Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/10 uku. 2
  • Kazi Muhimu Zaidi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kazi Muhimu Zaidi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Unaweza Kushiriki Katika Kazi ya Kufanya Wanafunzi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Tunahitaji Kudumisha Bidii Katika Huduma
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Iga Bidii ya Yesu ya Kuhubiri
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2025
  • Kujulisha Jina la Mungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2010
km 3/10 uku. 2

Kazi Muhimu Zaidi

1. Kuithamini sana huduma kutatusukuma tujidhabihu katika njia gani?

1 Kwa nini mara nyingi tunahimizwa kutumia wakati, nguvu, na mali zetu katika huduma? Kwa sababu hii ndiyo kazi muhimu zaidi. Tunapozingatia matokeo mengi mazuri ya huduma, tunachochewa kushiriki hata zaidi katika kazi hii ambayo haitarudiwa tena.—Mdo. 20:24.

2. Ni katika njia gani ambazo kazi yetu ya kuhubiri inasaidia kulitakasa jina la Yehova?

2 Huduma Hutakasa Jina la Yehova: Kazi ya kuhubiri inaonyesha kwamba Ufalme wa Yehova chini ya utawala wa Kristo Yesu, utaondoa serikali za wanadamu na kuleta suluhisho la matatizo yote ya binadamu. (Mt. 6:9, 10) Hivyo, Yehova hutukuzwa kwa sababu ni yeye tu anayeweza kutuokoa na dhambi na kifo. (Isa. 25:8; 33:24) Kwa kuwa sisi tunaitwa kwa jina lake, huenda watu wanaotazama mwenendo wetu na bidii yetu ya kuhubiri wakasukumwa kumtukuza Yehova. (1 Pet. 2:12) Inafurahisha sana kulijulisha jina la Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, kotekote duniani!—Zab. 83:18.

3. Watu wanaokubali ujumbe wa Ufalme wanafurahia baraka zipi?

3 Huduma Huokoa Uhai: Yehova “hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba.” (2 Pet. 3:9) Hata hivyo, watu wasipofundishwa, watajuaje maoni ya Yehova kuhusu mwenendo unaofaa na usiofaa? (Yona 4:11; Rom. 10:13-15) Watu wanafurahia maisha bora wanapoikubali habari njema na kuacha mazoea mabaya. (Mika 4:1-4) Zaidi ya hayo, wanapata tumaini lenye shangwe la uzima wa milele. Tunapohubiri na kufundisha kwa bidii, tunaokoa uhai wetu na uhai wa wale wanaotusikiliza. (1 Tim. 4:16) Kazi hii muhimu inatupa daraka lenye kuheshimika sana!

4. Kwa nini tunapaswa kufanya yote tuwezayo katika kazi ya kuhubiri kuhusu Ufalme na kufanya wanafunzi?

4 Hivi karibuni, ulimwengu huu usio na haki utaharibiwa ghafula katika dhiki kuu. Wale wanaomwabudu Yehova wataokoka. Kwa hiyo, kuhubiri na kufanya wanafunzi ndiyo kazi muhimu na yenye faida zaidi leo. Acheni sote tuitangulize kazi ya kuhubiri maishani mwetu!—Mt. 6:33.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki