Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/91 uku. 2
  • Mikutano ya Utumishi kwa Desemba

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano ya Utumishi kwa Desemba
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Desemba 2
  • Juma Linaloanza Desemba 9
  • Juma Linaloanza Desemba 16
  • Juma Linaloanza Desemba 23
Huduma Yetu ya Ufalme—1991
km 12/91 uku. 2

Mikutano ya Utumishi kwa Desemba

Juma Linaloanza Desemba 2

Wimbo 168

Dak. 12: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. “Shule ya Huduma ya Ufalme Huandaa Elimu ya Kitheokrasi.” Tia moyo kuwe na utegemezo wa utendaji wa kutoa magazeti Jumamosi hii.

Dak. 15: “Kupata Faida Zote za Kitheokrasi Desemba Huu.” Hotuba na mazungumzo ya familia.

(Dak. 3) Mwenyekiti azungumzia mafungu mawili ya kwanza na kutoa utangulizi wa mazungumzo ya familia. Hali ya kiroho ya familia haipaswi kupuuzwa wakati wa kipindi hiki. Vichwa vya familia vyapaswa kuhakikisha kwamba mahitaji ya kiroho yanashughulikiwa nyakati zote.—Kumb. 6:6, 7.

(Dak. 10) Mazungumzo ya familia yanayoshughulikia mambo makuu katika mafungu 3-6. Kichwa cha familia azungumza na familia mipango inayohitajiwa kuhakikisha kwamba kipindi hiki kitatia ndani utendaji wa kiroho. Mshiriki mmoja wa familia alipata mahali na saa za mikutano ya kundi la sehemu ambayo wangezuru. Familia ina fasihi ya kutosha kushiriki katika huduma ya shambani pamoja na kundi hilo, kutia ndani na kutumia kwa faida fursa za kutoa ushuhuda wa kivivi hivi. Wataja hali ambazo yamkini kuzikuta zinazotokeza fursa za kutoa ushuhuda. Kichwa cha familia aelekeza fikira kwenye mipango ya kuhudhuria “Wapendao Uhuru” Mkusanyiko wa Wilaya na kuwakumbusha kwamba mwishoni mwa kila siku ya mkusanyiko, watapitia mambo makuu ya programu ya siku hiyo, naye aeleza faida za kufanya hivyo. Familia yazungumzia kifupi juu ya mambo yanayofaa kutoka kwa nyongeza ya toleo la Huduma ya Ufalme Yetu ya Oktoba kuhusu mwenendo ufaao wakati wa kuhudhuria mkusanyiko. Wote wanatazamia kwa moyo kupata faida zote za kitheokrasi katika utendaji wao wa mwezi huu.

(Dak. 2) Mwenyekiti amalizia kwa habari zilizo katika fungu la 7. Katika mipango yoyote tufanyayo, tuhakikishe kwamba hatutapuuza mahitaji ya kiroho ya familia.

Dak. 18: Kichwa Kipya cha Mazungumzo. Pitia kichwa na maandiko yanayotegemeza. Taja kwamba mhubiri aweza kutumia ama Mithali 1:8 au Zaburi 119:9 ikitegemea ikiwa mwenye nyumba ni kijana au mtu mkubwa zaidi. Mhubiri anayestahili na mwenye ujuzi atoe wonyesho wa utoaji ufuatao uliodokezwa:

“Tunaongea na jirani zetu juu ya mahali pa kupata msaada unaofanya kazi ili kupambana na matatizo ya maisha. Zamani watu waliiendea Biblia. Lakini leo twaishi katika wakati ambao mielekeo inabadilika. Wewe waonaje? Je! waamini Biblia yaweza kuwa yenye msaada katika ulimwengu huu wa kisasa, ulio wa kitekinolojia? (Ruhusu jibu.) Kwa kupendeza, tunahakikishiwa katika maneno haya ya Warumi 15:4 kwamba Biblia iliandikwa hasa ili kutoa mwongozo na maagizo. (Soma) Hata hivyo, Je! hilo linatumika katika ulimwengu wa kisasa ambamo hali ni tofauti sana kwa kulinganisha na nyakati za Biblia? Kwa kweli tekinolojia imefanya maendeleo makubwa lakini kimsingi matatizo ya maisha ni yale yale. Na Biblia hutoa mashauri mema ya kushughulika na matatizo ya maisha. Ona maneno haya katika 2 Timotheo 3:16, 17. (Soma) Ndiyo, Biblia yaweza kutusaidia kulainisha mambo mahali ambapo matatizo ya mahusiano yapo. Kwa mfano, hutia moyo wazazi kutoa nidhamu inayofaa na kutoa mwongozo kwa wachanga wao. Tafadhali soma shauri hili la moja kwa moja kwenye Mithali 1:8. Kwa hiyo baba na mama pia wana daraka la kutia nidhamu na kuwekea watoto wao miongozo. Maarifa sahihi juu ya mashauri mazuri ya Biblia yatawawezesha wazazi kutekeleza daraka hili. Msaada huu wa kujifunzia Biblia, uliokusudiwa watoto, husaidia wazazi na watoto pia kutumia vizuri mashauri mazuri ya Biblia.” Halafu toa toleo la Kitabu Changu.

Wimbo 31 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 9

Wimbo 164

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Pitia Habari za Kitheokrasi.

Dak. 15: Sanduku la Swali-2. Pitio la maswali na majibu likishughulikiwa na mwangalizi wa utumishi. Tafadhali soma mafungu yote.

Dak. 22: Mazungumzo ya maswali na majibu ya makala “Kuwatendea Vijana Yaliyo Mema.” Wahoji wazazi ambao wamelea watoto katika kweli au wanaoweka mfano mzuri kusaidia watoto wao kiroho. Uliza jinsi wanavyoratibu wakati wa funzo, huduma, na tafrija; kile ambacho wameona kuwa chenye matokeo katika kusaidia watoto wao kukuza mwelekeo unaofaa kwa shule za kilimwengu, funzo la Biblia la kibinafsi, huduma ya shambani, kushughulikia madaraka ya migawo ya nyumbani, n.k.

Wimbo 183 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 16

Wimbo 169

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Tia ndani ripoti ya hesabu pamoja na shukrani za Sosaiti kwa michango ya kundi. Tia ndani maelezo ya ripoti ya mwaka na ripoti ya kundi ya Novemba.

Dak. 20: “Kuwa na Shughuli Nyingi Katika Utumishi wa Yehova.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Wonyesho wa familia ya watu wanne. Kwa kutumia kalenda ya 1992, baba azungumza na familia kuhusu kuratibu kwao wakati katika Januari. Yeye afikiria ni siku zipi za kuwekwa kando kwa huduma ya shambani na jinsi atakavyofanya kazi pamoja na kila mshiriki wa familia.

Dak. 15: “Upainia—Utumishi Unaothawabisha Sana.” Ipitiwe kwa maswali na majibu. Hoji mapainia wawili. Ni vipingamizi vipi walivyolazimika kushinda ili kuingia katika utumishi wa upainia? Ni nini kilichowasukuma kupainia? Ni nini kimewasaidia kuwa na mafanikio katika upainia wao? Watie wote moyo kufikiria hali zao kwa sala.

Wimbo 40 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 23

Wimbo 197

Dak. 13: Matangazo ya kwenu. Toa maonyesho ya jinsi ya kutoa magazeti ya karibuni. Pia zungumzia, “Video Mpya! Jinsi ya Kuitumia.” Dhihirisha mambo makuu katika makala. Rejezea barua ya Oktoba 15, 1991 iliyotangaza kutolewa kwa kifaa hiki kipya cha kujulisha watu juu ya tengenezo la Yehova.

Dak. 17: “Kudhihirisha Imani kwa Matendo Mema.” Makala ya nyongeza ipitiwe kwa maswali na majibu. Ikiwa kundi lenu linapangia mradi wa kujenga Jumba la Ufalme ruhusu kuwe na wakati wa kupitia mafungu 6 hadi 11 ya makala ya nyongeza “Fungu Lako Katika Kujenga kwa Ajili ya Wakati Ujao” kama inavyopatikana katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Desemba 1990. Ikiwa tayari mna Jumba la Ufalme lenu kazia fikira kazi ya kurekebisha inayohitaji kufanywa na jinsi kundi lenu linavyoweza kusaidia makundi mengine kifedha kujenga Jumba la Ufalme.

Dak. 15: Sanduku la Swali-1. Ishughulikiwe na mzee. Kazia kwa nini twapaswa kuelekezea fikira mwenendo wetu kwenye ubatizo na jinsi hilo linavyorudisha utukufu wa Yehova na ujumbe wa Ufalme.

Wimbo 196 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki