Wimbo 115
“Iweni na Upendo Wenye Juhudi Nyingi Nyinyi kwa Nyinyi”
1. Upendo mwingi sana
Unatuvumilisha
Na kupata kibali
kutoka Mungu.
Kwa upendo Yehova
Alimutuma Yesu,
Kuwe uhusiano
Kuwe umoja.
Wachaji wa Yehova
Tuwe wenye upendo,
Katika huu wenye
chuki mufumo.
Tukifuata Yesu,
kuwe upendo mwingi
Na ndiyo njia bora
—Kama Yehova, Kama Yehova.
2. Upendo wa halisi
Hauudhiki hasha,
Unaleta heshima
Kwa ndugu zetu,
Ni wenye kusubiri
Unatia wengine,
Haulalamikii
Wachaji Mungu.
Tuzidishe upendo,
Mwisho uko karibu
Upanuke ufike
Kwa wanadamu!
Tupendane sisi kwa
Hekima ya kimungu.
Kama Mungu tupende
Kwa umilele Kwa umilele.