Wimbo 161
Sali kwa Yehova Kila Siku
1. Sali kwa Mungu, anasikia.
Hilo ni pendeleo la sisi.
Tunasema naye kwa uhuru;
Twaweza kumwomba kama Baba.
Tusali kila siku.
2. Sali kwa Mungu na kila siku,
Tumwombe atusamehe dhambi.
Twatafuta musaada wake;
Tusiogope anatulinda.
Tusali kila siku.
3. Sali kwa Mungu kukiwa shida.
Tupumuzishe mioyo yetu,
Atwikwe mahangaiko yetu;
Hiyo ni baraka ametupa.
Tusali kila siku.
4. Sali kwa Mungu; umushukuru.
Musifu na kusema asante.
Sema na Yehova kwa unyofu,
Ndipo tutaona wema wake.
Tusali kila siku.