Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/00 uku. 1
  • “Hatuwezi Kukoma Kusema”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Hatuwezi Kukoma Kusema”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Kunena Neno la Yehova Kwa Ujasiri
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Endelea Kuhubiri Neno la Mungu kwa Ujasiri
    Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
  • ‘Sema Neno la Mungu kwa Ujasiri’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Julisha Rasmi Habari Njema kwa Ujasiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 7/00 uku. 1

“Hatuwezi Kukoma Kusema”

1 Yesu Kristo anasimamia kwa ukaribu kazi ya kuhubiri. (Mt. 28:20; Mr. 13:10) Ijapokuwa kuna watangazaji karibu milioni sita wanaotoa ushahidi katika nchi 234, tusidhani kwamba kazi yetu ya kutoa ushahidi imekwisha. Mungu asipotangaza kwamba kazi imekwisha, “hatuwezi kukoma kusema” juu ya mambo ambayo tumejifunza.—Mdo. 4:20.

2 Tegemea Roho ya Mungu: Shetani huongeza mkazo mwingi ili kutuvunja moyo. (Ufu. 12:17) Mwili wetu wenyewe usio mkamilifu pia hutuletea shida nyingi. Mambo hayo yanaweza kukengeusha fikira zetu kutoka katika kazi ya maana zaidi ya kuhubiri. Hata hivyo, tukimtumaini Yehova, roho yake itatusaidia tukabiliane na kizuizi chochote.

3 Kutaniko la Kikristo la karne ya kwanza liliponyanyaswa vibaya, akina ndugu walimwomba Mungu awasaidie waendelee kusema neno lake kwa ujasiri wote. Yehova alijibu sala yao, akiwajaza roho yake na kuwapa bidii na azimio lililohitajiwa ili kuendelea kuhubiri. Tokeo likawa kwamba waliendelea bila kuacha kutangaza kwa ujasiri habari njema.—Mdo. 4:29, 31; 5:42.

4 Usihofu Mazungumzo Yenye Kuvunja Moyo: Maoni ya watu kwa ujumla au uchongezi wa hadharani huenda ukatuogofya. Hata hivyo, kumbuka walivyosema kwa ujasiri Petro na mitume wale wengine mbele ya Sanhedrini, kama ilivyorekodiwa kwenye Matendo 5:29-32. Kama vile alivyokubali Gamalieli mwalimu wa Sheria, kazi ya Mungu haiwezi kupinduliwa. Haitimizwi kwa nguvu zetu wenyewe. Kazi hii kuu inategemezwa na Mungu, na ni yeye tu awezaye kuitimiza!—Zek. 4:6.

5 Na tumwombe sana Yehova kila siku atupe roho yake itusaidie tutangaze habari njema kwa bidii. Na tuseme kama Yeremia, kwamba ujumbe wa Ufalme ni kama moto uwakao ndani ya mifupa yetu. (Yer. 20:9) Hatuwezi kunyamaza!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki