Wimbo 84
Kazi Kubwa na za Ajabu za Mungu
1. Yehova Mungu, Mwenyezi,
Kazi zako ni tukufu!
Dunia, jua na mwezi
Vyakusifu Mutukufu.
2. U haki katika yote,
Mufalme wetu milele!
Vyasifu viumbe vyote.
Sisi tumupe shukrani.
3. Nani asikuogope,
Jina alipe adhama?
Mushikamanifu Wewe,
Mungu wa sifa daima.
4. Sheria ni nyingi sana!
Zaonyesha haki yako!
’Taifa yakuabudu,
Yaungame jina lako.