Uwe Ukijizoeza na Ujitoaji Kimungu Ukiwa Shabaha Yako
1 Shule ya Huduma ya Kitheokrasi hutuzoeza hatua kwa hatua ‘tutumie kwa halali neno la kweli.’ (2 Tim. 2:15) Je! umejiandikisha? Ikiwa sivyo na unastahili, kwa nini usifaidike na uandalizi huo mzuri kwa kujiandikisha sasa?
2 Sehemu ya maana ya shule hiyo ni programu ya usomaji wa Biblia wa kila juma. Ratiba ya funzo lako la kibinafsi lapasa kutia ndani kusoma sura zilizogawiwa katika Biblia hivyo kwa wakati utakuwa umesoma Biblia nzima.
3 Kuanzia na ratiba ya shule ya 1993, usomaji wa Biblia unaoenezwa na Hotuba Na. 2 utasomwa kabisa bila kukatizwa-katizwa. Hilo lamaanisha kwamba mwanafunzi anayeshughulikia hotuba hiyo atatia ndani maelezo katika utangulizi na umalizio wake tu. Ndugu anayegawiwa mambo makuu hapaswi kukazia maelezo yake mistari iliyogawiwa hotuba Na. 2 ili msemaji wa hotuba hiyo aweze kukuza habari yake kikamili juu ya usomaji wa Biblia.
4 Mwangalizi wa shule atatia alama kwenye Shauri la Usemi la wale wanaotoa Hotuba Na. 2, 3, na 4. Hatazamiwi kufuata utaratibu kwenye shauri la usemi lakini aweza kutoa shauri mahususi juu ya mambo ambayo mwanafunzi anahitaji kufanyia maendeleo. Hakuna uhitaji wa kutia alama kwenye shauri la usemi la msemaji anayetoa Mgawo Na. 1, ingawa shauri la faragha laweza kutolewa inapohitajika.
5 Wote wanaostahili wanapaswa watumie kwa kujifaidi maandalizi ya kiroho yanayotolewa na Yehova, kutia na mazoezi yanayotolewa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Mazoezi hayo yaweza kuongoza kwenye huduma yenye matokeo zaidi.—1 Tim. 4:7.