Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jv sura 33 kur. 713-717
  • Kuendelea Kufuliza Kulinda

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuendelea Kufuliza Kulinda
  • Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Kuwa na Uhakikisho Kamili’ juu ya Uelewevu Wao
  • Kufuliza Kulinda—Jinsi Gani?
  • “Ingojee”
  • Endeleeni Kuwa Tayari!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Endelea Kutarajia!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Sehemu ya 5—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Sehemu ya 4—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
jv sura 33 kur. 713-717

Sura ya 33

Kuendelea Kufuliza Kulinda

“KWA kuwa Yesu alisema waziwazi kwamba hakuna mtu anayejua ‘siku ile’ wala ‘saa ile’ wakati Baba atakapoamuru mwanaye ‘aje’ dhidi ya mfumo mbovu wa mambo wa Shetani, huenda wengine wakauliza hivi: ‘Sababu gani ni jambo lenye kutaka hatua ya haraka kuishi ukitazamia mwisho?’ Ni kwa sababu Yesu alitumia mkazo uo huo akaongeza hivi: ‘Endeleeni kuangalia, endeleeni kukesha . . . endeleeeni kulinda.’ (Marko 13:32-35, NW)”—Mnara wa Mlinzi, Mei 1, 1985.

Mashahidi wa Yehova wamekuwa wakilinda kwa miongo sasa. Wakilinda kwa ajili ya nini? Kwa ajili ya kuja kwa Yesu katika uwezo wa Ufalme ili kutekeleza hukumu dhidi ya mfumo mwovu wa mambo wa Shetani na kueneza manufaa kamili ya utawala wake wa Ufalme duniani pote! (Mt. 6:9, 10; 24:30; Luka 21:28; 2 The. 1:7-10) Hao wanaolinda wanajua kwamba “ishara” ya kuwapo kwa Yesu imedhihirika tangu 1914 na kwamba mfumo wa mambo wa sasa uliingia kwenye siku zayo za mwisho katika mwaka huo.—Mt. 24:3–25:46, NW.

Lakini, Yesu hajaja bado akiwa Mtekelezaji-Kifo na Mkombozi. Kwa hiyo Mashahidi wa Yehova huionaje hali yao ya sasa?

‘Kuwa na Uhakikisho Kamili’ juu ya Uelewevu Wao

Wakiwa kutaniko la ulimwenguni pote, wao wana “uhakikisho kamili wa uelewevu wao.” (Kol. 2:2, NW) Si kwamba wao huhisi wanaelewa kila jambo la makusudi ya Yehova. Wao huendelea kutafuta Maandiko kwa akili iliyofunguka, na wao huendelea kujifunza. Lakini yale wanayojifunza hayabadili maoni yao ya msingi kuhusu kweli za msingi za Neno la Mungu. Wao wana “uhakikisho kamili” juu ya kweli hizo za msingi; wamezitambua na kuzikubali kwa miongo mingi sasa. Hata hivyo, yale wanayojifunza, hufanya uelewevu wao uzidi kukua juu ya jinsi maandiko fulani hufaana na kiolezo kizima cha kweli ya Biblia na jinsi wanavyoweza kutumia kikamili shauri la Neno la Mungu katika maisha zao wenyewe.

Mashahidi wa Yehova wana “uhakikisho kamili” pia kuhusu ahadi za Mungu. Wao wana tumaini hakika kwamba hakuna ahadi yake itakayokosa kutimizwa hata katika jambo dogo zaidi na kwamba zote zitatimizwa katika wakati wake uliowekwa. Hivyo, utimizo wa unabii wa Biblia ambao wameona na kupata pia, huwaacha wakiwa na uhakika kamili kwamba ulimwengu wa sasa umo katika “wakati [wake] wa mwisho” na kwamba ahadi ya Mungu ya ulimwengu mpya wenye uadilifu itatimizwa karibuni.—Dan. 12:4, 9; Ufu. 21:1-5.

Kwa hiyo, basi, wao wapaswa kuwa wakifanya nini? “Fulizeni kutazama, fulizeni kuwa macho,” akaamuru Yesu, “kwa maana hamjui ni lini ulio wakati uliowekwa. Kwa hiyo fulizeni kulinda . . . ili [Bwana-Mkubwa] awasilipo kwa ghafula, asiwakute nyinyi mkiwa mmelala usingizi. Lakini lile niwaambialo nyinyi nawaambia wote, Fulizeni kulinda.” (Mk. 13:33, 35-37, NW) Mashahidi wa Yehova wanajua vema uhitaji wa kufuliza kulinda.

Hamu ya kupita kiasi ambayo nyakati nyingine wamedhihirisha kuhusu kutimizwa kwa unabii mbalimbali haibadilishi ithibati inayorundamana tangu Vita ya Ulimwengu 1 kwamba sisi tumo kwenye umalizio wa mfumo wa mambo. Kwa hakika, ni afadhali sana kuwa wenye bidii—hata kuwa wenye bidii kupita kiasi—ili kuona mapenzi ya Mungu yakitimizwa kuliko kuwa wenye kulala usingizi kiroho kuhusu kutimizwa kwa makusudi yake!—Linganisha Luka 19:11; Matendo 1:6; 1 Wathesalonike 5:1, 2, 6.

Kufuliza kulinda kwatia nini ndani?

Kufuliza Kulinda—Jinsi Gani?

Wakristo wenye kulinda hawaketi kitako tu na kungoja. Ni kinyume cha hilo! Ni lazima waendelee kuwa katika hali njema kiroho ili kwamba wakati Yesu anapokuja akiwa Mtekelezaji-Kifo, yeye atathibitika kuwa Mkombozi wao pia. (Luka 21:28) “Kazieni uangalifu kwa nyinyi wenyewe,” Yesu akaonya, “mioyo yenu isiwe kamwe yenye kulemewa na kula kupita kiasi na kunywa sana na mahangaiko ya maisha, na kwa ghafula siku hiyo iwe juu yenu mara hiyo kama mtego. . . . Fulizeni kuwa macho.” (Luka 21:34-36, NW) Kwa hiyo, Wakristo wenye kulinda ni lazima kwanza ‘wakazie uangalifu kwao wenyewe,’ wakiwa waangalifu kuishi kulingana na jinsi ambavyo Mkristo apaswa kuishi kila siku. Ni lazima wakae macho kuhusu madaraka ya Kikristo na kuepuka mwenendo usio wa Kikristo ulio tabia ya ulimwengu ‘unaokaa katika nguvu ya mwovu.’ (1 Yoh. 5:19; Rum. 13:11-14, NW) Ni lazima wawe tayari, Kristo anapokuja.

Ni nani ambao kwa kweli wamefuliza kukaa macho kabisa, katika hali njema ya kiroho? Rekodi ya kihistoria iliyotolewa katika sura zilizotangulia za kichapo hiki yaelekeza kwa Mashahidi wa Yehova. Kwa wazi, wao huchukua kwa uzito madaraka yanayotiwa ndani katika kuwa Wakristo. Katika wakati wa vita, kwa kielelezo, wamekuwa tayari kujasiria kufungwa na kufa kwa sababu ya kuwa macho kabisa kuhusu takwa la kutokuwa sehemu ya ulimwengu na kuonyesha upendo wa kujidhabihu kwa mmoja na mwenzake. (Yn. 13:34, 35; 17:14, 16) Watu wanaowatazama kwenye Majumba ya Ufalme yao, kwenye mikusanyiko yao mikubwa, au hata kwenye kazi zao za kimwili huvutiwa na ‘mwenendo wao mwema.’ (1 Pet. 2:12) Katika ulimwengu huu ambao ‘umekufa ganzi kiadili,’ wao wana sifa ya kuongoza maisha manyoofu, yaliyo safi kiadili.—Efe. 4:19-24; 5:3-5.

Hata hivyo, kufuliza kulinda hutia ndani mengi zaidi ya ‘kukazia uangalifu kwako mwenyewe.’ Ni lazima mlinzi atangazie wengine yale anayoona. Katika wakati huu wa mwisho, Wakristo wenye kulinda wanaoona waziwazi ishara ya kuwapo kwa Kristo ni lazima wapige mbiu kwa wengine juu ya “habari njema hii ya ufalme” na lazima wawaonye kwamba karibuni Kristo atakuja na kutekeleza hukumu dhidi ya mfumo huu mwovu wa mambo. (Mt. 24:14, 30, 44) Kwa njia hiyo wao husaidia wengine wajiweke katika mstari wa kuja ‘kukombolewa.’—Luka 21:28.

Ni nani ambao wamethibitika kuwa wakilinda kwa kutoa onyo? Mashahidi wa Yehova wanajulikana ulimwenguni pote kwa ajili ya bidii yao katika kupiga mbiu ya jina na Ufalme wa Mungu. Wao hawaachi mahubiri yawe ya jamii teule ya makasisi. Wanatambua kwamba ni daraka la waamini wote. Wanayatambua kuwa sehemu ya maana ya ibada yao. (Rum. 10:9, 10; 1 Kor. 9:16) Matokeo yamekuwa nini?

Wao sasa hufanyiza kutaniko linalokua la mamilioni ya washiriki watendaji katika nchi zaidi ya 220 kotekote duniani. (Isa. 60:22; linganisha Matendo 2:47; 6:7; 16:5.) Baadhi ya serikali zenye uwezo sana katika historia ya wanadamu zimepiga marufuku kazi yao, hata zikawasaka na kuwatia gerezani. Lakini Mashahidi wa Yehova wameendelea kupiga mbiu ya Ufalme wa Mungu! Azimio lao ni kama lile la mitume, ambao walipoagizwa waache kuhubiri, wao walijulisha hivi: “Sisi hatuwezi kukoma kusema juu ya mambo ambayo tumeyaona na kuyasikia.” “Lazima sisi tumtii Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu.”—Mdo. 4:18-20; 5:27-29, NW.

“Ingojee”

Hali ya Mashahidi wa Yehova leo ni kama ile ya Wakristo Wayudea wa karne ya kwanza. Yesu alikuwa amewapa ishara ambayo wangejua wakati wa kukimbia kutoka Yerusalemu ili watoroke uharibifu wayo. ‘Mwonapo Yerusalemu limezingirwa na majeshi, anzeni kukimbia,’ Yesu akasema. (Luka 21:20-23, NW) Muda unaozidi kidogo miaka 30 baadaye, katika 66 W.K., Yerusalemu ulizungukwa na majeshi ya Waroma. Wakati majeshi ya Waroma yalipoondoka ghafula bila sababu yoyote ya wazi, Wakristo Wayudea walifuata maagizo ya Yesu na kukimbia—si kutoka Yerusalemu tu bali kutoka nchi yote ya Yudea—kwenda kwenye jiji moja katika Perea liitwalo Pella.

Wakiwa huko, katika usalama, wakangoja. Mwaka 67 W.K. ukaanza na ukakwisha. Kisha 68 ukafuatwa na 69. Na bado, Yerusalemu ulibaki huru. Je, walipaswa kurudi? Kwa vyovyote vile, Yesu hakuwa amewaambia wangengoja muda gani. Lakini ikiwa Wakristo wowote walirudi, lilikuwa jambo la kusikitisha, kwa sababu katika 70 W.K., majeshi ya Waroma yalikuja tena katika idadi zilizofanya waonekane kana kwamba ni gharika ambayo haingeweza kusimamishwa, na wakati huu wao hawakuondoka. Badala yake, walibomoa jiji hilo na kuua watu zaidi ya milioni moja. Ni lazima iwe wale Wakristo Wayudea waliokuwa Pella walifurahi jinsi gani kwamba walikuwa wameendelea kungoja wakati wa Yehova uliowekwa rasmi ili kutekeleza hukumu!

Ni hali moja na wale wanaofuliza kulinda leo. Wanajua kikamili kwamba kadiri tuendeleavyo kusonga ndani katika wakati huu wa mwisho, ndivyo itakavyokuwa vigumu zaidi kuendelea kutazamia kuja kwa Yesu. Lakini wao hawajapoteza imani katika maneno ya Yesu: “Kweli nawaambia nyinyi kwamba kizazi hiki hakitapitilia mbali kwa vyovyote mpaka mambo yote haya yatukie.” (Mt. 24:34, NW) Maneno ‘mambo haya’ hurejezea mambo mbalimbali ya “ishara” yenye kutia ndani mambo mengi. Ishara hiyo imekuwa dhahiri tangu 1914 na itafikia upeo kwenye “dhiki kubwa.” (Mt. 24:21, NW) Mwisho hauwezi kuwa mbali sana.

Wakati uo huo, Mashahidi wa Yehova wanaazimia kabisa kufuliza kulinda, wakiwa na imani kamili kwamba Mungu atatekeleza ahadi zake zote kwa wakati wake! Wanathamini kwa moyo maneno ya Yehova kwa nabii Habakuki. Kuhusu kule kulikoonekana kuwa kama kuvumilia kwa Yehova uovu katika ufalme wa Yuda wakati wa sehemu ya mwisho ya karne ya saba K.W.K., Yehova alimwambia nabii huyo hivi: “Iandike njozi [kuhusu mwisho wa hali zenye uonevu] ukaifanye iwe wazi sana katika vibao, ili aisomaye apate kuisoma kama maji. Maana njozi hii bado ni kwa wakati ulioamriwa, inafanya haraka ili kuufikilia mwisho wake, wala haitasema uongo; [ijapoonekana kana kwamba inakawia], ingojee; kwa kuwa haina budi kuja, haitakawia.” (Hab. 1:2, 3; 2:2, 3) Vivyo hivyo, Mashahidi wa Yehova wana tumaini hakika katika uadilifu na haki ya Yehova, na hilo huwasaidia kuendelea kuwa na usawaziko na kungojea “wakati ulioamriwa” wa Yehova.

F. W. Franz, aliyebatizwa katika 1913, alieleza vizuri hisi za Mashahidi wa Yehova. Katika 1991, akiwa msimamizi wa Watch Tower Society, yeye alisema:

“Tumaini letu ni jambo la hakika, na litatimizwa kikamili kwa kila mmoja wa wale washiriki 144,000 wa kundi dogo kwa kadiri inayopita hata yale ambayo tumeweza kuwazia. Sisi wa mabaki waliokuwako katika mwaka wa 1914, wakati tulipotazamia kwamba sisi sote tungeenda mbinguni, hatujapoteza maoni yetu ya thamani ya tumaini hilo. Bali tungali wenye imara kwalo jinsi tulivyokuwa wakati wowote ule, na tunalithamini hata zaidi tunapozidi kulingojea. Ni jambo linalostahili kungojewa, hata ikiwa lingehitaji miaka milioni moja. Ninakadiri tumaini letu kuwa lenye thamani kubwa zaidi ya wakati mwingine wowote, nami sitaki kamwe kupoteza uthamini wangu kwalo. Tumaini la kundi dogo hutoa uhakikishio pia kwamba tazamio la umati mkubwa wa kondoo wengine litatimizwa kuupita upeo wa uwazio wetu ulio mwangavu zaidi, bila uwezekano wowote wa kutofaulu. Hiyo ndiyo sababu tunavumilia kwa imara hadi saa hii, nasi tutavumilia hadi wakati Mungu atakapoonyesha kwa hakika kwamba yeye ni mwaminifu kwa ‘ahadi zenye bei na zilizo bora sana.’”—2 Pet. 1:4; Hes. 23:19; Rum. 5:5.

Wakati unakaribia upesi ambapo kuwapo kwa Kristo katika uwezo wa Ufalme kutadhihirishwa waziwazi kwa wanadamu wote. Kisha, wale wanaolinda ‘watapokea utimizo wa ahadi.’ (Ebr. 10:36, NW) Kwelikweli, matazamio yao yatatimizwa kuupita upeo wa ‘yale waliyopata kuwazia wakati wowote.’ Jinsi watakavyokuwa wenye furaha na wenye shukrani kwamba katika siku za kumalizia za mfumo mwovu wa mambo, wao ndio walioendelea kufuliza kulinda, na waliopiga mbiu ya Ufalme wa Mungu kwa bidii!

[Blabu katika ukurasa wa 713]

Uhakika kamili kwamba ulimwengu wa sasa umo katika “wakati [wao] wa mwisho”

[Blabu katika ukurasa wa 714]

Wakiwa waangalifu kuishi kulingana na jinsi ambavyo Mkristo apaswa kuishi kila siku

[Blabu katika ukurasa wa 715]

Ni nani ambao wamethibitika kuwa wakilinda kwa kutoa onyo?

[Blabu katika ukurasa wa 716]

“Ninakadiri tumaini letu kuwa lenye thamani kubwa zaidi ya wakati mwingine wowote, nami sitaki kamwe kupoteza uthamini wangu kwalo” —F. W. Franz

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 717]

Ripoti juu ya Kutolewa kwa Ushahidi Duniani Pote

Mwaka Nchi

1920 ....... 46

1925 ....... 83

1930 ....... 87

1935 ...... 115

1940 ...... 112

1945 ...... 107

1950 ...... 147

1955 ...... 164

1960 ...... 187

1965 ...... 201

1970 ...... 208

1975 ...... 212

1980 ...... 217

1985 ...... 222

1992 ...... 229

Jumla ya Nchi

Hesabu ya nchi imewekwa kulingana na jinsi dunia ilivyokuwa imegawanywa katika miaka ya mapema ya 1990, si kulingana na mipaka ya kisiasa iliyokuwako, kwa kielelezo, wakati zile zilizokuwa milki kubwa zilipotawala eneo ambalo sasa limegawanywa miongoni mwa mataifa kadhaa yaliyo huru.

Mwaka Makut.

1940 ...... 5,130

1945 ...... 7,218

1950 ..... 13,238

1955 ..... 16,044

1960 ..... 21,008

1965 ..... 24,158

1970 ..... 26,524

1975 ..... 38,256

1980 ..... 43,181

1985 ..... 49,716

1992 ..... 69,558

Jumla ya Makutaniko

Kabla ya 1938 hakukuwako rekodi iliyowekwa ya kimataifa yenye kupatana ya jumla ya hesabu ya makutaniko.

Mwaka Wah.

1935 .. ... 56,153

1940 ...... 96,418

1945 ..... 156,299

1950 ..... 373,430

1955 ..... 642,929

1960 ..... 916,332

1965 ... 1,109,806

1970 ... 1,483,430

1975 ... 2,179,256

1980 ... 2,272,278

1985 ... 3,024,131

1992 ... 4,472,787

Jumla ya Wahubiri wa Ufalme

Njia ya kuhesabu wahubiri ilipata mabadiliko kadhaa wakati wa miaka ya 1920 na mapema miaka ya 1930. Ripoti za kutaniko zilipelekwa kwa Sosaiti kila juma, badala ya kila mwezi. (Ripoti za kila mwezi hazikuanza kupelekwa hadi Oktoba 1932.) Kulingana na “Bulletin” la Januari 1, 1929, ili mtu ahesabiwe kuwa mfanyakazi wa darasa (mhubiri wa kutaniko), yeye aliwajibika kutumia angalau muda wa saa 3 kila juma (au 12 kila mwezi) katika utumishi wa shambani. Walenga-shabaha (wahubiri walio mbali) walipaswa kutumia angalau muda wa saa mbili kila juma katika kutoa ushahidi.

Mwaka Mapainia

1920 ......... 480

1925 ....... 1,435

1930 ....... 2,897

1935 ....... 4,655

1940 ....... 5,251

1945 ....... 6,721

1950 ...... 14,093

1955 ...... 17,011

1960 ...... 30,584

1965 ...... 47,853

1970 ...... 88,871

1975 ..... 130,225

1980 ..... 137,861

1985 ..... 322,821

1992 ..... 605,610

Mapainia

Tarakimu zilizoorodheshwa hapa zatia ndani mapainia wa kawaida, mapainia wasaidizi, mapainia wa pekee, wamishonari, waangalizi wa mzunguko, na waangalizi wa wilaya. Hapo awali mapainia waliitwa makolpota, na mapainia wasaidizi waliitwa makolpota wasaidizi. Tarakimu za miaka mingi zinawakilisha wastani wa kila mwezi.

Mwaka Maf. Bib.

1945 ....... 104,814

1950 ....... 234,952

1955 ....... 337,456

1960 ....... 646,108

1965 ....... 770,595

1970 ..... 1,146,378

1975 ..... 1,411,256

1980 ..... 1,371,584

1985 ..... 2,379,146

1992 ..... 4,278,127

Mafunzo ya Biblia Nyumbani

Wakati wa miaka ya 1930, baadhi ya mafunzo yaliongozwa pamoja na watu mmoja-mmoja, lakini mkazo ulikuwa juu ya kufundisha watu jinsi ya kuyaongoza wenyewe na pia juu ya kupanga vikundi vya mafunzo ambavyo vingeweza kuhudhuriwa na watu wengine wenye kupendezwa katika eneo hilo. Baadaye, watu mmoja-mmoja walipoonyesha kupendezwa kikweli, mafunzo yaliongozwa pamoja nao hadi walipobatizwa. Baadaye, kitia-moyo kilitolewa ili kuendelea na funzo hadi mtu awe amepewa msaada wa kutosha kuweza kuwa Mkristo mkomavu.

Mwaka Saa

1930-35 ....... 42,205,307

1936-40 ....... 63,026,188

1941-45 ...... 149,043,097

1946-50 ...... 240,385,017

1951-55 ...... 370,550,156

1956-60 ...... 555,859,540

1961-65 ...... 760,049,417

1966-70 .... 1,070,677,035

1971-75 .... 1,637,744,774

1976-80 .... 1,646,356,541

1981-85 .... 2,276,287,442

1986-92 .... 5,912,814,412

Jumla ya Saa

Kwa ujumla, wakati haukuripotiwa hadi miaka ya mwishoni ya 1920. Njia ya kuhesabu muda wa saa ilipata mabadiliko fulanifulani: Katika miaka ya mapema ya 1930, wakati uliotumiwa katika kutoa ushahidi nyumba hadi nyumba ndio tu uliohesabiwa—sio ule uliotumiwa kwenye ziara za kurudia. Ingawa ripoti iliyoonyeshwa hapa ni yenye kuvutia kwelikweli, hiyo kwa kweli ni kadirio tu la muda mwingi uliotumiwa na Mashahidi wa Yehova katika kazi ya kupiga mbiu ya Ufalme wa Mungu.

Mwaka Fas. Zilizogaw.

1920-25 ....... 38,757,639

1926-30 ....... 64,878,399

1931-35 ...... 144,073,004

1936-40 ...... 164,788,909

1941-45 ...... 178,265,670

1946-50 ...... 160,027,404

1951-55 ...... 237,151,701

1956-60 ...... 493,202,895

1961-65 ...... 681,903,850

1966-70 ...... 935,106,627

1971-75 .... 1,407,578,681

1976-80 .... 1,380,850,717

1981-85 .... 1,504,980,839

1986-92 .... 2,715,998,934

Fasihi Zilizogawanywa

Isipokuwa katika pindi chache, tarakimu za miaka ya kabla ya 1940 hazitii ndani magazeti yaliyoangushwa, ingawa mamilioni ya nakala ziligawanywa. Tarakimu tangu 1940 zinatia ndani vitabu, vijitabu, broshua, na magazeti, lakini si mamia ya mamilioni ya trakti ambazo zimetumiwa pia ili kuchochea kupendezwa na ujumbe wa Ufalme. Jumla ya fasihi 10,107,565,269 zilizogawanywa kuanzia 1920 hadi 1992 katika lugha zaidi ya 290 hutoa ithibati ya kutolewa ushahidi duniani pote kunakostaajabisha.

Mwaka Hudhu. Washi.

1935 ...... 63,146 ... 52,465

1940 ...... 96,989 ... 27,711

1945 ..... 186,247 ... 22,328

1950 ..... 511,203 ... 22,723

1955 ..... 878,303 ... 16,815

1960 ... 1,519,821 ... 13,911

1965 ... 1,933,089 ... 11,550

1970 ... 3,226,168 ... 10,526

1975 ... 4,925,643 ... 10,550

1980 ... 5,726,656 .... 9,564

1985 ... 7,792,109 .... 9,051

1992 .. 11,431,171 .... 8,683

Hudhurio la Ukumbusho na Washiriki

Tarakimu zinazopatikana za hudhurio la Ukumbusho kabla ya 1932, huwa mara nyingi hazijakamilika. Nyakati nyingine, ni vikundi vya watu 15, 20, 30, au zaidi vilivyokuwa vikitiwa ndani katika jumla zilizotangazwa. Kwa kupendeza, miaka mingi ambayo tarakimu zozote zapatikana yaonyesha kwamba angalau baadhi ya wahudhuriaji hawakuwa washiriki. Kufikia 1933 tofauti ilikuwa 3,000 hivi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki