Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gm sura 14 kur. 184-189
  • Biblia na Wewe

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Biblia na Wewe
  • Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kubali Msaada
  • Tumia Shauri la Biblia
  • Kubali Mamlaka Yayo
  • Hakuna Aliye Mkamilifu
  • Ishi Kulingana na Neno la Mungu
  • Neno la Mungu Ni Ukweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Lishike kwa Mkazo Neno la Mungu
    Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
  • Kunufaika kwa Usomaji wa Biblia Kila Siku
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Chanzo cha Hali ya Juu Zaidi cha Hekima
    Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
Pata Habari Zaidi
Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
gm sura 14 kur. 184-189

Sura 14

Biblia na Wewe

Wahakiki wa ki-siku-hizi husema kwamba Biblia si ya kisayansi na inajipinga, kwamba hiyo ni mkusanyo wa ngano tu. Kwa upande mwingine, Yesu alisema: “Neno lako ndiyo kweli.” (Yohana 17:17) Uthibitisho waunga mkono Yesu badala ya wahakiki hao. Mambo ya hakika yaonyesha kwamba Biblia ni ya kweli kihistoria. Zaidi ya hayo, upatano wayo wenye kutokeza, unabii mwingi wayo wa kweli, hekima yayo ya kina kirefu, na nguvu zayo za kutokeza wema katika maisha za watu, yote hayo yaonyesha kwamba Biblia ndilo Neno la Mungu lililoandikwa. Ni kama mtume Paulo alivyoandika: “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa.”—2 Timotheo 3:16.

1. (Tia ndani utangulizi.) (a) Mambo ya hakika yathibitisha nini juu ya Biblia? (b) Uhakika wa kwamba Biblia ni Neno la Mungu alilopulizia wamaanisha nini?

UHAKIKA wa kwamba Biblia ni Neno la Mungu, si la binadamu, una maana kubwa sana. Wamaanisha kwamba kwa kweli Mungu amewasiliana na wanadamu. Amejibu mengi ya maswali yetu na ameonyesha utatuzi wa mengi ya matatizo yetu. Pia wamaanisha kwamba mataraja ya wakati ujao yanayoelezwa katika Biblia ni kweli. Ufalme wa Mungu unatawala kweli kweli na baada ya muda utatenda ili kuondoa katika dunia hii ukosefu wote wa haki, uonezi, na kuteseka.

2. Maarifa ya kwamba Biblia ni Neno la Mungu yapasa kutusukuma kufanya nini?

2 Sasa, swali ni hili: Wewe utafanyia nini habari hii? Angalau, maarifa ya kwamba Biblia ni Neno la Mungu yapasa kukutia moyo uichunguze. Mtunga zaburi aliahidi furaha kwa wale wanaofanya hivyo alipoandika: “Mwenye furaha ni mtu ambaye amekuwa hatembei katika shauri la waovu . . . bali kupendezwa kwake ku katika sheria ya Yehova, na katika sheria yake husoma kwa sauti ndogo mchana na usiku.”—Zaburi 1:1, 2, NW.

Kubali Msaada

3, 4. (a) Kama Biblia yenyewe inavyoonyesha, twapaswa kufanya nini tunapokuta mambo katika Biblia ambayo hatuyaelewi? (b) Ni nani ambao sikuzote wana nia ya kuwasaidia watu waielewe Biblia vizuri zaidi?

3 Yaelekea, katika usomaji wako wa Biblia, utakuta mambo ambayo huyaelewi. (2 Petro 3:16) Tukio moja lililoandikwa katika kitabu cha Biblia cha Matendo laonyesha kwamba hilo ni la kutazamiwa. Mara baada ya kifo cha Yesu, Mwethiopia mmoja alikuwa akisoma unabii mwingi wa kitabu cha Biblia cha Isaya. Mwevanjeli Mkristo Filipo alikutana na mwanamume huyo na kumwuliza: “Je! yamekuelea haya unayosoma?” Mwethiopia huyo hakuyaelewa, kwa hiyo akamwalika Filipo amsaidie kuyaelewa.—Matendo 8:30, 31.

4 Mwanamke mmoja katika United States alikuwa katika hali kama hiyo. Yeye alikuwa msomaji wa kawaida wa Biblia, lakini kulikuwako mafundisho mengi ya maana ya Biblia ambayo hakuwa ameyaelewa kwa kujisomea. Wakati tu alipokuwa na mazungumzo pamoja na Mashahidi wa Yehova ndipo alipojifunza kweli za msingi za Biblia, kutia ndani umaana wa Ufalme wa Mungu na baraka nyingi ambazo Ufalme huo utaletea ainabinadamu. Ukiwaalika, Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia pia ili uelewe vizuri zaidi unayosoma katika Biblia.

Tumia Shauri la Biblia

5. Kulingana na Biblia, ni mwendo gani unaoleta furaha?

5 Twatiwa moyo si kusoma Biblia tu bali pia kutenda tunayosoma. (Zaburi 119:2) Kuongezea hilo, Biblia yatia moyo: “Onjeni mwone ya kuwa BWANA [Yehova, NW] yu mwema. Heri mtu yule anayemtumaini.” (Zaburi 34:8) Kwa maneno mengine, inatualika tumtie Mungu kwenye mtihani. Jaribu kuishi kulingana na kanuni za Mungu, ukionyesha unategemea Mungu ili ujue yanayokufaa wewe zaidi. Hapo tu ndipo utakapoona kwamba kweli kweli hiyo ndiyo njia inayofaa. Wale wenye tegemeo hilo katika Mungu ni wenye furaha kweli kweli.

6. Je! ni jambo lenye kutumika kujaribu kuishi kulingana na viwango vya Biblia leo? Fafanua.

6 Wengine hudai kwamba hakuna yeyote anayeweza kuishi kulingana na kanuni za Biblia katika ulimwengu huu usiofuatia haki, usio na adili, wenye jeuri. Hata hivyo, ukweli ni kwamba wengi wameweza hivyo. Nani? Mwanamume mmoja kijana katika Afrika alipata kikundi cha watu kama hao. Aliandika: “Nimekuwa nikichunguza wakati wa miaka michache iliyopita kwamba hapa katika Zimbabwe ni nyinyi watu, Mashahidi wa Yehova, mnaojaribu kweli kweli kufuata kielelezo cha Yesu mwenyewe . . . Nyinyi ndio kikundi pekee, kufikia sasa, ambacho kimeweza kunisadikisha juu ya upendo wa Mungu na nguvu za gospeli Yake, kupitia maisha yenu na si kwa hotuba na maandishi tu. Mnaishi na kuhubiri gospeli ambapo watu wengi sana, wanahubiri gospeli lakini hawaishi kulingana nayo.”

Kubali Mamlaka Yayo

7. Ni mazoea gani ya kawaida yaliyo kinyume cha inayosema Biblia?

7 Mtume Paulo alisema kwamba Biblia inafaa “kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza.” (2 Timotheo 3:16) Hata hivyo, nyakati nyingine mambo ambayo Biblia husema hayapendwi na wengi. Kwa kielelezo, Biblia yalaani vitendo vya ngono ya jinsia moja, lakini ngono ya watu wa jinsia moja inaonwa na wengi kuwa mtindo wa maisha wenye kukubalika. (Warumi 1:24-27; 1 Wakorintho 6:9-11; 1 Timotheo 1:9-11) Pia Biblia yasema kwamba uhai wa mtoto asiyezaliwa ni wa maana na haupaswi kuangamizwa kimakusudi, lakini mimba zinazofikia karibu milioni 50 zinatolewa ulimwenguni pote kila mwaka. (Kutoka 21:22, 23; Zaburi 36:9; 139:14-16; Yeremia 1:5) Vipi ikiwa sisi binafsi twaona vigumu kukubali inayosema Biblia juu ya mambo kama hayo?

8, 9. Mara ya kwanza tunapoona vigumu kukubali jambo fulani katika Biblia, twapaswa kukumbuka nini, na ni viwango vya nani tunavyopaswa kukubali sikuzote?

8 Wakristo wamejifunza kwamba sikuzote ni hekima kufuata Neno la Mungu. Kwa nini? Kwa sababu mwishowe, kufuata inayosema Biblia sikuzote kunatokeza faida kwa kila mtu. (Mithali 2:1-11) Uhakika ni kwamba, wanadamu wamepungukiwa sana kwa habari ya hekima. Ni mara chache wanaweza kutangulia kuona matokeo ya mwisho ya vitendo vyao. Nabii Yeremia aliungama: “Ee BWANA [Yehova, NW], najua ya kuwa njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu.”—Yeremia 10:23.

9 Tunalotakwa kufanya tu ni kuangalia hapa na hapa ili kuona uchanganuzi huo ni sahihi. Mengi ya matatizo yanayoupata ulimwengu ni matokeo ya moja kwa moja ya watu kutofuata shauri la Neno la Mungu. Historia ndefu yenye shida ya ainabinadamu imeonyesha kwamba wanadamu hawawezi kujiamulia mambo ya kiadili wakafanikiwa. Mungu ni mwenye hekima nyingi isiyo na kikomo kuliko sisi. Mbona usikubali anayosema, badala ya kutegemea hekima yako mwenyewe?—Mithali 28:26; Yeremia 17:9.

Hakuna Aliye Mkamilifu

10, 11. (a) Ni mambo gani ya hakika juu ya jinsi tulivyofanyizwa, na pia ulimwengu tunamoishi yanayosababisha matatizo tunapojaribu kuishi kulingana na viwango vya Biblia? (b) Biblia inatutia moyo tutafute ushirika wa aina gani, nasi twaweza kuupata wapi ushirika huo?

10 Biblia yatutahadharishia eneo jingine ambalo twahitaji msaada. Sisi sote tuna mwelekeo wa kufanya dhambi. “Mawazo ya moyo wa mwanadamu ni mabaya tangu ujana wake.” (Mwanzo 8:21; Warumi 7:21) Tatizo hilo linazidishwa na uhakika wa kwamba tunaishi katika ulimwengu usiofuata kanuni za Biblia. Kwa hiyo, twahitaji msaada si wa kuelewa Biblia tu bali pia wa kuzoea mambo tunayojifunza. Ndiyo sababu Biblia hututia moyo tushirikiane na wengine wanaotamani kuishi kulingana na viwango vya kimungu. Mtunga zaburi aliandika: “Nimelichukia kusanyiko la watenda mabaya, wala sitaketi pamoja na watu waovu. . . . Katika makusanyiko nitamhimidi BWANA [Yehova, NW].” Na zaburi nyingine yasema: “Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza, ndugu wakae pamoja, kwa umoja.”—Zaburi 26:5, 12; 133:1.

11 Kushirikiana pamoja ni sehemu ya lazima ya ibada ya Mashahidi wa Yehova. Wana mikutano kadhaa kila juma, na pia makusanyiko ya pindi kwa pindi, ambapo wanajifunza Biblia pamoja na kuzungumza jinsi kanuni zayo zinavyotumika maishani mwao. Wao wanafanyiza “ushirika wa ndugu” ambamo kila mmoja anatiwa moyo na kusaidiwa adumishe viwango hivyo vya juu vya Biblia. (1 Petro 2:17, NW) Mbona usihudhurie mojawapo mikutano yao na kuona jinsi jumuiya hiyo inavyoweza kukusaidia wewe pia?—Waebrania 10:24, 25.

Ishi Kulingana na Neno la Mungu

12. Ni baraka gani zinazotokana na kujua kwamba Biblia ni Neno la Mungu?

12 Kwa hiyo, kujua kwamba Biblia ni Neno la Mungu huleta baraka na madaraka. Tunabarikiwa kwa sababu tunapata mwongozo wa mwenendo wetu wa kila siku usiopatikana kwingine. Kuongezea hayo, twajifunza juu ya upendo wa Mungu katika kumtoa Mwana wake mwenyewe atukomboe ili tuwe na tumaini la uhai wa milele. (Yohana 3:16) Twatambua kwamba Yesu sasa anatawala akiwa Mfalme na karibuni ataondoa uovu kutoka duniani. Nasi twasubiri kwa uhakika “mbingu mpya na dunia mpya” zenye uadilifu ambazo Mungu mwenyewe ameahidi.—2 Petro 3:13, NW.

13. Ni madaraka gani yanayotukalia tunapokubali Biblia kuwa Neno la Mungu?

13 Hata hivyo, kumbuka kwamba tuna daraka la kujifunza Biblia na kutwaa moyoni yale inayosema. Mungu mwenyewe asihi: “Mwanangu, usiisahau sheria yangu, bali moyo wako uzishike amri zangu.” (Mithali 3:1) Hata ikiwa walio wengi huiona Biblia kuwa neno la binadamu tu, kwa moyo mkubwa twapaswa kuacha ‘Mungu aonekane kuwa amini na kila mtu mwongo.’ (Warumi 3:4) Acha hekima ya Mungu iongoze maisha yako. “Mtumaini BWANA [Yehova, NW] kwa moyo wako wote . . . Katika njia zako zote mkiri yeye.” (Mithali 3:5, 6) Kutii kwa hekima Neno la Mungu katika njia hiyo kutaathiri maisha yako kwa wema sasa na kwa umilele wote.

[Blabu katika ukurasa wa 187]

Hatupaswi kusoma tu Biblia bali pia kutenda tunayosoma

[Blabu katika ukurasa wa 188]

Kufuata inayosema Biblia sikuzote hunufaisha sana

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki