Je, Ni Lazima Ukatize?
Wanaposhiriki katika utumishi wa shambani, ni jambo la kawaida kwa wahubiri wengine kukatiza utumishi wao ufikapo wakati fulani, kwa mfano adhuhuri. Bila shaka, hali za wahubiri fulani huenda zikawalazimu wakatize huduma yao ya shambani wakati fulani hususa. Lakini, je, wewe hukatiza utumishi wako kwa sababu wengine katika kikundi hufanya hivyo au kwa kuwa ni desturi ya wahubiri katika eneo lenu kukatiza utumishi wao wa shambani ifikapo saa fulani? Je, unaweza kuongeza muda unaotumia katika huduma kwa dakika chache zaidi na kushiriki katika aina nyingine ya mahubiri ya hadharani, kama vile kutoa ushahidi barabarani? Je, unaweza kufanya ziara moja au mbili za kurudia unaporudi nyumbani? Fikiria kuhusu mambo mazuri utakayotimiza ikiwa utampata tena nyumbani angalau mtu mmoja anayependezwa au ikiwa utamwachia mpita njia magazeti! Ikiwa hatuna sababu za kukatiza utumishi, kuendelea kwa dakika chache zaidi ni njia rahisi ya kuongeza ‘dhabihu yetu ya sifa.’—Ebr. 13:15.