MAISHA YA MKRISTO
“Mungu Ni Msaidizi Wangu”
Kwenye Zaburi ya 52-59 Daudi anaeleza hisia zake kuhusu matatizo mbalimbali aliyokabili maishani mwake. Alimtumaini Yehova hata katika nyakati hizo ngumu. (Zb 54:4; 55:22) Pia, alimsifu Yehova kwa sababu ya neno Lake. (Zb 56:10) Je, tunasitawisha imani ya aina hiyo na kumtumaini Mungu kama Daudi? Je, tunatafuta mwongozo katika Neno la Mungu tunapokabili magumu? (Met 2:6) Ni mistari gani ya Biblia iliyokusaidia . . .
ulipokuwa umeshuka moyo?
ulipokuwa mgonjwa?
wengine walipokukosea?
ulipokabili mateso?