Wimbo 53
Ongezeko la Theokrasi
1. Theokrasi yazidi, shangilia!
Kuna mupanuko wa ajabu.
Yehova azidi kuimbiwa na
Waenda nuru ya uso wake.
Ni kale mambo yalipoanzia
Kwa Mwokozi kujishusha chini.
Kundi kubwa, ’baki, wamupatia
Sifa yu kwa Mungu kuumeni.
2. Yesu kiti cha enzi akalia;
Mataifa yaja mbele yake.
Enzi ya Mungu atashikilia,
Aponde adui zake wote.
Mushauri, Baba wa Juu sana,
Mungu, Mwana-Mufalme-Amani.
Yah ataleta amani milele.
Aongeze utawala wake.
3. Kuishi sasa ni pendeleo we!
Je! ongezo usifurahie?
Furaha ya kutoa furahia,
Kushuhudia ufurahie.
Onya wakashifu jina la Mungu;
Wa’mbie ’Magedo’ ni karibu.
Endelea kutangaza habari
Njema za Ufalme kwa wapole.