MAISHA YA MKRISTO
Utafanya Nini Katika Mwaka wa Ukame?
Tunahitaji kuwa na imani na kumtegemea Yehova sana. Kwa mfano, imani yenye nguvu katika Yehova hutusaidia kumtegemea tukiwa na uhakika kwamba atatulinda na kututunza. (Zb 23:1, 4; 78:22) Kadiri tunavyozidi kukaribia mwisho wa mfumo huu wa mambo, ndivyo tunavyotarajia kwamba Shetani atazidisha mashambulizi yake. (Ufu 12:12) Ni nini kitakachotusaidia?
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA UTAFANYA NINI KATIKA MWAKA WA UKAME? KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Kwa nini sisi ni kama “mti” unaotajwa kwenye Yeremia 17:8?
Taja aina moja ya “joto”?
“Mti” huo unaathiriwaje, na kwa nini?
Shetani anataka kuharibu nini?
Kwa nini sisi ni kama marubani wenye uzoefu?
Kwa nini tunapaswa kuendelea kumtumaini mtumwa mwaminifu na mwenye busara, na ushikamanifu wetu utajaribiwaje?
Kwa nini tunapaswa kuendelea kutegemea kanuni za Biblia hata tunapodhihakiwa na ulimwengu?