Je! Aprili Utakuwa Mwezi wa Pekee Kwako?
1 Mara nyingi huwa tunarejezea miezi ya Machi na Aprili kuwa kipindi cha Ukumbusho. Kwa kuwa mwadhimisho wa Ukumbusho huwa wakati huu wa mwaka, watu wa Yehova wanachochewa kuongeza ushiriki wao wa utumishi wa shambani.
2 Baadhi ya waliojiandikisha kuwa mapainia wasaidizi katika Machi wataendelea na kuungwa na wengine katika huduma hiyo iliyopanuka wakati wa Aprili. Iwapo unaweza kushiriki, ombi lako lapasa litolewe bila kukawia.
3 Hata wale wasioweza kupainia wanaweza kuufanya Aprili kuwa mwezi wa pekee kwa kuongeza utumishi wao wa shambani. Kwa kweli, kuna mengi ya kufanywa. Labda wahubiri wa kundi na mapainia wanaweza kualika wahubiri wapya wasiobatizwa wahubiri pamoja nao shambani. Jitihada ya ziada yapaswa ifanywe kuwaalika watu wote wanaopendezwa kwenye Ukumbusho Aprili 17.
4 Kwa kuwa chonjo kuwaalika wapya wanaohudhuria, huenda ukaweza kuanzisha funzo lingine la Biblia. Kwa baraka ya Yehova juu ya jitihada zako zilizoongezeka, huduma yako itakuwa na mazao na Aprili utathibitika kuwa mwezi wa pekee kwako.—Zab. 34:8; Mit. 10:22.