Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 10/15 kur. 17-23
  • Wateteaji wa Kweli ya Ufalme Wakusanyika

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wateteaji wa Kweli ya Ufalme Wakusanyika
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kweli ya Ufalme Yakaziwa
  • Wahudumu (Maminista) wa Kweli ya Ufalme
  • Kuishi Kupatana na Kanuni za Kweli
  • Kuishika Sana Kweli ya Kiunabii
  • Wakristo Huabudu kwa Roho na Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Kwa Kweli ni Nani Walio na Kweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Wamejitolea Kufuata Njia ya Mungu ya Maisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Walimu wa Neno la Mungu Wahimizwa Watimize Kazi Yao
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 10/15 kur. 17-23

Wateteaji wa Kweli ya Ufalme Wakusanyika

WATU wa Yehova ni mabingwa-wateteaji wa kweli ya ufalme. Wao wanaifurahia sana. Zaidi ya hilo, sikuzote wanashangilia wakati wanapokaribishwa wahudhurie kusanyiko fulani la pekee lenye kudhaminiwa na Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi, kwa maana wanajua kwamba kitakuwa kipindi cha ushirika, kutiana moyo na kupata mashauri yenye mafaa. Kwa uhakika “Kweli ya Ufalme” Makusanyiko ya Wilaya ya mwaka wa 1982 yalionyesha hivyo.

Kweli ya Ufalme Yakaziwa

Wakati wa kukusanyika na kutulia ili kusikiliza kipindi cha kufungua cha alasiri ya Alhamisi, wajumbe wa kusanyiko walizidi kuwa na matazamio walipokuwa wakiangalia programu iliyopigwa chapa na kutazama vichwa vingi vya maana ambavyo vingezungumzwa. Kwa kweli, alasiri nzima hiyo “Kweli” ingekaziwa​—si kweli kwa ujumla tu, bali “Kweli ya Ufalme,” ambayo inachukua ndani yayo makusudi ya Yehova Mungu kuhusiana na mwanadamu, dunia, ulimwengu mzima wote na Jina kuu Lake mwenyewe.

Kwa hiyo mkazo ulitiwa juu ya kuijua kweli na kutenda kupatana kabisa na maarifa hayo ya kuijua. Ni kweli kwamba inahitajiwa kabisa kupata maarifa sahihi ya kujua mafundisho ya msingi ya Biblia, lakini shabaha ni kuwezesha waabudu wa Yehova wawafunze vizuri mafundisho hayo watu wanaowakuta katika kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba. Ni jambo la maana sana pia kufahamu kwamba Yehova ndiye Mungu wa pekee wa ukweli, ndiye chanzo halisi cha kweli yote, na kwamba anapingwa na maadui waovu wasioonekana wanaotumia hila nyingi ili kugeuza watu wamwache Mungu na uadilifu! Sana-sana wasikilizaji walithamini kwa kujifunza juu ya njia za kunyemelea polepole zinazotumiwa na Ibilisi na mawakili wake wanapojaribu kumomonyoa imani yetu.

Katika programu hiyo njia ya kupigana na roho waovu hao na kupata ushindi ilionyeshwa. Ni lazima sisi sote tutambue kwamba adui anajaribu kukuza roho ya kujitegemea wenyewe kwa uchoyo, kutaka kuwa na ubinafsi, na pia kututia katika mtego wa uasherati. Tunahitaji kumjua na kumpenda Mungu na kuwa na chuki ya mambo anayoyachukia. Ikiwa tunalichukua jina lake, kwa uhakika hatutataka kumletea suto yeye wala kundi lake la mashahidi washikamanifu. Juu ya yote, tunahitaji kujipatia-patia nguvu kutokana naye kupitia sala yenye bidii, na tunahitaji kukaa karibu nyakati zote na tengenezo lake lionekanalo lenye ulinzi.

Hotuba ya msingi ya kusanyiko ilionyesha wazi suala la maana kabisa ambalo muda fulani baadaye ni lazima kila mtu ajichagulie kama ataliunga mkono au sivyo. Uchunguzi ni ama kuwa upande wa Shetani, makundi yake ya kishetani na matengenezo yake yote ya kilimwengu pamoja na porojo zao au kuwa upande wa Yehova Mwenye Enzi Mkuu Aliye Mweza Yote na ahadi zake bora zitakazotimizwa na ufalme wake. Karibuni suala hilo litafanyiwa uamuzi limalizike. Hakuna nafasi ya kukaa katikati bila kuunga upande wo wote mkono. Tukichukua hatua bila kukawia na kwa kutegemea matazamio mazuri tutakuwa na uhakikisho wa kupata ulinzi na baraka kwa Yehova.

Wahudumu (Maminista) wa Kweli ya Ufalme

Hicho ndicho kilichokuwa kichwa cha programu ya Ijumaa, na kwa uhakika kilisaidia kila mtu atambue kwamba mapenzi ya Yehova ni kwamba sisi tuwe wahudumu (maminista) wa ufalme wake, kuutangaza ufalme huo nyumba kwa nyumba na hivyo tustahilishe wengine zaidi wajiunge nasi katika huduma hiyo yenye pendeleo. Kwa sababu ya uharaka wa wakati tunamoishi, inatupasa sisi sote tutafute njia za kuongeza ushiriki wetu katika utumishi huo tuliopewa na Mungu, tukiwa wahubiri wa nusu-wakati au wakati wote. Maonyesho fulani yalionyesha namna fikira za bidii zinavyoweza kuelekezwa kwenye uhitaji wa kupanua “utumishi mtakatifu” wetu tukiwa watu mmoja mmoja na jamaa-jamaa.​—Warumi 12:1, NW.

Alasiri hiyo wahudumu wote wa Yehova walionywa ya kwamba maadui wanaopaswa kujihadhari nao si wale wenye kuonekana wazi-wazi ‘huko nje’ bali ni wale wanaojisema kuwa wa upande wetu na kumbe wanatumia ujanja kujaribu kulegeza imani na utumishi wetu. Akasema msemaji: “Wanatoa wazo la kwamba, kwa kuwa Yehova ni Mungu mwenye upendo sana, anatutaka tuwe watu wema tu, tuwatunze wengine kimwili, tupende jirani zetu, na basi.” Maoni ya namna hiyo yanaweza kuwa hatari, kwa maana hayaifikirii amri iliyowekwa juu ya kila mmoja wa wafuasi wa Kristo, yaani: “Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote.”​—Mathayo 28:19, NW.

Wengine wanatia shaka wakisema hakuna uhitaji wa kuwa na tengenezo na kudai kwamba mtu akijisomea Biblia yeye mwenyewe tu, hiyo imetosha. Ukosefu wa upatani wa maoni hayo unaonekana wakati watu hao wanaposonga mbele na kuanzisha tengenezo lao wenyewe na kufuata mwendo wa kujifunza waliojiamulia wenyewe, kwa kutegemea hekima ya kibinadamu.

Tunapokabiliwa na ubishi mbaya huo, Maandiko Matakatifu yanatupa shauri la wazi juu ya tunalopaswa kufanya: Waacheni wawe hivyo. Waepukeni. Songeni mbele pamoja na huduma yenu yenye thamani kubwa. (Mathayo 15:14; Warumi 16:17, 18) Kubishana vikali mbele ya watu pamoja na wale wenye kuleta migawanyiko kungeonyesha ukosefu wa uamuzi mzuri. Kila mmoja wetu anapaswa kutimiza fungu lake asaidie wale wa nyumba ya imani waendelee kuwa na nia inayofaa kuelekea wale wanaotaka kuharibu sifa ya Yehova, ya tengenezo lake na ya watu wake waliopangwa kitengenezo. Utangazaji wa ufalme utamalizwa kwa mafanikio, kwa maana Kristo Yesu aliahidi atakuwa pamoja na watumishi wake “siku zote mpaka umalizio wa mfumo wa mambo.”​—Mathayo 28:20, NW.

Mchezo wa kuigizwa ulioonyeshwa siku ya Ijumaa uliwaacha watu wengi wakiwa na machozi ya kuguswa moyoni. Walivutwa sana kwa kuona fungu ambalo watoto waliofundishwa vizuri wanaweza kutimiza katika kusaidia wasiopendezwa warekebishe njia yao ya kufikiri na kutambua ubora wa kukubali na kufuata mashauri ya Mungu!

Ilifaa sana baada ya mazungumzo hayo yote ya “Wahudumu wa Kweli ya Ufalme” tukawa na nafasi ya kutumia wakati fulani katika kuhubiri nyumba kwa nyumba mwanzoni mwa jioni hiyo. Baadaye wahubiri wengi walieleza kwa furaha kwamba walikaribishwa vizuri na wenye nyumba. Ni kama alivyosema mhubiri mmoja: “Huo ulikuwa umalizio wenye kuridhisha wa siku iliyotumiwa kwa kuifikiria huduma yetu tukufu.”

Kuishi Kupatana na Kanuni za Kweli

Hicho ndicho kilichokuwa kichwa cha programu ya Jumamosi, nacho kilikazia kufuata kwa matendo mambo tuliyokuwa tukijifunza kwenye kusanyiko hilo. Ni lazima sisi mabingwa-wateteaji wa kweli ya ufalme tuishi kupatana na kanuni za kweli hiyo.

Baada ya mazungumzo ya andiko la siku hiyo, tulifurahia kikoa cha wasemaji watatu. Kilionyesha wazi matakwa ya Mungu kwa vijana na wazee, watoto na wazazi. Ilionekana kwamba kuendesha mambo ya kijamaa kupatana na kanuni za Yehova ndiyo njia ya mafanikio. Upendo, ambayo ni sifa kubwa zaidi ya Wakristo wa kweli, unawezesha watoto na wazazi kufanya mambo kwa ushirikiano wenye upatani.​—Yohana 13:34, 35.

Tulipokea vikumbusho vya wakati unaofaa kupitia hotuba na maonyesho juu ya hatari ya wendekevu. Wendekevu umefungua njia ya kuingia kwa matatizo na magumu mengi na ni lazima yakabiliwe kwa kushikilia kanuni za Biblia kwa uthabiti. Kwa hiyo, ni lazima tukaze sana pande nyingi za maisha yetu ya Kikristo. Ingawa kufanya hivyo kunatuwekea vizuizi, ilionekana kwamba kwa kufanya hivyo hali nyingi zenye kuleta sana majaribu ziliepukwa ama zikashughulikiwa kwa mafanikio.

Habari moja iliyokaziwa fikira za pekee ni ile ya muziki. Tulijifunza kwamba muziki unaweza kutukuza viumbe vya kiroho au unaweza kuvunja heshima. Umetumiwa kukaza ndani ya watu Ushetani na ufisadi. Basi, ni lazima Mkristo ajihadhari aone ni muziki wa namna gani anaosikiliza sawa na vile anavyochunguza ni mambo gani anayotazama katika televisheni.

Vipindi vya Jumamosi vilimaliziwa kwa ile hotuba yenye kusisimua yenye kusema “Ile Kweli Inayoongoza Kwenye Paradiso ya Kidunia.” Msemaji alitukumbusha uhakika wa kwamba Kristo Yesu alionyesha kungekuwa na ufalme na paradiso ya kidunia. Kwa mfano, Kristo alishuhudia mbele ya Pilato kwamba Yeye kweli alikuwa ni mfalme na alitumwa aishuhudie kweli hiyo. Halafu, baada ya mkosaji mwenye kuning’inia juu ya mti kando yake aliposema, “Yesu, nikumbuke mimi wakati uingiapo katika ufalme wako,” Yesu alijibu hivi: “Kweli kweli mimi nakuambia leo, Utakuwa pamoja na mimi katika Paradiso.” (Luka 23:42, 43, NW; Yohana 18:36, 37) Tumaini la kuishi milele katika paradiso ya kidunia linaonwa kuwa la kweli kabisa na wale wanaompenda Mungu na uadilifu leo!

Kuishika Sana Kweli ya Kiunabii

Msemaji wa mwanzoni-mwanzoni katika programu ya Jumapili asubuhi alionyesha kwamba sisi leo tunakabiliwa na hali inayofanana na ile iliyowakabili Wakristo katika karne ya kwanza. Walikuwako wengine waliotaka kurudia mambo manyonge ya msingi, mambo yenye kuhusu falsafa ya wanadamu na mabishano yanayohusu maneno​—mambo yasiyojenga wala yasiyohusiana na kupata wokovu. (Wagalatia 4:9) Hatari za kisasa zinatia ndani kujiruhusu tuwe na tamaa ya kutaka vitu visivyo vya lazima maishani mpaka iyanase mawazo yetu yote na wakati wetu; kutafuta tafrija za kilimwengu ambazo mara nyingi zinakuwa chafu na pia zenye kula wakati; kuchezea-chezea uasherati pamoja na hatari nyingi za huo. Kupata uzima wa milele kunategemea kama sisi tutaishika sana ile kweli na njia ya kweli hiyo. Watu fulani ambao wamekuwa mabingwa-wateteaji wa kweli ya ufalme kwa muda mrefu wakiwa watendaji walihojiwa kwa faida ya wahudhuriaji wote. Maelezo ya mambo waliyoona yalionyesha kwamba inawezekana mtu awe mshikamanifu kwa Yehova na kanuni zake hata anapokabiliwa na majaribu na magumu.

Ndipo ikafuata hotuba yenye kichwa kilichosema “Wakisongamana Pamoja Katika Mpango wa Vita.” Kichwa hicho kilitumia habari za andiko lililo kwenye 1 Mambo ya Nyakati 12:38 (NW). Kwa kuwa msemaji alieleza sana uhakika wa kwamba Wakristo wako katika vita na wanatazamiwa wawe waminifu wakiwa askari za Yesu Kristo, wakivumilia magumu na kuendeleza umoja katika safu zao, mwito wa pigano wenye kusikiwa wazi ulitolewa. Tangu tulipoandikwa katika jeshi la Bwana, hasa kuanzia wakati wa wakf na ubatizo wetu, kila utendaji mwingine wa maisha unapasa kuwekwa chini ya utumishi tunaompa Jemadari Mkuu wa Yehova, Yesu Kristo. Kama Kiongozi na Amiri wetu ni lazima tukumbuke kwamba jina takatifu la Mungu na Mfanyi wetu linahusika katika vita hiyo.

Kwa kuwa yetu ni vita ya kiroho, silaha zetu pia ni za kiroho lakini “zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome,” kama vile falsafa za bure tu za kibinadamu, mambo yaliyo kinyume cha kweli ya lile Neno, mafundisho yenye hila ya mashetani na mavutano ya kutufanya tuweke starehe yetu wenyewe na masilahi yetu mbele ya utumishi wa Yehova. (2 Wakorintho 10:4) Ni kama vile msemaji alivyosema kwa hekima: “Hakika sisi hatuwezi kutia shaka kwamba Jemadari wa Yehova anaiweza kabisa kazi ya kuwatunza wale ambao amewaandika katika jeshi lake! Ikiwa sisi tumelemewa na hangaiko juu ya mahitaji ya kimwili, je! hicho si kikumbusho chenye uharaka cha kwamba tutupie Yehova na Kristo mambo yanayotulemea?” Kusongamana kwetu pamoja katika mpango wa vita kunamaanisha kwamba tufanye ushirikiano wa karibu pamoja na lile tengenezo moja lionekanalo ambalo Yehova analitumia leo. Ni lazima kila mmoja wetu awe na vifaa vya kutosha na kuwa mtendaji katika kuiunga mkono shughuli kubwa ya kiroho kama inavyoelekezwa na yule Kiongozi, Kristo.

Ndipo programu ya asubuhi ilipomaliziwa kwa mchezo wa kuigiza mwingine wa kupendeza sana. Ulionyesha utumishi wa kutokuogopa wa nabii Yeremia akiwa anatangaza muda wa miaka mingi ujumbe usiopendwa na watu walio wengi wa siku zake, kutia na mfalme mwenyewe, wana-wafalme na manabii wa uongo. Tulipokuwa tukimwona Yeremia akielekeana kwa uthabiti na vitisho na jeuri na huku akiwatia wengine moyo waendelee kuwa washikamanifu wa Yehova, je! hicho hakikuwa kikumbusho chenye mkazo kwamba watu wa Yehova leo wanaombwa wadumu kwa uaminifu katika kuutangazia ulimwengu mzima huu ulio chini ya Shetani ujumbe wa hukumu za Yehova zinazokuja mbio-mbio, ujumbe wenyewe ukiwa ni kitu kinachochukiwa kweli kweli na watu wengi? Lakini, tuna furaha ya kujua kwamba, kwa sababu ya utumishi wa ushikamanifu tunaofanya, watu wengi sana wataokolewa katika kizazi kilichohukumiwa maangamizi kisha wapate usalama na wokovu wa kuingia katika mfumo mpya wa mambo ya Mungu.

Hotuba ya watu wote yenye kusema “Ile Kweli Inayoweza Kukuweka Huru” ilipangiwa kutolewa mwanzoni mwa alasiri. Wasikilizaji wengi wenye hamu walikuwapo wakati msemaji alipozidi kutaja-taja mambo mengi ya uhakika yanayoonyesha kwamba watawala wa ulimwengu huu na watu mashuhuri hawawezi kufutilia mbali wala umaskini, jeuri wala ukosefu wa usalama. Aliendelea kuonyesha kutokana na Maandiko Matakatifu kwamba Yehova, yule Mungu Mweza Yote, ameahidi kufanya yote hayo na mengine mengi, tena ana uwezo mwingi sana wa kuyafanya. Yehova ataondoa visababishi vyote vya maombolezo na machozi, pia afutilie mbali magonjwa, maumivu na kifo kinachotokana na urithi tulioupata kwa Adamu mtenda dhambi. Zaidi ya hilo, Yeye atafanya watu wengi sana warudi kwa kutoka katika kifo. Wao watapewa nafasi ya kuishi milele katika dunia-paradiso.

Halafu, kukawa na marudio mafupi ya karamu ya kiroho yenye kutosheleza ambayo Yehova alikuwa ametuandalia kwenye hilo “Kweli ya Ufalme” Kusanyiko la Wilaya. Kwa uhakika, kikombe chetu cha baraka kutoka kwa Yehova kilikuwa kimejaa na kikawa kikifurika! Nayo matokeo yalikuwa nini? Hapo tulikuwa tayari kuisikia hotuba ya kumalizia iliyotuhimiza sote tuendelee na utangazaji wa kweli ya ufalme maadamu Yehova anaendelea kuiacha njia ikiwa wazi. Sisi tunajua tunaifuata njia iliyo sawa. Katikati yetu wameondolewa wale wenye kutafuta-tafuta makosa, walalamikaji na wenye kujitegemea wenyewe. Sasa Yehova anatubariki kwa kutupa ongezeko, kama tunavyoweza kuona kutokana na ripoti zinazoingia kutoka sehemu zote za ulimwengu. Wahubiri wengi zaidi wanatumia saa zaidi kwenye huduma ya shambani. Wengine wengi zaidi wamo katika utendaji wa painia msaidizi na wa wakati wote. Mafunzo ya Biblia yenye kuongozwa katika nyumba za watu walioanza kupendezwa hivi majuzi yameongezeka kwa njia ya kutazamisha. Hakuna shaka kwamba sisi tunapewa mwelekezo ulio wazi na roho ya Yehova na tengenezo lake.

Tulipokuwa tukiondoka kwenye sehemu za kusanyiko na kuelekea kwenye makundi yetu ya nyumbani, je! hatukujawa na usadikishi mwingi sana kwamba Yehova na Mfalme aliyemweka, Kristo Yesu, wamekuwa pamoja nasi? Je! sisi hatusadiki kwamba wao wametupa misaada kwa ukarimu mpaka tukawa na vifaa vya kusonga mbele kwa umoja tukizitangaza habari njema, tukiwa mabingwa-wateteaji wa kweli ya Ufalme? Sifa yote na utukufu na apewe yule Mungu aliye mwingi wa uadilifu na kweli!

[Picha katika ukurasa wa 18]

Watoto Wakristo wanaweza kusihi mtu kweli kweli!

Kweli! Jina la Mungu ni Yehova

Aliyekuwa mpinzani anaelekeza kidole kuonyesha mahali Jina hilo lipo

[Picha katika ukurasa wa 19]

Yeremia anapigwa na wapinzani

. . . amefungwa katika mikatale

. . . anaokolewa katika shimo la matope

[Picha katika ukurasa wa 20]

Kuagizwa rasmi kuwa wahudumu (maminista) kwa kubatizwa

[Picha katika ukurasa wa 21]

Utumishi mzuri wa kutoa chakula

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki