Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/91 kur. 1-2
  • Zoea Ujitoaji Kimungu Kama Alivyofanya Kristo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Zoea Ujitoaji Kimungu Kama Alivyofanya Kristo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UWE MWENYE BIDII NA UHODARI
  • UJITOAJI KIMUNGU, NJIA YETU YA MAISHA
  • Fuata Kielelezo cha Yesu cha Ujitoaji Kimungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Tieni Ujitoaji Kimungu Katika Uvumilivu Wenu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Ongezeni Kwenye Uvumilivu Wenu Ujitoaji-kimungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Karibu Kwenye “Ujitoaji Kimungu” Mikusanyiko ya Wilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1991
km 6/91 kur. 1-2

Zoea Ujitoaji Kimungu Kama Alivyofanya Kristo

1 Usemi wa Biblia “ujitoaji kimungu” hurejezea staha yetu yenye kina kumwelekea Yehova Mungu na utumishi wa ushikamanifu kwake. Kielelezo chenye kutokeza zaidi cha ujitoaji kimungu alikuwa Bwana wetu Yesu Kristo.

2 Kwa mwendo wake wa maisha hapa duniani, Yesu alijidhihirisha mwenyewe kuwa yule mtu wa ujitoaji kimungu kamili. Kwa hiyo, twafanya vema kufikiria mambo fulani juu ya maisha yake, hasa kama yanavyohusiana na daraka lake akiwa mnenaji mwenye kutokeza zaidi wa Yehova Mungu.

UWE MWENYE BIDII NA UHODARI

3 Yesu alikuwa mwenye bidii katika kutangaza yale ambayo Isaya 61:2 hueleza kuwa ‘mwaka wa nia njema upande wa Yehova.’ Kwa kufuata kielelezo cha Yesu, sisi twapaswa kushiriki kwa bidii katika kazi hii yenye kuokoa uhai wakati wa siku za mwisho za huu mfumo mbovu wa mambo. Ni lazima pia tuwe hodari kama alivyokuwa Yesu. Kwa nini? Kwa sababu ujumbe wa Ufalme tutangazao hupiga kwa nguvu sana na wengine hawaupendi, hasa wakati tunenapo juu ya siku ya kisasi cha Yehova.

4 Ili kutusaidia tunene kwa ujasiri na kuonyesha ujitoaji kimungu, twahitaji roho na mwelekezo wa Yehova. Kwenye Luka 4:18, Yesu alisema: ‘Roho ya Yehova i juu yangu.’ Kwa roho na baraka ya Yehova, sisi pia twaweza kuzoea ujitoaji kimungu na kumpendeza Yehova. Kuzoea jambo humaanisha kuwa na zoea la kulifanya. Humaanisha kwamba jambo fulani limekuwa njia yetu ya maisha ya kila siku. Ujitoaji kimungu lazima uwe njia ya maisha kwa watumishi wa Mungu. Mtume Paulo alitaarifu hivi: “Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.”—1 Kor. 10:31.

UJITOAJI KIMUNGU, NJIA YETU YA MAISHA

5 Nyakati zote lazima sisi tusisahau uhitaji wenye kuendelea wa kumwiga Kristo kwa kutumia kwa faida fursa kushiriki habari njema na wengine. Tufanyapo hivyo wakati wa mwezi wa Juni, inapendekezwa kwamba tuonyeshe kitabu Mankind’s Search for God, au Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya Mwana-Mfalme wa Amani katika Kiswahili.

6 Huenda ukataka kutumia Kichwa cha Mazungumzo kilichoonyeshwa katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Desemba 1990. Ikiwa hivyo, inadokezwa kwamba watu wajitambulishapo kuwa washiriki wa kikundi fulani kikubwa cha kidini, twaweza kukubali uhakika huo na, labda, tuseme: “Inapendeza kupata watu wa dini mbalimbali. Kutafuta-tafuta Mungu kwa wanadamu kumefuata pande nyingi tofauti-tofauti. [Ikifaa, kufikia hapo, waweza kurejezea Matendo 17:26, 27.] Je! wewe hukubali kwamba kwa kawaida watu hufuata dini ya wazazi wao, badala ya kumtafuta Mungu wao wenyewe? Yaani, walizaliwa katika dini fulani. Jambo hilo ndilo linaloonyeshwa katika sura ya kwanza ya kitabu hiki Mankind’s Search for God. [Onyesha ukurasa wa 8, fungu la 12.] Kujifunza zaidi juu ya dini nyinginezo ni jambo lenye kuarifu na kuelimisha. Kitabu hiki kinaeleza mwanzo, mazoea, na mafundisho ya zile dini kubwa-kubwa za ulimwengu.”

7 Njia yetu ya maisha yatutaka si kutangaza tu siku ya kisasi cha Yehova na mwaka wa nia njema bali pia kudhihirisha ujitoaji kimungu katika maisha yetu ya binafsi na ya familia. Ni lazima tumwige Yesu, tukifundisha wengine kwa kielelezo ujitoaji kimungu ni nini hasa. Kwa kufuata kielelezo cha Kristo cha ujitoaji kimungu, sikuzote sisi tutajitahidi kuwa na kusudi linalofaa katika kila jambo tufanyalo, tukimsifu Yehova na kujithibitisha kuwa watumishi wake washikamanifu.

8 Kuzoea kwetu ujitoaji kimungu na kusaidie wengine katika kutafuta-tafuta Mungu kwao na kuelekeza wanyofu kwenye maarifa ya kumjua Yehova, yule Mungu wa kweli.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki