Endelea Kuyanena Mambo Uliyoyaona na Kuyasikia
1 Hata walipotishwa kwa mapigo na kufungwa gerezani, mitume waliwaambia wapinzani wao hivi: “Sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia.” (Matendo 4:20) Walithamini thamani ya matendo na mafundisho ya Yesu.
2 Habari njema kuhusu Yesu na Ufalme wake ni za maana kwa watu leo kama zilivyokuwa wakati huo. Kwa hiyo, twapaswa kutwaa kila nafasi ili kunena juu ya yale tuliyoyaona na kuyasikia kutoka kwa Neno la Mungu. Kwa kawaida watu huwa na hali ya akili iliyo bora zaidi ya kunena juu ya mambo ya kidini wakati wa majira ya sikukuu, na hilo hufungua nafasi za ziada za kutoa ushahidi.
3 Vijana, Neneni Shuleni: Mashahidi wengi wachanga hutumia kwa kujifaidi nafasi za kutoa ushahidi kwa wanadarasa wenzao na walimu. Shahidi mchanga mmoja anayejitahidi sikuzote kuwa chonjo kuhusu vichwa vya mazungumzo vya sasa miongoni mwa wanadarasa wenzake alitumia kwa kujifaidi jambo moja lililotukia shuleni akawaendea walimu na wanadarasa wenzake akiwa na kichapo kilichofaa. Tokeo likawa nini? Aliangusha vitabu 35 katika siku moja! Kwa hiyo tumia nafasi kwa kujifaidi wakati wa muhula wa shule ili kuwawezesha wanadarasa wenzako na walimu wajue jinsi Yesu akiwa Mfalme anayetawala awezavyo kusuluhisha matatizo ya ulimwengu.—Linganisha Luka 2:14.
4 Ikiwa kuepuka kwako kushiriki katika mapokeo ya kidini yanayohusiana na Krismasi kunatokeza tatizo, unaweza kusema hivi:
◼ “Mimi sishiriki katika sherehe za Krismasi kwa sababu sherehe hizo hazimhesimu Yesu akiwa njia yetu pekee ya kupata wokovu na mtu pekee atakayeleta mwisho wa vita na matatizo ya rangi. [Nukuu au soma Matendo 4:12.] Yesu si kitoto tena bali ni Mfalme anayetawala. Kitabu hiki, Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi, kinazungumza juu ya mafundisho na miujiza yote ya Yesu na kinaonyesha jinsi atakavyoleta mwisho wa kuteseka kwa mwanadamu.” Halafu onyesha kielezi katika sura ya 133, na usome fungu la pili katika ukurasa unaofuata. Onyesha mambo mengine ambayo unahisi yaweza kumvutia mtu huyo, na kisha utoe kitabu.
5 Nena na Wanafanya Kazi Wenzako: Ndugu mmoja aliangusha vitabu 63 kwa kuweka tu nakala moja ya kitabu Mtu Mkuu Zaidi kwenye deski lake. Sura yacho yenye kuvutia na kichwa chenyewe huchochea maswali. Waweza tu kumwuliza mfanyakazi mwenzako hivi: “Ni nani ungesema ndiye mtu mkuu zaidi aliyepata kuishi?” Halafu uongeze: “Kitabu hiki kinaeneza mambo yote madogomadogo juu ya maisha mazima ya Yesu, kinazungumza juu ya kila hotuba aliyotoa, kinajibu maswali ambayo wengi huuliza juu ya miujiza yake, na kinatoa mambo mengine madogomadogo yenye kupendeza. Ni pitio kamili ya yale ambayo Biblia hufundisha juu ya Yesu na kinathibitisha bila shaka kwamba Yesu Kristo ndiye aliyekuwa mtu mkuu zaidi aliyepata kuishi.” Halafu rejezea maelezo ya Napoléon juu ya Yesu kama yalivyonukuliwa katika fungu la tatu la utangulizi wa kitabu.
6 Nafasi kama hizo zaweza kutokea za kutolea ushahidi majirani au watu wa ukoo wasioamini. Sali kwamba Yehova atakupa ujasiri na uwezo wa kunena katika wakati ufaao. (Matendo 4:29, 31) Yale tuliyonayo ya kusema juu ya Yesu yatachangamsha mioyo ya watu wenye kufikiri walio na mwelekeo mwadilifu. Tungekuwa na ono gani bora kuliko kumsaidia mwanafunzi mwenzetu, mfanyakazi mwenzetu, jirani, au mtu wa ukoo apate kuwa kwenye barabara inayoelekea kwenye uhai wa milele?—Yn. 14:6.