Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 1/1 kur. 3-7
  • ‘Sauti Yao Ilitoka Ikaenea Katika Dunia Yote’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Sauti Yao Ilitoka Ikaenea Katika Dunia Yote’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Habari Zinazolingana
  • Fanya Tangazo la Hadharani kwa Ajili ya Wokovu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Uungaji-Mkono wa Duniani Pote kwa Suala la Ufalme
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Kutoa Ushuhuda Kunaleta Ongezeko la Ufalme
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Jumla Kuu Mwaka 2012
    2013 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 1/1 kur. 3-7

‘Sauti Yao Ilitoka Ikaenea Katika Dunia Yote’

KATIKA ZABURI 19, Daudi anahimidi matukufu ya uumbaji wa kimwili wa Mungu na kuendelea kutaja uthamini mchangamfu kwa sheria, vikumbusha, maagizo, amri, na maamuzi ya hukumu za Yehova. Mtume Paulo pia alionyesha uthamini kwa mambo hayo. Yeye alinukuu kutokana na zaburi hiyo na akapanua utumizi wayo uhusu kazi ile muhimu ya Wakristo wa kweli. Alisema hivi juu yao: “Sauti yao imetoka, ikaenea katika dunia yote, na maneno yao hata mwisho wa dunia.”​—Warumi 10:18, ZSB.

“Maneno” hayo yanahusu uhai na kifo kwa aina ya binadamu yote leo, kwa maana maamuzi ya hukumu za Yehova yako karibu kufikilizwa juu ya mfumo mbovu wa mambo duniani. (Sefania 2:2, 3; 3:8) Kwa uhakika aina ya binadamu inahitaji kujua juu ya habari njema za Ufalme wa Yehova. Kokote unakotazama leo, kuna ukosefu wa muungamano, kutotii sheria, uhalifu, ukosefu wa adili, jamaa zilizovunjika. Oh, ndiyo, kuna maongezi juu ya amani, lakini zile serikali mbili zilizo kubwa zaidi ulimwenguni zinaendelea kujenga silaha za hali ya juu zaidi, huku hesabu ya washiriki wa ‘klabu ya nyukilia’ ikipanuka ifikie mataifa mengi zaidi. Ni wazi kwamba hali zilizopo duniani zinapatana na “siku za mwisho” zilizoelezwa na Paulo kwenye 2 Timotheo 3:1-5.

Ni nani atakayeokolewa kutoka mborongo huo wa mambo, na jinsi gani? Paulo anajibu kwa uwazi, akinukuu unabii kwenye Yoeli 2:32: “Kila atakayeliitia Jina la Bwana [Yehova, NW] ataokoka.” (Warumi 10:13) Lakini jamii za watu wa dunia zinawezaje ‘kuitia jina la Yehova’? Kwani, wengi sana hata hawajui kwamba Yehova ndilo jina la Mungu! Watu hao wanaweza kusaidiwaje? Paulo anajibu kwamba ni lazima wapelekewe wahubiri.​—Warumi 10:14-16.

Kwa kufurahisha, Yehova amepeleka Mashahidi wake wakaarifu watu kwamba Ufalme wa Mungu u karibu na kwamba utamaanisha wokovu wa kupata uhai wa milele kwa ajili ya wale wanaopata kujua Mungu na Mwanaye, Yesu Kristo. (Isaya 43:10, 12; Luka 21:25, 26, 31; Yohana 17:3) Habari njema hizo zinavumishwa “katika dunia yote.”

Mamilioni wanatii uhubiri huo, kama vile inavyothibitiwa na jumla ya ulimwenguni pote ya 9,201,071 waliohudhuria mkutano uliokifanyia ukumbusho kifo cha Yesu, siku ya Aprili 1, 1988. Wakati wa mwaka huo, kilele cha wapiga mbiu ya Ufalme 3,592,654 kilifikiwa katika shamba la ulimwenguni, na wahudumu wapya 239,268 wakabatizwa​—ongezeko la asilimia 3.6 zaidi ya mwaka uliotangulia. Wamisionari waaminifu waliweka sehemu iliyo kubwa ya msingi wa ongezeko hilo, kama inavyoelezwa baadaye katika gazeti hili. Lakini katika miaka ya majuzi, mamia ya maelfu ya Mashahidi wa mahali-mahali, wale ambao ‘wameamini habari walizosikia,’ wamefyonza pia roho ya upainia na kila siku ‘wanatangaza habari njema za mambo mema.’ Wastani wa Mashahidi 455,561 wamekuwa wakiripoti wakiwa mapainia, hilo likiwa ni ongezeko la asilimia 4.4 kwa mwaka huo. Tokeo ni kwamba, jumla kuu ya saa 785,521,697 zilitumiwa katika kuhubiri, hiyo ikiwa ni zaidi ya maradufu ya jumla ya saa zilizokuwako miaka 6 iliyopita.

Orodha iliyo katika kurasa nne zinazofuata za gazeti hili inaonyesha kirefu jinsi uhubiri huo ulivyoenea sana. Sisi tunakualika wewe uchunguze ripoti hiyo ya 1988 ya utendaji wa Kikristo ulimwenguni pote.

[Chati katika ukurasa wa 4-7]

RIPOTI YA MWAKA WA UTUMISHI WA 1988 WA MASHAHIDI WA YEHOVA ULIMWENGUNTI POTE

(Ona Buku lililojalidiwa)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki