Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 11/15 kur. 5-7
  • Je! Wewe Unawaheshimu Wafu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Unawaheshimu Wafu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UNAONYESHAJE MAJONZI
  • NAMNA GANI JUU YA MAZISHI?
  • KUNAKUWA NA MATOKEO GANI JUU YA KUNDI LA KIKRISTO?
  • Maoni ya Mkristo Kuhusu Desturi za Mazishi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Mazishi ya Kikristo Ni Yenye Heshima, Kiasi, na Yanampendeza Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Je, Wafu Wapasa Kuheshimiwa?
    Amkeni!—1999
  • Ni Nani Anayestahili Kuombolezewa na Kuzikwa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 11/15 kur. 5-7

Je! Wewe Unawaheshimu Wafu?

UMEKWISHA kupatwa na hasara kubwa inayofuata kifo cha mpendwa? Watu wengi waliofiwa huvurugika kifo kinapomaliza mambo na kutojiweza kunakofuata. Mara nyingi kunakuwa tamaa ya kulipia jambo hilo kupitia kwa vitendo vinavyokusudiwa kuheshimu wafu. Kwa ajili ya imani ya nafsi isiyokufa, sherehe za mazishi mara nyingi hutia ndani sherehe zinazodhaniwa kuwa zinatuliza wafu na kuleta kibali yao, au kuwasaidia katika ulimwengu wa roho.

Ni jambo la asili kuheshimu kumbukumbu la mpendwa. Maono ya moyoni yaliyo kawaida ya binadamu hutaka “mazishi ya heshima” yafanywe. Maono ayo hayo hutokeza tamaa ya kutimiza mapendezi ya mwisho ya mfu, maadamu jambo hilo halikosei dhamiri ya mtu na kutambua kwake yaliyo sawa. Vivyo hivyo, watu wengi hujiepusha na vitendo ambavyo visingekuwa vya kuheshimu wafu.

Hata hivyo, wanaotamani kuongozwa na kanuni za Mungu watahakikisha kwamba mazoea yao hayachochewi na imani ya kwamba wafu wanaona yale yanayofanywa. Sababu gani hivyo? Kwa sababu imani hiyo haina msingi wa kweli, bali wa ushirikina ambao umeenea kutoka Babeli ya kale. Vilevile msingi wake ni hila za mashetani wanaojifanya wafanane na waliokufa.

Ushuhuda unaoonekana unaunga mkono fundisho la Biblia kwamba kifo ndio mwisho wa maisha yote na kwamba mwanadamu hana nafsi isiyokufa inayoweza kuokoka na kuingia katika ulimwengu wa roho. Mwanadamu mwenyewe ndiye nafsi, kwa kuwa twaambiwa hivi katika Maandiko: “[Yehova] Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.” Wanapokufa, wanadamu hurudi mavumbini nayo mawazo yao yanakoma.​—⁠Mwa. 2:7; 3:19; Zab. 146:4; Eze. 18:4, NW.

Bila shaka, kuna imani zinazopingana na hilo. Walakini twawezaje kuishikilia kweli kwa namna tunavyowatendea wafu? Na twawezaje kufanya jambo hilo kwa habari ya kuonyesha majonzi kwa kumpoteza mpendwa?

UNAONYESHAJE MAJONZI

Kuona majonzi kunatuliza mikazo ya maono ya ndani, walakini maono ya ndani hayawezi kukosa kutokeza hali isiyosawazika ya maono ya ndani yakiachiliwa yajionyeshe bila kuzuiwa. Kwa hiyo ni jambo la hekima kuzuia mambo yanayoonyesha majonzi.

Watumishi wa Mungu wa nyakati zilizopita walionyesha huzuni wapendwa walipokufa. (Mwa. 23:2; Kum. 34:8; Yohana 11:33) Hata hivyo walikatazwa kujiingiza katika vitendo vyenye kuonyesha imani ya kwamba wafu waliendelea kuishi katika ulimwengu wa roho. Watu wa Yehova hawakupaswa wachafue dini yao kwa kuiga mataifa katika vitendo vyao vyenye kuonyesha maoni mabaya juu ya wafu.​—Law. 19:28; Kum. 14:1; 18:10-12.

Yesu alilia kwa ajili ya kifo cha Lazaro naye akatabiri kwamba wafuasi wake wangefunga kula kwa sababu ya majonzi baada ya kifo chake mwenyewe. (Yohana 11:35, 38; Marko 2:20) Lakini pia alisema kwamba wangepaswa kufunga kula ili waonekane na Mungu peke yake wala si wanadamu. Wonyesho wao ungekuwa wa kutoka moyoni, si wa kujionyesha nje-nje. (Mt. 6:16-18; linganisha Yoeli 2:12, 13) Yesu aliwaambia wanafunzi wake kwamba hawakuwa sehemu ya ulimwengu. Na, bila shaka, yeye hakutaka kwamba watafute kibali ya ulimwengu kwa kutenda kinyume cha kweli.​—Yohana 15:19.

Yote hayo yanatia moyo Wakristo wasiige desturi ya kuvaa vazi jeusi kuwa wonyesho wa nje-nje wa kuomboleza. Hata hivyo, wakati wa majonzi yanayoletwa na kifo, yaelekea kwamba watu watawa watavaa mavazi ya heshima hadharani, kwa kuwa wakati huo haingependeza kuvalia vivi hivi.​—Mhu. 3:1, 4.

Je! vilevile hiyo inakataza zoea la kesha la usiku? Kama inavyofuatwa na dini mbalimbali, desturi hiyo mara nyingi hufuatana pamoja na nyimbo za kuomboleza na kulia usiku kucha. Jambo hilo linaleta hali ya huzuni na yenye kushusha moyo jamaa iliyofiwa. Kwa wazi kesha la usiku lilitokana na kuogopa waliokufa, nalo zoea hilo lilikusudiwa limtulize aliyekufa na kuzuia pepo waovu. Walakini kwa kuwa Biblia inaonyesha kwamba wafu “hawajui neno lo lote,” msingi wa zoea hilo ni uongo na hivyo haliwezi kupatanishwa pamoja na Ukristo wa kweli.​—Mhu. 9:5, 10.

Hata hivyo, ni jambo linalofaa kutembelea jamaa iliyofiwa. Jambo hilo laweza kufanywa hata ikiwa maiti bado haijaondolewa nyumbani, hata ingawa Mkristo hatashiriki katika kesha la kimila ambalo msingi wake ni maoni na mazoea yasiyokuwa ya kimaandiko. Kwa kawaida, kuketi katika hali yenye huzuni hakuwezi kutoa faraja wala kupunguza majonzi. Wala lisingekuwa jambo la akili kuwekelea watu waliofiwa mzigo wa fedha wa kuwapa wageni chakula kingi. Lingekuwa jambo la huruma kuepuka ziara ndefu, isipokuwa wewe ni mshiriki wa jamaa hiyo au rafiki wa karibu. Lakini lingekuwa jambo lenye kuchangamsha kutoa msaada na ‘kusema kwa kufariji nafsi hizo zilizoshuka moyo.’ (1 The. 5:14, NW) Pengine unaweza kusaidia kwa kutunza nyumba au kununua vitu dukani au kutoa chakula kinachohitajiwa.

Hata hivyo, je! unayaonyesha majonzi yako namna gani unapofiwa? Wakristo hawaombolezi kupita kiasi wala hawawaogopi wafu. Wala hawafikiri kwamba aliyekufa anahitaji msaada kutoka kwa walio hai. Mahali pake, Wakristo wana tumaini kwamba wafu watarudishwa kwenye uzima, kwa kuwa mtume Paulo alisema hivi: “Hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.” (1 The. 4:13) Hivyo, huzuni ya Mkristo huongozwa na kusawazishwa na tumaini.​—Yohana 11:24; Matendo 24:15.

Iwapo umempoteza mpendwa katika mauti, tumaini hilo la ufufuo litakusaidia ushinde maono ya hasara na majonzi. Litakusaidia utumie kwa njia bora zaidi hali zako za sasa nalo litakutia nguvu usaidie wengine. Kwa mfano, unaweza kuwaambia watu wengine waliofiwa juu ya tumaini lako la ufufuo na hivyo uwasaidie wakabiliane na majonzi yao.​—Yohana 5:28, 29.

NAMNA GANI JUU YA MAZISHI?

Katika mazishi ya Kikristo inatakiwa maiti iondolewe katika njia inayotimiza matakwa ya kisheria ya usafi na katika njia inayokubaliwa katika ujamii. Jambo hilo linatoa nafasi ya kufariji waliofiwa na kuwapa wote waliohudhuria ujumbe wa tumaini. Hapana, mazishi ya Kikristo si sakramenti ya kustarehesha nafsi, wala kitendo cha kutuliza “roho iliyoondoka.” Vilevile, Wakristo hawawezi kuwa yawezekana ‘kuwatakasa’ wafu kwa namna mazishi yanavyofanywa. Kwa kuwa wafu “hawajui neno lo lote,” vitendo wanavyofanyiwa haviwezi kuwafaidi wala kuwatuliza, au kuwa na matokeo juu ya uhusiano wao machoni pa Mungu. (Zab. 6:5; 115:17) Hata hivyo mazishi huwafariji watu wa jamaa waliobaki na kuonyesha aliyekufa alivyoheshimiwa.

Hata hivyo, mazishi yenye mambo mengi yangekuwa na thamani gani ikiwa aliyekufa hakuheshimiwa alipokuwa hai? Wengine wamebisha kwamba mazishi yenye mambo mengi na karamu zinazofuatana nayo yanahitajiwa ili kuonyesha heshima na kuonyesha kuthamini alivyoishi maisha mema. Walakini kuthamini huko kungekuwa kwenye thamani zaidi kama kungeonyeshwa wakati wa maisha ya mtu huyo, wakati ambapo angeweza kuona na kufaidika kutokana na jambo hilo.

Ingawa ni jambo la kutoa shukrani kwamba mtu aliyekufa amemaliza maisha mema, kifo ni adui. (1 Kor. 15:26) Ni wakati wa huzuni, si kufurahi, wakati wa kufikiri kwa akili timamu juu ya maana ya kutumia uzima kwa kupatana na mapenzi ya Mungu.​—Mhu. 7:2; 9:10.

Mambo hayo yanaweza kufikiriwa kwa faida wakati wa kuamua kadiri ya kumwonyesha heshima mpendwa aliyekufa. Kwa upande mwingine, kwa kuwa wafu hawana fahamu wala hawawezi kufanya lo lote, sala au matambiko yanayotolewa kwa ajili yao ni kazi bure, vilevile ni kosa.​—Isa. 8:19; 38:18.

KUNAKUWA NA MATOKEO GANI JUU YA KUNDI LA KIKRISTO?

Ikiwa mtu aliyekufa alikuwa anashirikiana na kundi la Kikristo, lingekuwa jambo la kawaida kwa kundi hilo kuulizwa liongoze mazishi. Kwa kweli, mtu huyo aliyekufa huenda akawa alitaka iwe hivyo, na ingefaa kwa watoto walioachwa au washiriki wengine wa jamaa waheshimu jambo hilo. Bila shaka, jukumu (daraka) la jamaa linatia ndani kufanya mipango ya mazishi. Hata hivyo, inaposhughulika na gharama, na mambo ya kisheria na mambo ya kawaida yanayopaswa kufanywa, jamaa hiyo inaweza kuliuliza kundi, kupitia kwa wazee, liongoze mazishi.​—1 Tim. 5:8.

Hata hivyo, uhitaji wa kweli ukiwapo, kundi linaweza kuchukua madaraka fulani ya mazishi ya Mkristo mwaminifu anayekufa akiwa fukara (bila kitu) na bila watu wa jamaa wanaoweza kuyaangalia mambo hayo. (Linganisha 1 Timotheo 5:​9, 10) Hilo ni jambo la kuamuliwa na baraza ya wazee ya mahali hapo. Kwa kawaida, washiriki wa jamaa wasioamini wakiendesha mipango ya mazishi, kundi la Kikristo halipaswi kupanga namna fulani ya mazishi ya kushirikiana na watu wengine hivyo wajihatirishe kwa kuchangamana na watu wa dini nyingine.​—2 Kor. 6:14-17; Ufu. 18:4.

Katika mambo yote yanayohusu kuhudumia wafu, ni jambo la lazima kujipatanisha na yaliyo kweli. Hivyo, Wakristo huepuka jambo lo lote ambalo hata kidogo tu linaelekea kufanana na ibada ya mababu au kuwa na imani na “roho zilizoondoka.” Watu watawa huamini mpango wa ufufuo na azimio la kumsifu Yehova kupitia kwa kushiriki ibada isiyochafuliwa na namna yo yote ya uongo.​—Yohana 4:23, 24; Yak. 1:27.

[Picha katika ukurasa wa 5]

Je! unaijaza kwa huzuni nyumba ambayo kuna maombolezo au

Je! unawatia moyo wanaoomboleza kwa kuwapa tumaini ambalo msingi wake ni Neno la Mungu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki