Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/98 uku. 7
  • Kutoa Ushahidi kwa Mwenendo Mzuri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutoa Ushahidi kwa Mwenendo Mzuri
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari Zinazolingana
  • “Kutoka Kinywani mwa Watoto Wachanga”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Matendo Mema Yamtukuzayo Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Tunawafurahia Vijana Wanaotembea Katika Njia ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Vijana Wanaoangaza Kama Mianga
    Huduma ya Ufalme—2006
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 6/98 uku. 7

Kutoa Ushahidi kwa Mwenendo Mzuri

1 Katika jamii ya leo yenye uendekevu, vijana wengi hufuja maisha yao kwa dawa za kulevya, ukosefu wa adili, uasi, na jeuri. Kinyume na hayo, mwenendo bora wa vijana wafaao katika kutaniko la Kikristo ni wenye kuburudisha na kwa hakika ni jambo lenye kupendeza kwa Yehova. Huo hutoa ushahidi wenye nguvu ambao huenda ukawavuta wengine waje kwenye kweli.—1 Pet. 2:12.

2 Mambo mengi yaliyoonwa yaonyesha kwamba mwenendo mzuri wa vijana Wakristo umekuwa na matokeo mazuri kwa watazamaji. Mwalimu mmoja, akiongea kuhusu Shahidi mchanga ambaye alikuwa mwanafunzi wake, aliambia darasa lote kwamba Mungu wa msichana huyu, Yehova, ndiye Mungu wa kweli. Alisema hivyo kwa sababu mwenendo wa msichana huyo sikuzote ulikuwa wenye staha. Mwalimu mwingine aliandikia Sosaiti, akisema hivi: “Mimi ningependa kuwasifu kwa sababu ya kuwa na vijana wazuri sana mlio nao katika dini yenu. . . . Vijana wenu ni mfano kweli kweli. Wao wanaheshimu wazee wao, ni waungwana na wanavaa kwa kiasi. Nao wanazijua Biblia zao wee! Hiyo ni dini kweli kweli!”

3 Mwalimu mwingine wa shule alipendezwa na mwenendo mzuri wa Shahidi mwenye umri wa miaka saba katika darasa lake. Alivutiwa na utu wa mvulana huyo ulio mpole na wenye kupendeza, ambao ulimfanya awe tofauti kabisa na vijana wengine. Alipendezwa sana na mtazamo wake wenye kuchukulia mambo kwa uzito kuelekea itikadi zake—hakuaibika kuwa tofauti kwa sababu ya yale aliyoamini. Angeweza kuona kwamba dhamiri ya mvulana huyo ilikuwa imezoezwa na kwamba aliweza “kutofautisha lililo sahihi na lililo kosa pia.” (Ebr. 5:14) Hatimaye, mama ya mvulana huyo alimtembelea mwalimu huyo, na funzo la Biblia likaanzishwa. Baada ya muda, mwalimu huyo alibatizwa na baadaye akawa painia wa kawaida!

4 Mwanamume mmoja asiye na umri mkubwa alivutiwa na mwenendo mzuri wa Shahidi mmoja katika shule yake. Yeye alikuwa tofauti kikweli—mpole sana, mwenye bidii ya mafunzo, na mwenye mavazi ya kiasi sikuzote; pia, tofauti na wasichana wale wengine, hakuchezacheza na wavulana kamwe. Angeweza kuona kwamba alikuwa akiishi kupatana na kanuni za Biblia. Mwanamume huyo asiye na umri mkubwa alimwuliza maswali juu ya itikadi zake naye alipendezwa na yale aliyojua. Alianza kujifunza, naye akabatizwa upesi, na hatimaye alishiriki katika huduma ya painia na utumishi wa Betheli.

5 Ikiwa wewe ni kijana Mkristo ambaye hutamani kutoa ushahidi mzuri kwa wengine, angalia sana mwenendo wako katika kila njia. Usijishushe kamwe kwa kupendelea mitazamo yenye uendekevu, maoni, au mitindo-maisha ya ulimwengu. Weka kielelezo cha hali ya juu katika usemi, mavazi, na kujipamba kwako, si tu unaposhiriki katika huduma ya shambani na kwenye mikutano ya kutaniko bali pia unapokuwa shuleni na unapokuwa katika tafrija. (1 Tim. 4:12) Utakuwa na shangwe kwelikweli mtu fulani apendezwapo na kweli kwa sababu umekuwa ‘ukiacha nuru yako ing’ae’ kupitia mwenendo wako.—Mt. 5:16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki