Wimbo 172
Endeleeni Kuutafuta Kwanza Ufalme
1. Ni wenye thamani kwake
Mungu, wa kupendeza,
Ni Ufalme wake Yesu,
Utayanyosha mambo.
Manabii kauona
Kwa taraja, imani.
Leo Yesu atusihi
Tutumai Ufalme.
(Korasi)
2. Pendeleo kushiriki
Huduma ya Ufalme!
Huduma tuliyopewa,
Tuifanye zaidi.
Mbona tunahangaika
Kesho ni njaa, kiu?
Mungu kutupa riziki
’Falme ukiwa kwanza.
(Korasi)
3. Mfumo huu kukoma;
Mupya wa Mungu kuja.
Watu watamusifu Yah;
Dunia Paradiso.
Na tuhubiri Ufalme,
Na Kondoo wajue
Tumaini ni Yehova
Na Theokrasi yake.
(KORASI)
Tafuta Ufalme kwanza
Pia uadilifu.
Yehova tetea kwanza,
Ukiwa mwaminifu.