Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/09 uku. 3
  • Watafute Wanaostahili

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watafute Wanaostahili
  • Huduma ya Ufalme—2009
  • Habari Zinazolingana
  • Njia za Kuhubiri Habari Njema
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Je, Una Eneo la Kibinafsi?
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Timiza Huduma Yako Kikamili
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Je, Utanufaika kwa Kuwa na Eneo la Kibinafsi?
    Huduma ya Ufalme—2013
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2009
km 9/09 uku. 3

Watafute Wanaostahili

1. Tunaonyeshaje uthamini kwa pendeleo la kushiriki katika huduma?

1 Wakati wa huduma yake, Yesu alijitahidi sana kuwafariji wapole kwa habari njema. (Isa. 61:1, 2) Leo, sisi tukiwa mabalozi na wajumbe badala ya Kristo, tuna pendeleo la kumwiga kwa kuwatafuta kwa bidii na kwa makini watu wanaostahili katika eneo letu.—Mt. 10:11; 2 Kor. 5:20.

2. Paulo alionyeshaje kwamba alikuwa tayari kuhubiri katika maeneo tofauti-tofauti, na matokeo yalikuwa nini?

2 Uwe Tayari Kuhubiri Katika Maeneo Tofauti-Tofauti: Mtume Paulo alikuwa na desturi ya kwenda kwanza katika sinagogi ili kuwahubiria Wayahudi na watu wa mataifa waliokuwa wafuasi wa dini ya Kiyahudi. (Mdo. 14:1) Huko Filipi, yeye na Sila walienda kuwatafuta watu mahali ambapo ‘walifikiri ni mahali pa sala.’ Walianza kuwahubiria wanawake waliokuwa wamekusanyika, na upesi mmoja wao aitwaye Lidia akakubali kweli.—Mdo. 16:12-15.

3. Mbali na kuhubiri nyumba kwa nyumba, tunaweza kuhubiri katika maeneo gani mengine?

3 Mbali na kuhubiri nyumba kwamba nyumba, je, unaweza pia kuwahubiria watu kwenye vituo vya usafiri, bustani, ofisi, pembe za barabara zenye watu wengi, maeneo ya biashara, na maduka katika eneo lenu? Labda unaweza kuwahubiria kwa barua au kwa simu watu wanaoishi katika majengo ambayo watu wasioishi humo hawaruhusiwi kuingia. Ukiwa mwenye utambuzi na tayari kubadilika kulingana na hali ya eneo lenu, unaweza kuwa “na mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana.”—1 Kor. 15:58.

4. Tunaweza kufanya nini ikiwa kutaniko letu halina eneo la kutosha?

4 Wahubiri wengi wamepanua huduma yao kwa kuhamia kutaniko lingine katika nchi yao au nchi ya kigeni. Wengine wamejifunza lugha mpya ili kuwahubiria watu ambao wametoka nchi nyingine.

5. Tunapaswa kuwa na maoni gani kuhusu nyakati tunamoishi, nasi tunapaswa kuazimia kufanya nini?

5 Sote tunapaswa kukumbuka kwamba “shamba ni ulimwengu.” (Mt. 9:37; 13:38) Kwa kuwa mwisho wa ulimwengu huu mwovu unakaribia, kila mmoja wetu anapaswa kufikiria kwa uzito hali yake, nafasi na vipawa vyake, na pia uwezekano wa kupanua huduma yake. Yehova anatuhakikishia kwamba tukitanguliza mambo ya Ufalme, atabariki jitihada zetu za kupanua huduma yetu.—Mt. 6:33.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki