Kuwa na Shughuli Nyingi Katika Utumishi wa Yehova
1 Tuna pendeleo kweli kweli la kumtumikia Yehova. Tukiwa tumepata maarifa sahihi juu yake na Mwana wake wa pekee, Yesu, tunasukumwa na upendo kujitoa wenyewe kikamili katika kufanya mapenzi Yake. (Yn. 17:3) Huenda tukachoka, lakini Yehova hutupa uwezo ili kwamba tujawe na nguvu kamili.—Isa. 40:29.
2 Tunawezaje kuonyesha vema kabisa uthamini wetu kwa upendo mkuu ambao Yehova Mungu na Yesu Kristo waonyesha kutuelekea? (2 Kor. 5:14, 15) Njia ya msingi ni kwa kumwiga Yesu, ambaye alitoa ushuhuda juu ya jina na Ufalme wa Baba yake bila kuchoka. (1 Pet. 2:21) Ikiwa sisi tuna imani yenye nguvu, maisha zetu zitaambatanishwa na kazi iliyopewa na Mungu ya kuhubiri habari njema.—Mt. 24:14.
3 Je! kuna kiwango cha chini cha wakati tunaopaswa kutumia katika huduma ya shambani? Hali hutofautiana. Huenda tukazuiwa na umri mkubwa sana, afya mbaya, au madaraka ya familia. Hata hivyo, sisi sote tunatakiwa tuwe wenye moyo wote katika utumishi wetu kwa Yehova. Hii yamaanisha kwamba kila mtu mmoja mmoja apaswa aonyeshe kina cha ujitoaji wetu na uhalali wa wakfu wetu kwa kufanya yote tuwezayo katika utumishi. (2 Tim. 2:15) Kuna fursa zilizo wazi kwa kila mmoja wetu kulingana na hali za mtu mmoja mmoja. Baadhi yazo ni zipi?
4 Njia za Kupanua Huduma Yetu: Kwanza twapasa tupendezwe na kufanyia maendeleo ubora wa huduma yetu. Hili laweza kutimizwa kwa kukuza ustadi zaidi ukiwa mwalimu. Moja la malengo ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ni kutusaidia kuwa wenye matokeo zaidi katika huduma ya shambani. Je! sisi hufikiri kuhusiana na huduma ya shambani tunapotayarisha migawo yetu? Je! sisi hutumia mashauri tunayopokea ili kwamba tufanyie maendeleo utumishi wetu binafsi? (sg-SW kur. 96-9) Vivyo hivyo, madokezo mengi kwa ajili ya huduma ya shambani yanatolewa wakati wa Mkutano wa Utumishi. Acheni tutumie hayo upesi iwezekanavyo.
5 Halafu, fikiria uwezekano wa kurekebisha hali zako ili kushiriki katika kazi ya upainia msaidizi au ya kawaida. Kufanya hivyo bila shaka kutakufanya uwe na shughuli nyingi katika utumishi wa Baba yetu, Yehova. (1 Kor. 15:58) Namna gani ikiwa huwezi kupainia? Unaweza kuonyesha roho ya upainia kwa kukuza upendo wa kweli kwa huduma na hangaikio la ndani sana kwa watu katika eneo. Waweza pia kutumia kila fursa kusaidia wenye mioyo minyofu kujua Yehova na makusudi yake ya ajabu kwa kufanya ziara za kurudia na kuongoza mafunzo ya Biblia.
6 Kuitikia mwito wa kutumika mahali penye uhitaji mkubwa zaidi kwaweza pia kuwa sehemu ya maendeleo yetu. (Isa. 6:8) Wale ambao wamehamia kwenye kundi lililohitaji msaada kwenye baraza la watumishi au ambalo lilikuwa likitafuta msaada katika kueneza eneo lalo wamepokea baraka nyingi kikweli.
7 Tulipojifunza kweli hapo kwanza, upendo kwa Yehova na Yesu Kristo ulitusukuma kufanya marekebisho makubwa maishani mwetu. Sasa, tunapokua katika uthamini wetu wa Baba yetu wa kimbingu na wa kile Mwana wake alichotenda kwa ajili yetu, je! kuna marekebisho mengine tunayoweza kufanya ili kupanua huduma yetu? Acheni tujitoe wenyewe kila mmoja kwa kuwa wenye shughuli nyingi katika utumishi wa Yehova.—Rum. 12:11.