Wimbo 131
Kushikamana na Yehova Mungu Wetu
1. Twatumikia Mungu, sisi wa “nyumba” ya Mungu;
tunamwabudu yeye peke yake.
Tumeacha ‘miungu ya mataifa.’
Tumutumikie Yehova pekee.
Atutie moyoni ukweli wake.
2. Mambo ya ahadi, yale aliyosema,
Yanatimia—Uonezi utakoma!
Ufalme wake utakomesha vita.
Twashikamana naye ajulikane.
Yeye ni Mungu; ataleta amani.
3. Tusome Kitabu cha ukweli wa Mungu.
Tunashikamana kabisa na Yehova.
Tujifunze kumupenda, kumwabudu.
Mapenzi na kusudi lake tujue.
Kumwabudu kuwe jambo kuu kwetu.