Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/93 uku. 12
  • Toa Uangalifu kwa Kupendezwa Kunakopatikana

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Toa Uangalifu kwa Kupendezwa Kunakopatikana
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Kutumia Magazeti Yetu Nyumba kwa Nyumba
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Rudi kwa Shangwe ili Kusaidia Wenye Kupendezwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Ziara za Kurudia Sahili na Zenye Matokeo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Tumia Kitabu Kutoa Sababu Kwenye Ziara za Kurudia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1993
km 10/93 uku. 12

Toa Uangalifu kwa Kupendezwa Kunakopatikana

1 Tunapogawanya magazeti yetu na vichapo vinginevyo vya kitheokrasi, tunaeneza mbali ujumbe ambao Yesu Kristo alipiga mbiu juu yao. Kwa hiyo twapaswa kufanya jitihada ya pekee kumrudia kila mtu anayeonyesha kupendezwa.

2 Ikiwa ulikazia makala hususa katika Amkeni! iliyompendeza mwenye nyumba, zungumzia habari zaidi kutoka kwa makala hiyo unaporudi, mazungumzo yako yakikazia andiko moja kuu na labda fungu moja au mawili. Ikiwa kuna kupendezwa kunakoendelea, taja kwamba Amkeni! hunufaisha familia nzima. Kila toleo hushughulikia habari mbalimbali, kama vile mazingira, kujiboresha, kukabili matatizo ya leo, na maswali yanayowahangaisha vijana. Acha mwenye nyumba ajue kwamba Amkeni! hupatikana kwa uandikishaji na kwamba yeye aweza kupokea nakala 24 kwa kipindi cha mwaka 1 au nakala 12 kwa kipindi cha miezi sita kwa michango ya kawaida.

3 Vipi ikiwa mwenye nyumba hapendezwi na makala zozote katika toleo la karibuni la Amkeni!? Badala ya kumaliza mazungumzo, huenda ukatumia fursa hiyo kumfundisha mwenye nyumba mengi zaidi juu ya kazi ya Mashahidi wa Yehova kwa kutumia habari katika ukurasa wa 185 wa kitabu Kutoa Sababu.

4 Ikiwa hivi karibuni uliangusha toleo la “Mnara wa Mlinzi” kwa kutumia 2 Timotheo 3:1-5 na kukazia habari kwenye ukurasa wa 2 wa gazeti hilo, huenda ukasema hivi unaporudi:

◼ “Katika mazungumzo yetu ya wakati uliopita, tulizungumzia umaana wa yale yanayotukia kila mahali ulimwenguni leo. Watu wengi huonekana kutopendezwa na viwango vya kuishi vya Mungu kama vinavyoonyeshwa katika Biblia. Hilo limekuwa na uvutano mkubwa juu ya mtazamo wa watu baina yao, kama inavyoelezwa katika andiko kwenye 2 Timotheo 3:1-5. Je! wafikiri kwamba kuna sababu inayofaa kutazamia hali bora zaidi wakati ujao?” Baada ya kuruhusu elezo, huenda ukaelekeza fikira kwenye 2 Petro 3:13. Halafu fungua kurasa 327-33 za kitabu Kutoa Sababu, na ukazie mambo ambayo Ufalme utafanyia ainabinadamu.

5 Kwenye ziara ya kurudia, huenda ukatambua kwamba mwenye nyumba hataki kuzungumzia dini yake, akihisi kwamba hilo ni jambo la kibinafsi sana. Ungeweza kusema jambo kama hili:

◼ “Kukiwa na dini nyingi sana katika ulimwengu unaozidi kuwa mdogo kwa sababu ya usafiri na mawasiliano ya haraka zaidi, matokeo ya imani mbalimbali yanahisiwa ulimwenguni pote, tupende tusipende. Hivyo, kuelewa maoni ya watu kwaweza kuongoza kwenye mazungumzo ya maana zaidi kati ya watu wa imani tofauti. Hilo huenda likaondoa chuki fulani inayotegemea itikadi za kidini. Wewe waonaje?” Baada ya kuruhusu elezo, elekeza fikira za mwenye nyumba kwenye yaliyomo katika kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu.

6 Acheni tutie kila jitihada kurudia wale wote wanaoonyesha kupendezwa katika kweli na kuwasaidia kwenye kijia kiongozacho kwenye uhai wa milele.—Yn. 4:23, 24.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki