-siku-hizi. Wakati wa karne zilizopita, mara nyingi “uhalifu” kama huo uliongoza kwenye kuteswa-teswa na kifo.

11, 12. Tyndale alionyeshaje upendo wake kwa Biblia?

11 Wenye kulingana na hilo umekuwa ni ule ujitoaji ambao umechochewa na Biblia. Wengi wamestahimili katika kuisoma ijapokuwa mnyanyaso usiokoma. Fikiria William Tyndale, Mwingereza wa karne ya 16 aliyeelimishiwa Oxford University na akaja kuwa mfunzi mwenye kuheshimiwa katika Cambridge University.

12 Tyndale aliipenda Biblia. Lakini katika siku zake, mamlaka za kidini zilisisitiza ibaki katika Kilatini, lugha isiyotumika. Kwa hiyo, ili afanye ipatikane kwa wananchi wenzake, Tyndale aliazimia kutafsiri Biblia katika Kiingereza. Kwa kuwa hilo lilikuwa ni kinyume cha sheria, Tyndale alilazimika kuacha kazi-maisha yake ya kielimu yenye starehe na kukimbilia Continent. Aliishi maisha magumu ya mtoro muda mrefu kutosha kutafsiri Maandiko ya Kigiriki (“Agano Jipya”) na baadhi ya Maandiko ya Kiebrania (“Agano la Kale”) katika lugha yake ya kuzaliwa; lakini hatimaye alikamatwa, akahukumiwa hatia ya kuwa mzushi, na kunyongwa, na mwili wake ukachomwa.

13. Ni jambo gani moja linalofanya Biblia kuwa ya kipekee kweli kweli?

13 Tyndale ni mmoja tu wa idadi kubwa ya watu ambao wamedhabihu kila kitu ili wasome Biblia au kuifanya ipatikane kwa wengine. Hakuna kitabu kinginecho chote ambacho kimechochea wanaume na wanawake wengi hivyo wa kawaida wafikie kuwa na ujasiri mkubwa kama huo. Katika jambo hili, kweli kweli Biblia haina kifani.

Dai Kwamba Hiyo Ni Neno la Mungu

14, 15. Ni dai gani ambalo mara nyingi waandikaji wa Biblia hutoa?

14 Biblia ni ya kipekee pia kwa sababu ya dai linalotolewa na wengi wa waandikaji wayo. Watu mmoja mmoja wapatao 40, kutia ndani wafalme, wachungaji, wavuvi, watumishi wa serikali, makuhani, angalau jemadari mmoja, na tabibu mmoja, walishiriki katika kuandika sehemu tofauti za Biblia. Lakini tena na tena, waandikaji hao walitoa dai lile lile: kwamba walikuwa wakiandika si mawazo yao wenyewe bali ya Mungu.

15 Hivyo, katika Biblia mara nyingi twasoma semi kama vile: “Roho ya BWANA [Yehova, NW] ilinena ndani yangu, na neno lake likawa ulimini mwangu” au, “BWANA [Yehova, NW] wa majeshi, asema hivi.” (2 Samweli 23:2; Isaya 22:15) Katika barua moja iliyopelekwa kwa mwevanjeli mwenzake, mtume Paulo aliandika hivi: “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.”—2 Timotheo 3:16, 17.

16. Biblia huzungumza juu ya maswali gani?

16 Kupatana na dai la kwamba hiyo ni neno la Mungu, si la binadamu, Biblia hujibu maswali ambayo ni Mungu tu awezaye kuyajibu. Kwa kielelezo, hiyo hueleza ni kwa nini serikali za wanadamu zimeshindwa kuleta amani ya kudumu, jinsi wanadamu wanavyoweza kupata uradhi wa kina kirefu zaidi maishani, na mambo ambayo wakati ujao umewekea dunia na ainabinadamu iliyo juu yayo. Basi, ukiwa mtu mwenye kufikiri, lazima uwe mara nyingi umeuliza maswali haya na yanayofanana na hayo. Mbona usifikirie angalau uwezekano wa kwamba Biblia ni Neno la Mungu na hivyo kwa njia ya pekee yaweza kutoa majibu yenye mamlaka?

17, 18. (a) Ni baadhi ya mashtaka gani kwa Biblia yanayozungumzwa katika kichapo hiki? (b) Ni habari gani zaidi zitakazofikiriwa?

17 Twakutia moyo uchunguze kwa uangalifu uthibitisho unaotolewa katika kitabu hiki. Baadhi ya sura zacho zitazungumza uhakiki mwingi wa Biblia unaosikiwa mara nyingi. Je! Biblia ni ya kisayansi? Je! hiyo hujipinga yenyewe? Je! ina historia halisi au ni ngano tu? Je! miujiza iliyoandikwa katika Biblia ilitukia kwa halisi? Uthibitisho wa kufikiri kuzuri umetolewa katika kujibu maswali hayo. Baada ya hilo, maonyesho yenye nguvu ya upulizio wa kimungu wa Biblia yazungumzwa: unabii mbalimbali wayo, hekima yayo yenye kina kirefu, na tokeo lenye kutokeza ambalo imekuwa nalo kwenye maisha za watu. Mwishowe, tutaona tokeo ambalo Biblia yaweza kuwa nalo maishani mwako.

18 Hata hivyo, kwanza, tutazungumza jinsi tulivyoipata Biblia. Hata historia ya kitabu hiki cha kustaajabisha hutoa uthibitisho kwamba chanzo chayo ni zaidi ya kile cha kibinadamu.

[Picha ya ukurasa mzima katika ukurasa wa 4]

[Picha katika ukurasa wa 6]

Biblia ndicho kitabu chenye kutawanywa zaidi na kutafsiriwa zaidi katika historia yote

[Picha katika ukurasa wa 9]

Kama ambavyo kipande hiki cha ubao cha karne ya 15 kinavyotoa kielezi, wengi walichomwa wakiwa hai kwa ajili ya “uhalifu” wa kusoma Biblia

[Picha katika ukurasa wa 11]

Waandikaji wa Biblia walidai kuwa walipuliziwa na Mungu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki