Wimbo 159
Mali Yetu Amani
1. Mwenye kukana Mungu,
Hana amani;
Wala wenye akili
zake Shetani.
Kwake Yesu amani,
Hutoka juu,
Ikiwajia watu,
Wenye imani.
2. Sifu Yehova Mungu,
Mwenye amani,
Atakomesha vita,
Kupatanisha.
Yesu Mwana Mufalme
Mwenye amani.
Rafiki ya wapole,
Amani kwao.
3. Tumeacha machungu,
Hatuogopi.
Tumefua mikuki
Na panga kuwa
Majembe na miundu.
Kuwe amani,
Tusamehe kwa pendo,
Kama “kondoo.”
4. Na tuwe na amani,
Ni ya adili,
Hakika ya hekima
Kutoka juu,
Twatafuta kwa sala.
Na njia yetu
Iwe yenye amani,
Ilete shangwe.