Mikutano Ya Utumishi Kwa Desemba
Juma Linaloanza Desemba 7
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na matangazo yaliyochaguliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Dokeza njia za kuamsha kupendezwa katika magazeti yenye kutokezwa katika utumishi wa shambani mwisho-juma huu.
Dak. 15: “Chochea Wengine Wamtazame Yesu kwa Mkazo.” Hotuba yenye kutia moyo, inayotoa muhtasari wa thamani ya kitabu Mtu Mkuu Zaidi katika kuwasaidia watu wachukue ibada ifaayo.
Dak. 20: “Kutoa Habari Njema—Kwa Kutumia Kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi.” Ishughulikiwe ikiwa mazungumzo yenye ushiriki wa wasikilizaji. Uwe na maonyesho mawili. La kwanza lapasa kutumia utoaji uliodokezwa katika fungu la 3. La pili lapasa kuonyesha kifupi jinsi funzo la Biblia liwezavyo kuanzishwa kwa kutumia kichapo hicho.
Wimbo 205 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 14
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Tia ndani ripoti ya hesabu na shukrani kwa upaji. Pongeza kundi kwa utegemezo wenye ukarimu wa mahitaji ya kwenu na kazi ya Sosaiti ya ulimwenguni pote. Jinsi wakati uruhusuvyo, simulia maono yaliyochaguliwa katika kutumia trakti na labda kitabu Mtu Mkuu Zaidi kuwasaidia watu wachukue ibada ifaayo. Tangaza mipango yoyote ya pekee ya kutoa ushahidi kwa ajili ya Desemba 25.
Dak. 10: “Endelea Kuyanena Mambo Uliyoyaona na Kuyasikia.” Hotuba. Tia ndani maono ya kwenu yaliyochaguliwa yanayohusu kutoa ushahidi vivi hivi.
Dak. 15: “Kutumia Trakti Ili Kuwa na Matokeo Yenye Manufaa.”—Sehemu ya 1. Pitio la maswali na majibu la mafungu 1-8 ya nyongeza. Baada ya fungu 8, toa wonyesho wa kutoa ushahidi vivi hivi kwa kutumia trakti.
Dak. 10: Sanduku la Swali. Hotuba yenye kutolewa na mzee.
Wimbo 71 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 21
Dak. 10: Matangazo ya kwenu; tia ndani tangazo lolote la utoaji ushahidi wa pekee katika Januari 1. Dokeza jambo moja au mawili ya kuzungumzia yanayoweza kutumiwa katika maneno ya utangulizi mwisho-juma huu katika utumishi wa shambani.
Dak. 15: “Fuatia Kupendezwa kwa Utambuzi Wakati wa Majira ya Sikukuu.” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Toa wonyesho wa mambo yaliyomo katika fungu 4.
Dak. 20: “Kutumia Trakti Ili Kuwa na Matokeo Yenye Manufaa”—Sehemu ya 2. Mazungumzo ya maswali na majibu ya mafungu 9-16 ya nyongeza. Baada ya fungu 10, toa wonyesho wa namna ya kuanzisha funzo la Biblia kwa kutumia trakti.
Wimbo 128 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 28
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Toa maelezo pia juu ya ripoti yenu ya shambani ya hivi karibuni na ripoti ya mwaka. Toa wonyesho wa namna ya kutumia fasihi itakayotokezwa kwenu katika Januari.
Dak. 10: “Uwe Ukijizoeza na Ujitoaji Kimungu Ukiwa Shabaha Yako.” Hotuba yenye kutia moyo ikishughulikiwa na mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Eleza kwa wazi jinsi Hotuba Na. 2 inavyopasa itolewe, na uwakumbushe wale wanaogawiwa mambo makuu ya Biblia kwamba hawapaswi kutoa maelezo marefu juu ya sehemu ya Biblia inayogawiwa Hotuba Na. 2.
Dak. 13: “Wewe Waweza Kupata Faraja Katika Nyakati za Taabu.” (w92-SW 7/15 kur. 19-22) Hotuba yenye kutia moyo ikishughulikiwa na mzee.
Dak. 12: Mahitaji ya kwenu. Baraza la wazee lapasa kuamua mambo ya kutokeza.
Wimbo 103 na sala ya kumalizia.