Tumia kwa Matokeo Makala za Kusudi la Pekee
1 Ugawaji wa magazeti unaongezeka kwa kutobadilika. Uchapaji wa 1979 wa magazeti 394,899,446 uliruka kufika 585,369,060 katika 1987, karibu ongezeko la asilimia 50, au magazeti zaidi 190,469,614 yalichapwa katika 1987 kuliko 1979! Na zaidi ya nakala 1,135,585,000 za Mnara wa Mlinzi na Amkeni! zilichapwa katika miaka miwili iliyopita.
2 Kwa tumizi la rangi kamili, maendeleo yenye kutazamisha katika sura yalitokea katika Mnara wa Mlinzi wa Januari 1986 na katika Amkeni! (Kiingereza) katika Januari 1987. Je! wewe umethamini hilo? Wengi wamethamini, nao wametuambia hivyo. Swali ni, Je! tunaweza kutumia magazeti yetu kwa matokeo zaidi?
3 Ili kukusaidia ufanye hivyo, Huduma ya Ufalme Yetu itatangaza kimbele makala za kusudi la pekee au makala ambazo huenda zikapendeza sana sehemu mahususi ya watu katika eneo lenu. Madokezo yatatolewa kuhusu nani watakaovutiwa na makala hizo. Wahubiri wakitaka nakala zaidi, hizo zinapasa kuagizwa mara moja.
4 Mathalani, Amkeni! (Kiingereza) la Septemba linazungumzia mada “Wazazi—Mna Mgawo wa Kufanyia Nyumbani Pia!” Makala hizo zapasa kuvutia mwalimu na mkuu ye yote wa shule kwa kuwa makala hizo zinakazia madaraka ya wazazi kushirikiana na mfumo wa shule katika kuelimisha watoto wao. Pia, kila mzazi anaweza kunufaika na habari hiyo. Kwa hiyo huenda kundi lenu likataka kuagiza nakala zaidi.
5 Amkeni! (Kiingereza) la Oktoba 8 litazungumzia kikamili ugonjwa UKIMWI, litapendeza sana watu wengi, kutia na wale wanaofanya kazi ya kitiba. Na Amkeni! (Kiingereza) la Oktoba 22 linazungumzia suala la talaka na haki ya kutunza mtoto. Huenda ukataka kuachia kila mwanasheria na mshauri wa jamaa katika eneo lenu.
6 Kuagizwa kwa haraka-haraka kwa magazeti zaidi kwapasa kuepukwe. Jambo hilo linaweza kufanywa ikiwa mwangalizi wa utumishi anatangulia kuona uhitaji wa kundi na kupeleka maagizo bila kuchelewa.