Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/93 uku. 4
  • Kuwasaidia Wengine Watambue Hazina Iliyo Kuu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuwasaidia Wengine Watambue Hazina Iliyo Kuu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Kitabu Kiandaacho Mwongozo wa Kweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Kurudi Ili Kuchochea Kupendezwa Katika Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Rudi Usitawishe Kupendezwa Katika Ujumbe wa Ufalme
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Sitawisha Kupendezwa Katika Ufalme wa Mungu wa Amani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1993
km 9/93 uku. 4

Kuwasaidia Wengine Watambue Hazina Iliyo Kuu

1 Tunapohubiria wengine habari njema za Ufalme, mojapo malengo yetu, ni kusaidia watu wenye mioyo yenye haki kuthamini thamani bora ya Neno la Mungu. (Flp. 3:8) Fasihi zetu za Biblia hutimiza sehemu ya maana katika kueneza ujumbe wa Ufalme. Kwa mfano, kitabu Kuishi Milele kimesaidia mamia ya maelfu ya watu wamtumikie Yehova kwa sababu ya kweli za Biblia walizojifunza.

2 Huduma yetu yahusisha mengi zaidi ya kumwachia mtu yeyote mwenye nia ya kuichukua fasihi. Twahitaji kujulisha ujumbe kwa njia yenye kuvutia, kusikiliza kwa utambuzi kile asemacho mwenye nyumba, kisha tuwe tayari ‘kumtolea sababu kutoka kwa Maandiko.’—Mdo. 17:2, NW.

3 Hilo Laweza Kufanywaje? Matangulizi yetu yaweza kufungulia wenye nyumba njia ya kuonyesha kama kweli wanapendezwa na Biblia na ujumbe wayo.

Waweza kusema:

◼ “Tunazuru ili kuzungumza maana ya mambo yanayotendeka kati yetu ulimwenguni leo. Miongoni mwa watu wengi kumekuwa na upunguaji wa kupendezwa na viwango vya Mungu vya kuishi vilivyoandikwa katika Biblia. Jambo hili limetokeza kushuka kwa maadili na limeathiri sana mtazamo wa watu juu ya mtu na mwenzake. Je! umeona jambo hilo? [Ruhusu maelezo. Waweza kurejezea visa hususa.] Tafadhali angalia mwelekeo wa wale wanaotajwa katika 2 Timotheo 3:1-5, kisha uniambie kama wafikiri yanapatana na hali za ulimwengu leo. [Soma; ruhusu maelezo.] Je! kuna sababu nzuri ya kutazamia hali bora katika wakati ujao?” Kupendezwa kukionyeshwa, rejezea picha iliyoko kwenye kurasa 12 na 13 za kitabu Kuishi Milele na uelekeze uangalifu kwenye mafungu 12 na 13. Ikiwa kupendezwa si kwingi sana, basi trakti Amani katika Ulimwengu Mpya yaweza kutolewa.

4 Mzazi akija mlangoni, twaweza kuanzisha mazungumzo yetu hivi:

◼ “Tunazungumza na watu wanaotaka kujua jinsi tunavyoweza kukabiliana na matatizo ya maisha ya familia. Sote tunajaribu kufanya yote tuwezavyo, lakini kama kuna jambo liwezalo kutusaidia tufanikiwe zaidi, twalitaka hilo, sivyo? [Ruhusu itikio.] Biblia hutoa mwelekezo kuhusu jambo hilo kama upatikanavyo kwenye Wakolosai 3:12-14. [Soma.] Kwa hiyo, ni jambo gani la lazima ili kufurahia maisha ya familia yenye mafanikio? Angalia jambo ambalo limeandikwa katika kichapo hiki kwenye sura yenye kichwa ‘Kufanikisha Maisha ya Jamaa.’” Soma fungu la 3 kwenye ukurasa 238 wa kitabu Kuishi Milele. Tutafurahi kukuachia kichapo hiki kwa mchango wa. . . . . . . Ikiwa mwenye nyumba ana shughuli au haitikii upesi, jaribu kumtolea gazeti la karibuni ambalo linaongea juu ya mambo ya familia, au trakti Furahia Maisha ya Familia.

5 Hatutaki kamwe kukosa kuelewa kusudi letu la kutoa ushahidi kamili juu ya Ufalme. (Mt. 24:14) Kwa kutumia Biblia vema na uandalizi wa fasihi za kitheokrasi tulizo nazo, kwa uhakika twaweza kutazamia baraka za Yehova katika kutimiza mapenzi yake katika nyakati hizi za maana sana.—Gal. 6:9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki