Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/95 uku. 12
  • Ziara za Kurudia Zenye Kusudi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ziara za Kurudia Zenye Kusudi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Wewe Unahubiri Ukiwa na Kusudi?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Ziara za Kurudia Huongoza Kwenye Mafunzo ya Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Je! Wewe Unafanya Ziara za Kurudia Zako?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Chochea Ukuzi kwa Ziara za Kurudia za Maana
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 10/95 uku. 12

Ziara za Kurudia Zenye Kusudi

1 Unapofanya ziara ya kurudia, unapaswa kujitahidi kutumia andiko ambalo litaongeza ujuzi wa huyo mtu wa habari ya Biblia mliyozungumzia wakati uliopita.

2 Ikiwa uliangusha makala “Ulimwengu Usio na Vita—Lini?” unaweza kusema:

◼ “Maisha katika dunia hii yangekuwaje ikiwa hakungekuwa na vita tena? [Ruhusu itikio.] Acha nikuonyeshe kile ambacho Mungu ameahidi kufanya.” Soma Zaburi 37:10, 11, na ufafanue jinsi mambo yatakavyokuwa wakati mapenzi ya Mungu yatakapofanywa hapa duniani. Mkumbushe huyo mtu juu ya kile Yesu alifundisha wanafunzi kuomba kama ilivyorekodiwa kwenye Mathayo 6:9, 10. Msaidie asababu kuhusu maana ya maneno ya Yesu. Fanya mipango ya kurudi kwa ajili ya mazungumzo zaidi.

3 Ikiwa ulirudi kwa mazungumzo zaidi juu ya makala “Kwa Nini Maisha ni Mafupi Mno” unaweza kuanza hivi:

◼ “Wakati wa mwisho nilipokutembelea, tulizungumzia urefu wa maisha ya binadamu. Kama ulivyoona bila shaka katika makala za Amkeni!, wanasayansi hawatoi tumaini la kutusaidia kuishi zaidi ya miaka 70 au 80. Lakini wafikiri nini kuhusu kile inachoahidi Biblia? [Ruhusu jibu.] Biblia huonyesha kwamba Mungu ana jambo bora zaidi akilini kwa ajili ya mwanadamu.” Kisha soma Yohana 17:3, na ueleze jinsi kutwaa ujuzi kwaweza kuongoza kwenye uhai udumuo milele. Kufikia hapa huenda ukaweza kutoa funzo la Biblia nyumbani au kupanga mazungumzo mengine ya Biblia.

4 Moja ya malengo ya kufanya ziara za kurudia mahali ulipoangusha magazeti ni kuanzisha njia ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaida. Utoaji sahili kama huu waweza kuwa na matokeo:

◼ “Natumaini ulifurahia makala ya Mnara wa Mlinzi niliyokuachia ambayo ilieleza kwa nini twapaswa kumhofu Mungu. Leo nimeleta makala katika gazeti la Amkeni! inayouliza, ‘Kwa Nini Maisha Ni Mafupi Mno?’ Hilo ni swali zuri, sivyo?” Ungeweza kuendelea kwa kusema hivi: “Maneno yajulikanayo sana ya Yesu kwenye Yohana 3:16 hutoa ahadi ya uhai udumuo milele. Tafadhali pokea gazeti hili na utiwe moyo na tumaini hakika linalotolewa katika Neno la Mungu.” Kisha eleza kwamba utarudi ili kuleta matoleo yajayo na labda kuzungumzia zaidi kile ambacho Mungu ameahidi kwa wanadamu watiifu. Kumbuka kwamba kila wakati unapopeleka magazeti unaweza kuripoti ziara ya kurudia.

5 Kuanzisha funzo la Biblia ni lengo muhimu katika huduma yetu. Labda umefanya ziara kadhaa kwa mtu ambaye amekubali magazeti. Kwa nini usijaribu mfikio huu unaporudi wakati ufuatao?:

◼ “Watu wana mawazo mengi tofauti kuhusu dini na thamani yayo katika maisha ya kisasa. Kuna itikadi zenye kupingana kuhusu kwa nini Mungu ameruhusu uovu au kwa nini tunazeeka na kufa. Watu fulani wangependa kujua jinsi ya kusali ili kusikiwa na Mungu.” Fungua moja ya vichapo vyetu vya funzo la Biblia kwa habari ambayo wahisi itampendeza mwenye-nyumba, na uonyeshe kifupi jinsi funzo linavyoongozwa.

6 Yehova ni Mungu wa kusudi. Na tumwige wakati wa Oktoba kwa kufanya ziara za kurudia zenye kusudi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki