Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/93 uku. 8
  • Kitabu Kiandaacho Mwongozo wa Kweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kitabu Kiandaacho Mwongozo wa Kweli
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Weka Msingi Katika Ziara Yako ya Kwanza
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Thamani ya Biblia Katika Ulimwengu wa Leo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Biblia—Kiongozi Ambacho Mungu Amewapa Watu Wote
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Kuwasaidia Wengine Watambue Hazina Iliyo Kuu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1993
km 11/93 uku. 8

Kitabu Kiandaacho Mwongozo wa Kweli

1 Ulimwengu umebadilika kwa njia ya kutazamisha wakati wa karne iliyopita. Ingawa kumekuwa na maendeleo katika nyanja za uwasiliano, tiba, na usafiri, ubora wa maisha ya familia umeshuka hatua kwa hatua. Mamilioni ya watu hujiruhusu waongozwe na falsafa ya wanadamu ibadilikayo daima.

2 Katika mandhari hii ya ulimwengu yenye kubadilika upesi, watu wa Yehova wamenufaika sana kwa kushikamana na Neno lake. Biblia imeendelea bila kubadilika kwa maelfu ya miaka, na bado mashauri yayo ndiyo yafaayo zaidi ili kuwezana na matatizo tunayokabili leo. Twaweza kuwasaidiaje watu waliopendezwa waje kuthamini kwamba Biblia huandaa mwongozo wa kweli kwa ajili ya siku yetu ya kisasa?

3 Ikiwa uliacha trakti “Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani” kwenye mahubiri ya kwanza, huenda ukarudi na kusema:

◼ “Kwa kuwa Biblia husema waziwazi kwamba hiyo ni ujumbe kutoka kwa Mungu mwenyewe na kwamba yeye hututolea uzima wa milele katika ulimwengu mpya wenye amani, je, wahisi kwamba lingekuwa jambo linalofaa kujua zaidi juu ya ahadi hizo? [Ruhusu itikio.] Angalia yale Biblia hutabiri kuhusu ulimwengu mpya unaokuja. [Soma na uzungumzie habari kwenye ukurasa 3 wa trakti hiyo kuanzia kichwa kidogo ‘Maisha Katika Ulimwengu Mpya wa Mungu.’]” Halafu waweza kuweka msingi wa ziara nyingine kwa kuzungumzia ukurasa 5 wa trakti au kwa kutumia ukurasa 161 wa kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, ambao wakazia zaidi lile tumaini zuri ajabu ambalo Biblia hutolea ainabinadamu.

4 Ikiwa kitabu “Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?” kiliangushwa na mwenye nyumba akapendezwa na thamani ifaayo ya Biblia na ulionyesha kanuni hususa katika sura 12, huenda ukasema:

◼ “Twapendezwa na mambo yafaayo kwetu leo, sivyo? Je, ungekubali kwamba kukomesha jeuri na vita ni jambo lifaalo? [Ruhusu itikio.] Ikiwa watu wangejifunza kuishi pamoja katika amani na wale wa mataifa na makundi mengineyo, huo ungekuwa mwanzo mzuri, sivyo? [Ruhusu itikio.] Biblia imetabiri mambo hayo hasa.” [Soma Isaya 2:2, 3.] Waweza kutumia mambo zaidi yanayohusiana nayo kutoka kitabu Kutoa Sababu kwenye kurasa 328-30 kuonyesha mambo yatakayotimizwa na Ufalme wa Mungu. Halafu uulize, “Je! umepata kujiuliza mambo hayo yatatukia lini?” Eleza kwamba ungependa kuzungumzia swali hilo zaidi katika wakati unaomfaa mwenye nyumba.

5 Ikiwa uliacha Biblia “New World Translation,” huenda ukarudi na kusema:

◼ “Katika kusoma Biblia niliyokuachia, huenda ikawa uliona kwamba hiyo yatumia jina la binafsi la Mungu kotekote. Huo ni ubora wa maana kupita tafsiri nyingine nyingi za Biblia. Ingawa watu fulani huenda wakasita kutumia jina Yehova, ni lazima tukumbuke kwamba yeye alifunua jina lake zamani za kale na akawatia moyo watumishi wake kulitumia ili kumtambua yeye kuwa Mungu wa kweli aishiye. Angalia yale ambayo mtunga-zaburi aliandika kwenye Zaburi 83:18.” Soma andiko hilo, na uruhusu mwenye nyumba aseme. Kulingana na kupendezwa kunakoonyeshwa, huenda ukatumia habari zaidi inayopatikana chini ya kichwa “Yehova,” kuanzia ukurasa 420 wa kitabu Kutoa Sababu.

6 Ni Biblia pekee iandaayo mwongozo ambao binadamu ahitaji. (Yer. 10:23) Kujifunza Neno la Mungu ndiyo njia pekee ya kujifunza juu ya makusudi Yake na kupata upendeleo Wake. Kwa hiyo, acheni tuwaalike wengine kwa bidii ili wanufaike na shauri layo lenye hekima na nasaha yenye kufaa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki