Je, Saa Zenu za Mikutano Zitabadilika?
Kuhusu visa ambavyo makutaniko kadhaa yanayotumia Jumba la Ufalme moja yamekubaliana kubadili au kurekebisha saa za mikutano, jambo hili lapaswa kufanywa tarehe moja Januari. Utayari wa kushirikiana na mpango ambao umewekwa waonyesha upendo na ufikirio wa wote. Kwa kawaida badiliko la saa za mikutano litakuwa kwa manufaa yako binafsi, likifanya iwe rahisi zaidi kuhudhuria mikutano.
Kwa upande ule mwingine, badiliko la mwaka huu huenda lisifae ratiba yako ya utendaji. Huenda ikataka marekebisho katika kawaida yako ambayo huenda ikawa yenye kuvuruga. Utayari wa kila mmoja wa kushirikiana waonyesha uthamini kwa mpango wote, ambao ni wa manufaa kwa wote wanaohusika.
Bila shaka, badiliko lifuatalo la saa za mikutano huenda likakupendeza zaidi. Kwa wakati huu, watiwa moyo kufanya marekebisho ya kibinafsi ya lazima ili uweze kuhudhuria mikutano yote ya kila juma kulingana na ratiba ambayo imeamuliwa na kutaniko. Jitahidi kudumisha maoni ya mtunga-zaburi Daudi, aliyetangaza: “Nalifurahi waliponiambia, Na twende nyumbani kwa BWANA.”—Zab. 122:1.